-
Kusema kwa LughaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Hata hivyo, Biblia inaonyesha muda ambao ‘zawadi ya lugha’ ingekuwa sehemu ya maisha ya Wakristo. Kulingana na maandishi, watu walipokea zawadi hiyo na zawadi nyingine za roho kwa kuwekewa mikono na mitume wa Yesu Kristo au mitume hao wakiwapo. (Mdo. 2:4, 14, 17; 10:44-46; 19:6; ona pia Mdo. 8:14-18.) Basi, baada ya kufa kwao na wakati watu waliokuwa wamepokea zawadi hizo kwa njia hiyo walipokufa, zawadi za kimuujiza zinazotokana na utendaji wa roho ya Mungu bila shaka zilikoma. Maoni hayo yanapatana na kusudi la zawadi hizo kama ilivyoandikwa katika Waebrania 2:2-4.
Je, andiko la Marko 16:17, 18 (UV) linaonyesha kwamba uwezo wa ‘kusema kwa lugha mpya’ ungekuwa ishara ya kuwatambulisha waamini?
Inafaa kukumbuka kwamba mistari hiyo haitaji tu ‘kusema kwa lugha mpya’ bali pia kushika nyoka na kunywa sumu inayoua. Je, wote ‘wanaosema kwa lugha’ wanawatia watu moyo wafanye mambo hayo pia?
Ili kupata maelezo kuhusu sababu zinazowafanya wasomi wengine wa Biblia wasiikubali mistari hiyo, ona ukurasa wa 357, 358, chini ya kichwa, “Uponyaji.”
Mtu Akisema—
‘Je, unaamini kusema kwa lugha?’
Unaweza kujibu hivi: ‘Mashahidi wa Yehova husema lugha nyingi, lakini sisi hatusemi kwa msisimuko katika “lugha zisizojulikana.” Lakini hebu nikuulize, Je, unaamini kwamba ‘kusema kwa lugha’ kunakofanywa leo kunafanana na kule kulikofanywa na Wakristo wa karne ya kwanza?’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Hapa kuna habari fulani za kulinganisha ambazo zimenipendeza sana. (Labda tumia habari katika ukurasa wa 121, 122.)’
Au unaweza kusema: ‘Tunaamini kwamba Wakristo wa karne ya kwanza “walisema kwa lugha” na kwamba hilo lilitimiza kusudi hususa wakati huo. Je, unajua kusudi hilo lilikuwa nini?’ Kisha labda ongeza hivi: (1) ‘Kulikuwa ishara ya kwamba Mungu ameikataa ibada ya Wayahudi na kulikubali kutaniko la Kikristo lililoanzishwa hivi karibuni. (Ebr. 2:2-4)’ (2) ‘Ilikuwa njia nzuri ya kueneza habari njema katika mataifa yote kwa muda mfupi. (Mdo. 1:8)’
-
-
KutesekaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kuteseka
Maana: Jambo linalompata mtu anapokuwa na maumivu au taabu. Huenda kuteseka kukawa kwa kimwili, kiakili, au kihisia-moyo. Mambo mengi yanaweza kusababisha kuteseka; kwa mfano, madhara yanayotokana na vita na pupa ya kibiashara, udhaifu unaorithiwa, ugonjwa, misiba, “misiba ya asili,” mambo mabaya ambayo wengine husema au kufanya, kusumbuliwa na pepo, kujua msiba unaokaribia, au upumbavu wa mtu mwenyewe. Kuteseka kunakotokana na sababu hizo mbalimbali kutazungumziwa hapa. Hata hivyo, huenda pia mtu akateseka kwa sababu anawahurumia watu wengine walio katika hali mbaya au akateseka kwa sababu ya kuwaona watu wakitenda mambo yanayomvunjia Mungu heshima.
-