-
NafsiKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Je, mtu huendelea kuwa na fahamu baada ya roho kuuacha mwili?
Zab. 146:4: “Roho [Kiebrania, kutokana na ruʹach] yake hutoka, naye hurudi kwenye udongo wake; siku hiyo mawazo yake hupotea.” (VB [145:4] hutafsiri neno ruʹach kuwa “roho.” Tafsiri fulani husema “pumzi.”) (Ona pia Zaburi 104:29)
Imani ya Jumuiya ya Wakristo kuhusu nafsi isiyo na mwili, isiyoweza kufa ilitoka wapi?
“Wazo la Kikristo la nafsi ya kiroho iliyoumbwa na Mungu na kutiwa katika mwili wakati wa kutungwa kwa mimba ili kufanyiza mwanadamu kuwa mtu kamili lilitokana na falsafa ya Kikristo iliyositawi kwa muda mrefu. Ni kupitia Origen tu [aliyekufa karibu mwaka wa 254 W.K.] upande wa Mashariki na Mtakatifu Agustino [aliyekufa mwaka wa 430 W.K.] upande wa Magharibi kwamba nafsi ilithibitishwa kuwa kitu cha kiroho na wazo la kifalsafa likafanyizwa kuhusu asili yake. . . . Fundisho lake [la Agustino] . . . lilikuwa na mambo mengi (kutia ndani makosa fulani) yaliyotoka kwa Plato.”—New Catholic Encyclopedia (1967), Buku la 13, uku. 452, 454.
“Wazo la kutoweza kufa lilitokana na Wagiriki, lakini tumaini la ufufuo lilitokana na Wayahudi. . . . Baada ya ushindi wa Aleksanda, mwishowe dini ya Kiyahudi ilichukua mawazo ya Kigiriki.”—Dictionnaire Encyclopédique de la Bible (Valence, Ufaransa; 1935), iliyohaririwa na Alexandre Westphal, Buku la 2, uku. 557.
“Kutoweza kufa kwa nafsi ni wazo la Kigiriki lililofanyizwa katika madhehebu ya kale ya kifumbo na kupanuliwa na Plato mwanafalsafa.”—Presbyterian Life, Mei 1, 1970, uku. 35.
“Je, tunaamini kwamba kuna kitu kama kifo? . . . Je, kifo si kutengana kwa nafsi na mwili? Na kufa ndio ukamilisho wa hilo; wakati nafsi inapoishi peke yake, na inapofunguliwa kutoka katika mwili na mwili unapofunguliwa kutoka katika nafsi, je, hicho si kifo? . . . Na je, nafsi inakubali kifo? Hapana. Basi nafsi haiwezi kufa? Ndiyo.”—“Phaedo” ya Plato, Sehemu ya 64, 105, kama ilivyochapishwa katika Great Books of the Western World (1952), kilichohaririwa na R. M. Hutchins, Buku la 7, uku. 223, 245, 246.
“Tumeona kwamba, lile tatizo la kutoweza kufa liliwavutia sana wanatheolojia wa Babiloni. . . . Watu wala viongozi wa mafundisho ya kidini hawakupata kamwe kuukabili uwezekano wa kutoweka kabisa kwa kile ambacho hapo kwanza kiliumbwa. Kifo kilikuwa ni njia ya kuingia katika maisha mengine.”—The Religion of Babylonia and Assyria (Boston, 1898), M. Jastrow, Jr., uku. 556.
Ona pia ukurasa wa 102-104, chini ya kichwa “Kifo.”
-
-
NdoaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Ndoa
Maana: Muungano wa mwanamume na mwanamke ili kuishi pamoja wakiwa mume na mke kulingana na kiwango kilichowekwa katika Maandiko Matakatifu. Ndoa ni mpango wa Mungu. Inawezesha kuwepo uhusiano wa karibu sana kati ya mume na mke pamoja na hisia ya usalama kwa sababu kuna upendo na kwa sababu ya wajibu wa kibinafsi ambao umefanywa na kila mmoja wa wenzi hao. Alipokuwa akiianzisha ndoa, Yehova alifanya hivyo ili kumwandalia mwanamume mwenzi wa karibu ambaye angekuwa kikamilisho chake na pia kuanzisha njia ambayo wanadamu wangeweza kuzaana katika mpango wa familia. Inapohitajiwa, kuandikisha kisheria ndoa inayokubalika katika kutaniko la Kikristo ni takwa.
Je, ni muhimu kufunga ndoa kupatana na matakwa ya kisheria?
Tito 3:1: “Endelea kuwakumbusha wajitiishe na kuzitii serikali na mamlaka zikiwa watawala.” (Watu wanapotii maagizo hayo, kila mmoja katika muungano huo hawezi kushutumiwa, nao watoto hawashutumiwi kama watoto ambao wazazi wao hawajafunga ndoa. Pia, kuandikisha ndoa kisheria hulinda haki za mali za familia, ikiwa mmoja wa wenzi hao atakufa.)
Ebr. 13:4: “Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kiwe bila unajisi, kwa maana Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.” (Kufunga ndoa kisheria hutimiza sehemu muhimu katika kuwa na ndoa inayoonwa kuwa ‘yenye kuheshimiwa.’ Tunapoeleza maana ya maneno “uasherati” na “uzinzi,” lazima tukumbuke yanayosemwa katika andiko la Tito 3:1, lililotangulia kunukuliwa.)
-