Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Roho ya Ulimwengu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • “Mungu wa mfumo huu wa mambo,” Shetani Ibilisi, huchochea matendo yote mbalimbali ambayo hupotosha mwelekeo wa ibada ambao Mungu alimpa mwanadamu. (2 Kor. 4:4) Watawala fulani wametendewa kama miungu. (Mdo. 12:21-23) Mamilioni ya watu husujudia sanamu. Mamilioni zaidi huwatukuza waigizaji na wanamichezo mashuhuri. Mara nyingi sherehe huwapa wanadamu fulani heshima wasiyostahili. Roho hii imeenea sana hivi kwamba wale wanaompenda Yehova kikweli na wanaotaka kumtolea ibada ya pekee wanahitaji kukaa macho kila siku ili wajiepushe na uvutano wa roho hiyo.

  • Sabato
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Sabato

      Maana: Neno Sabato limetokana na neno la Kiebrania sha·vathʹ, linalomaanisha “pumzika, koma, acha.” Mfumo wa sabato ulioandikwa katika Sheria ya Musa ulitia ndani siku ya Sabato ya kila juma, siku kadhaa za ziada zilizotajwa waziwazi katika kila mwaka, mwaka wa saba, na mwaka wa hamsini. Sabato ya kila juma ya Wayahudi, siku ya saba ya juma lao la kalenda, inaanza wakati wa kutua kwa jua siku ya Ijumaa mpaka kutua kwa jua siku ya Jumamosi. Watu wengi wanaojiita Wakristo wameshika tangu zamani Jumapili kuwa siku yao ya pumziko na ya ibada; wengine wameshikamana na siku iliyowekwa kando katika kalenda ya Kiyahudi.

      Je, Wakristo wana wajibu wa kushika siku ya sabato ya kila juma?

      Kut. 31:16, 17: “Wana wa Israeli lazima waishike sabato, ili kuitimiza sabato katika vizazi vyao. Ni agano mpaka wakati usio na kipimo [“agano la milele,” UV]. Kati yangu na wana wa Israeli ni ishara mpaka wakati usio na kipimo.” (Ona kwamba kushika sabato kulikuwa ishara kati ya Yehova na Israeli; haingekuwa hivyo ikiwa watu wengine wote wangekuwa na wajibu wa kushika Sabato. Neno la Kiebrania lililotafsiriwa “milele” katika UV ni ‛oh·lamʹ, ambalo kwa msingi linamaanisha kipindi cha wakati ambacho, kwa sasa, hakina kipimo au kimefichwa lakini ni cha muda mrefu. Hicho kinaweza kumaanisha milele, lakini si lazima kiwe hivyo. Katika Hesabu 25:13 neno lilelile la Kiebrania linatumiwa kuhusu ukuhani, ambao baadaye ulikoma, kulingana na Waebrania 7:12.)

      Rom. 10:4: “Kristo ndiye mwisho wa Sheria, ili kila mtu anayeonyesha imani awe na uadilifu.” (Kushika sabato kulikuwa sehemu ya Sheria hiyo. Mungu alimtumia Kristo kuikomesha Sheria hiyo. Kupata msimamo wenye uadilifu mbele za Mungu kunategemea imani katika Kristo, wala si kushika sabato ya kila juma.) (Ona pia Wagalatia 4:9-11; Waefeso 2:13-16)

      Kol. 2:13-16: “[Mungu] alitusamehe kwa fadhili makosa yetu yote na kuifuta kabisa ile hati iliyoandikwa kwa mkono kutupinga, iliyokuwa na amri na iliyokuwa ikitupinga sisi . . . Kwa hiyo mtu yeyote asiwahukumu ninyi katika kula na kunywa au kuhusu sherehe au kuhusu kushika mwezi mpya au sabato.” (Ikiwa mtu alikuwa chini ya Sheria ya Musa na alihukumiwa kuwa na hatia ya kuitia Sabato unajisi, yeye alipaswa kupigwa mawe na kutaniko zima mpaka afe, kulingana na Kutoka 31:14 na Hesabu 15:32-35. Wengi wanaosema kwamba watu washike sabato wana sababu ya kufurahi kwamba sisi hatuko chini ya Sheria hiyo. Kulingana na andiko ambalo limenukuliwa hapa, si lazima mtu ashike sabato ambayo Waisraeli waliagizwa washike ili akubaliwe na Mungu.)

      Jumapili ilikujaje kuwa siku kuu ya ibada kwa sehemu kubwa ya Jumuiya ya Wakristo?

      Ijapokuwa Kristo alifufuliwa siku ya kwanza ya juma (ambayo sasa huitwa Jumapili), Biblia haina agizo la kutenga siku hiyo ya juma kuwa takatifu.

      “Kutunzwa kwa jina la kale la Kipagani ‘Dies Solis,’ au ‘Siku ya Jua,’ kwa ajili ya sikukuu ya Kikristo ya kila juma, kwa kadiri kubwa, ni kwa sababu ya muungano wa Upagani na [lile linaloitwa] wazo la Kikristo ambalo kwake siku ya kwanza ya juma ilipendekezwa na Konstantino [kwa amri mwaka wa 321 W.K.] kwa raia zake, Wapagani na Wakristo pia, kuwa ndiyo ‘siku ya kuheshimiwa ya Jua.’ . . . Huo ulikuwa mtindo wake wa kuzipatanisha dini zenye kutofautiana za Milki chini ya shirika moja la ujumla.”—Lectures on the History of the Eastern Church (New York, 1871), A. P. Stanley, uku. 291.

      Je, takwa la kushika sabato lilitolewa kwa Adamu na hivyo kufanywa liwe lazima kwa wazao wake wote?

      Yehova Mungu alipumzika kuhusiana na kazi zake za uumbaji duniani baada ya kuitayarisha dunia kuwa makao ya wanadamu. Hilo limeandikwa katika Mwanzo 2:1-3. Lakini hakuna lolote katika maandishi ya Biblia linalosema kwamba Mungu alimwagiza Adamu ashike siku ya saba ya kila juma kuwa sabato.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki