-
SabatoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Unaweza kujibu hivi: ‘Jibu langu litategemea sabato unayomaanisha. Je, unajua kwamba Biblia inasema kuhusu sabato kadhaa? . . . Mungu aliwapa Wayahudi sheria za sabato. Lakini unajua kwamba Biblia inasema kuhusu sabato fulani tofauti ambayo Wakristo wanapaswa kushika?’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Sisi hatushiki siku moja kila juma kuwa Sabato kwa sababu Biblia inasema kwamba takwa hilo ‘lingeondolewa mbali.’ (2 Kor. 3:7-11; ona maelezo kuhusu jambo hilo katika ukurasa wa 253, 254.)’ (2) ‘Lakini kuna sabato ambayo sisi hushika kwa ukawaida. (Ebr. 4:4-11; ona ukurasa wa 254, 255.)’
-
-
SalaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Sala
Maana: Maneno ya kuabudu, yanayoweza kusemwa kwa sauti kubwa au kimya-kimya katika mawazo ya mtu, yanayoelekezwa kwa Mungu wa kweli au kwa miungu ya uwongo.
Je, wewe unaona, kama wengine, kwamba sala zako hazijibiwi?
Mungu anapenda kusikiliza sala za nani?
Zab. 65:2; Mdo. 10:34, 35: “Ee msikiaji wa sala, kwako wewe watu wote wenye mwili watakuja.” “Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mtu ambaye anamwogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.” (Taifa, rangi ya ngozi, wala hali za kiuchumi za mtu si muhimu kuhusiana na jambo hili. Lakini jambo muhimu ni kile kinachouchochea moyo wa mtu na njia yake ya maisha.)
Luka 11:2: “Wakati wowote mnaposali, semeni, ‘Baba, jina lako na litakaswe.’” (Je, unatoa sala zako kwa Baba, ambaye Biblia inasema jina lake ni Yehova? Au, badala yake unatoa sala zako kwa “watakatifu”?)
Yoh. 14:6, 14: “Yesu akamwambia: ‘Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna anayekuja kwa Baba ila kupitia kwangu. Mkiomba jambo lolote katika jina langu, nitalifanya.’” (Je, wewe husali katika jina la Yesu Kristo, ukitambua kwamba ukiwa mwanadamu mwenye dhambi unahitaji kutetewa?)
1 Yoh. 5:14: “Na huu ndio uhakika ambao tunao kwake, kwamba, hata tukiomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye hutusikia.” (Hata hivyo, ili kuwa na uhakika huo, ni lazima kwanza ujue mapenzi ya Mungu. Kisha uhakikishe kwamba maombi yako yanapatana na mapenzi hayo.)
1 Pet. 3:12: “Macho ya Yehova yako juu ya waadilifu, na masikio yake yanaielekea dua yao; bali uso wa Yehova uko dhidi ya wale wanaotenda mambo mabaya.” (Je, umetenga wakati wa kujifunza yale ambayo Yehova anasema kupitia Neno lake kuhusu mambo ya uadilifu na mambo mabaya?)
1 Yoh. 3:22: “Chochote kile tunachoomba tunapokea kutoka kwake, kwa sababu tunazishika amri zake na tunafanya mambo yanayopendeza machoni pake.” (Je, kweli unatamani kumpendeza Mungu, na je, unajitahidi kutii amri zake ambazo tayari unazijua?)
Isa. 55:6, 7: “Mtafuteni Yehova, wakati anapoweza kupatikana. Mwiteni akiwa bado yupo karibu. Mtu mwovu aiache njia yake, na mtu mwenye madhara ayaache mawazo yake; naye arudi kwa Yehova, ambaye atamwonyesha rehema, na kwa Mungu wetu, kwa maana atasamehe kwa njia kubwa.” (Kwa rehema, Yehova anawaalika hata watu ambao wametenda mambo mabaya wamwombe katika sala. Lakini, ili wapate kibali cha Mungu, ni lazima watubu kwa unyoofu njia zao na mawazo yao mabaya na kubadili mwenendo wao.)
Ni nini kinachoweza kumfanya Mungu asikubali sala za mtu?
Mt. 6:5: “Wakati mnaposali, msiwe kama wanafiki; kwa sababu wanapenda kusali wakiwa wamesimama katika masinagogi na kwenye pembe za njia pana ili waonekane na watu. Kwa kweli ninawaambia ninyi, Wanapata thawabu yao kwa ukamili.” (Pia Luka 18:9-14)
Mt. 6:7: “Mnaposali, msiseme mambo yaleyale tena na tena, kama vile watu wa mataifa wanavyofanya, kwa maana wao huwaza watasikiwa kwa kutumia maneno mengi.”
Met. 28:9: “Anayegeuzia mbali sikio lake asiisikie sheria [ya Mungu]—hata sala yake ni chukizo.”
Mika 3:4: “Wakati huo watamwomba Yehova msaada, lakini hatawajibu. Naye atauficha uso wake kutoka kwao wakati huo, kulingana na walivyotenda ubaya kwa matendo yao.”
Yak. 4:3: “Mnaomba, na bado hampokei, kwa sababu mnaomba kwa kusudi baya, ili mvitumie kwa tamaa zenu za mwili.”
Isa. 42:8, ZSB; Mt. 4:10, UV: “Mimi ni BWANA [“Yehova,” NW], ndilo jina langu; na utukufu wangu sitamupa mwingine, wala sanamu ya kuchonga sifa zangu.” “Msujudie Bwana Mungu [“Yehova Mungu,” NW] wako, umwabudu yeye peke yake.” (Pia Zaburi 113:4-8 [115:4-8], VB) (Sala ni namna ya ibada. Ukisali mbele ya vitu vya kuchongwa, au sanamu, je, hilo litampendeza Mungu?)
-