Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Vipindi vya Wakati
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • KUHESABU ZILE “NYAKATI SABA”

      “Nyakati saba” = 7 x 360 = miaka 2,520

      “Wakati” wa Kibiblia, au mwaka = 12 x siku 30 = 360. (Ufu. 11:2, 3; 12:6, 14)

      Katika utimizo wa “nyakati saba” kila siku hulingana na mwaka mmoja. (Eze. 4:6; Hes. 14:34)

      Mapema Oktoba, 607 K.W.K., hadi Desemba 31, 607 K.W.K. = mwaka 1⁄4

      Januari 1, 606 K.W.K., hadi Desemba 31, 1 K.W.K. = miaka 606

  • Wanawake
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Wanawake

      Maana: Wanadamu wa jinsia ya kike ambao ni watu wazima. Katika Kiebrania, neno mwanamke ni ’ish·shahʹ, ambalo kihalisi humaanisha “mwanadamu wa kike.”

      Je, Biblia inawashushia wanawake heshima au inawatendea kana kwamba ni watu duni?

      Mwa. 2:18: “Yehova Mungu akaendelea kusema: ‘Si vema huyo mwanamume aendelee kuwa peke yake. Nitamfanyia msaidizi, awe kikamilisho chake.’” (Katika andiko hilo, Mungu hasemi kwamba mwanamume ni mtu bora kuliko mwanamke. Badala yake, Mungu alionyesha kwamba mwanamke angekuwa na sifa ambazo zingekamilisha zile za mwanamume katika mpango wa Mungu. Kikamilisho ni kimoja cha vitu viwili vinavyokamilishana. Basi wanawake kwa ujumla hutokeza katika sifa na uwezo fulani; wanaume nao hutokeza katika sifa nyingine. Linganisha na 1 Wakorintho 11:11, 12.)

      Mwa. 3:16: “[Mungu] akamwambia mwanamke: ‘ . . . tamaa yako itakuwa kwa mume wako, naye atakutawala.’” (Tangazo hilo lililotolewa baada ya Adamu na Hawa kufanya dhambi halikumaanisha jambo ambalo wanaume wanapaswa kufanya bali lilimaanisha jambo ambalo Yehova alijua mapema kwamba wanaume wangefanya kwa kuwa sasa ubinafsi ulikuwa umeingia katika maisha ya wanadamu. Masimulizi kadhaa ya Biblia yaliyoandikwa baada ya tukio hilo husema kuhusu hali zenye huzuni sana zilizositawi kwa sababu ya wanaume kuwatawala wanawake kwa ubinafsi. Lakini Biblia haisemi kwamba Mungu alikubali mwenendo huo wala haisemi kwamba huo ni mfano wa kufuatwa na wengine.)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki