Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Damu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • ulianzishwa kwa ajili ya Mashahidi wa Yehova walio watu wazima kwa sababu dini yao inakataza kutiwa damu mishipani, sasa umeanza kutumiwa kwa ajili ya watoto wenye magonjwa ya moyo.”—Cardiovascular News, Februari 1984, uku. 5.

      Mtu Akisema—

      ‘Ninyi huwaacha watoto wenu wafe kwa sababu mnakataa kutiwa damu mishipani. Hilo ni jambo baya sana’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Lakini tunawaruhusu wapate matibabu kupitia mishipa—yaliyo salama. Sisi tunakubali matibabu kupitia mishipa yasiyoweza kuwaambukiza magonjwa kama vile UKIMWI, ugonjwa wa ini, na malaria. Tunataka matibabu bora zaidi kwa ajili ya watoto wetu, nami nina hakika mzazi yeyote mwenye upendo angetaka hivyo.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Mtu anapopoteza damu nyingi sana, kinachohitajiwa hasa ni kurudisha kiasi cha umajimaji. Bila shaka unajua kwamba zaidi ya asilimia 50 ya damu yetu ni maji; pia kuna zile chembe nyekundu na nyeupe, na kadhalika. Mtu anapopoteza damu nyingi, mwili wenyewe hutokeza kiasi kikubwa cha chembe za damu na kuharakisha kufanyizwa kwa chembe mpya. Lakini kiasi cha kutosha cha umajimaji ndicho kinachohitajiwa. Vitu vya kuongeza kiasi cha plazima ambavyo havina damu vyaweza kutumiwa kujazia uhitaji huo, nasi tunavikubali.’ (2) ‘Vitu vya kuongeza kiasi cha plazima vimetumiwa kwa maelfu ya watu, kukiwa na matokeo bora sana.’ (3) ‘Jambo lililo muhimu zaidi kwetu ni lile ambalo Biblia yenyewe inasema katika Matendo 15:28, 29.’

      Au unaweza kusema: ‘Naelewa maoni yako. Huenda unawazia mtoto wako mwenyewe akiwa katika hali hiyo. Tukiwa wazazi tungefanya kila tuwezalo ili kumlinda mtoto wetu, sivyo? Basi ikiwa mtu kama wewe na mimi tungekataa aina fulani ya matibabu kwa ajili ya mtoto wetu, kwa hakika lazima kungekuwa na sababu ya kukataa.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Je, unafikiri kwamba huenda wazazi fulani wakawa wanaongozwa na yale yanayosemwa na Neno la Mungu hapa katika Matendo 15:28, 29?’ (2) ‘Basi swali ni, Je, tuna imani ya kutosha kufanya mambo ambayo Mungu anaamuru?’

      ‘Ninyi hamkubali kutiwa damu mishipani’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Magazeti yamechapisha habari juu ya visa fulani ambavyo ilionekana kwamba Mashahidi wanaweza kufa ikiwa hawakubali damu. Je, hayo ndiyo maoni yako? . . . Kwa nini sisi tumechukua msimamo huo?’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Je, unampenda mke (mume) wako vya kutosha hata ungekuwa tayari kufa kwa ajili yake? . . . Pia kuna watu walio tayari kufa kwa ajili ya nchi yao, nao huonwa kuwa mashujaa, sivyo? Lakini kuna mtu mkuu kuliko mtu yeyote au kitu chochote hapa duniani, naye ni Mungu. Je, wewe ungekuwa tayari kufa kwa sababu unampenda na kwa sababu ya ushikamanifu wako kwa utawala wake?’ (2) ‘Kwa kweli, suala linalohusika ni ushikamanifu kwa Mungu. Neno la Mungu ndilo linalotuambia tujiepushe na damu. (Mdo. 15:28, 29)’

      Au unaweza kusema: ‘Kuna mambo mengi yaliyo ya kawaida sana leo na ambayo Mashahidi wa Yehova huyaepuka—kwa mfano, uwongo, uzinzi, wizi, kuvuta tumbaku, na kama ulivyotaja, kutumia damu. Kwa nini? Kwa sababu maisha yetu yanaongozwa na Neno la Mungu.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Je, unajua kwamba Biblia inasema tunapaswa ‘kujiepusha na damu’? Ningependa kukuonyesha jambo hilo. (Mdo. 15:28, 29)’ (2) ‘Labda unakumbuka kwamba Mungu aliwaambia wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Hawa, kwamba wangeweza kula kutokana na kila mti uliokuwa katika Edeni isipokuwa mti mmoja. Lakini hawakutii, wakala tunda walilokatazwa, wakapoteza kila kitu. Walikosa hekima. Bila shaka, leo hakuna mti ulio na tunda lililokatazwa. Lakini baada ya Gharika ya siku za Noa, Mungu aliwapa tena wanadamu amri moja. Wakati huo ilihusu damu. (Mwa. 9:3, 4)’ (3) ‘Kwa hiyo swali ni, Je, tunamwamini Mungu? Tukimtii, tutakuwa na tumaini la kuishi milele maisha makamilifu chini ya Ufalme wake. Hata tukifa, yeye anatuhakikishia ufufuo.’

      ‘Namna gani daktari akisema, “Utakufa usipotiwa damu mishipani”?’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Ikiwa hali ni mbaya sana hivyo, je, daktari huyo anaweza kukuhakikishia kwamba mgonjwa huyo hatakufa akitiwa damu?’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Lakini kuna mtu anayeweza kumrudishia mtu uhai, naye ni Mungu. Je, hukubali kwamba, unapokaribia kufa, kuamua kumwacha Mungu kwa kuvunja sheria yake kungekuwa kosa? Kwa kweli mimi ninamwamini Mungu. Namna gani wewe? Neno lake linawaahidi ufufuo wale wanaomwamini Mwanawe. Je, wewe unaamini hivyo? (Yoh. 11:25)’

      Au unaweza kusema: ‘Huenda ikamaanisha kwamba yeye mwenyewe hajui jinsi ya kushughulikia kisa hicho bila kutumia damu. Inapowezekana, sisi hujaribu kumwelekeza kwa daktari ambaye amepata ujuzi unaohitajiwa, au tunamwendea daktari mwingine.’

  • Dawa za Kulevya
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Dawa za Kulevya

      Maana: Kuna maana mbalimbali za neno “dawa.” Katika sehemu hii, tutazungumzia dawa za kulevya, ambazo si vyakula, bali ni vitu vinavyobadili tabia ambavyo havionwi kuwa vya lazima kitiba. Watu huvitumia kujaribu kuepuka matatizo ya maisha, ili kupata hisia kama ya ndoto, au hali ya kuhisi vizuri au kusisimuka.

      Je, kwa kweli Biblia inakataza kutumia dawa za kulevya ili kupata raha?

      Biblia haitaji kwa jina vitu kama heroini, kokeini, LSD, PCP, bangi, na tumbaku. Lakini inatoa miongozo inayohitajiwa ili tujue jambo la kufanya na la kuepuka ili tumpendeze Mungu. Vivyo hivyo, Biblia haisemi kwamba ni kosa kutumia bunduki kumuua mtu, lakini inakataza uuaji.

      Luka 10:25-27: “‘Nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?’ . . . ‘“Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote,” na, “jirani yako kama wewe mwenyewe.”’” (Je, kweli mtu anampenda Mungu kwa nafsi yake yote na akili yake yote ikiwa anatenda mambo yanayofupisha maisha yake bila sababu na kufanya akili zake zipumbazike? Je, anampenda jirani yake ikiwa anawaibia wengine ili aendeleze tabia yake ya kutumia dawa za kulevya?)

      2 Kor. 7:1: “Kwa kuwa tuna ahadi hizi [za Yehova kuwa Mungu na Baba yetu], acheni tujisafishe wenyewe kila unajisi wa mwili na roho, tukiukamilisha utakatifu katika kumwogopa Mungu.” (Lakini je, tunaweza kutarajia kukubaliwa na

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki