Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mbingu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • “Umati mkubwa mbinguni” unaotajwa katika Ufunuo 19:1, 6 si sawa na ule “umati mkubwa” wa Ufunuo 7:9. Wale walio mbinguni hawasemwi kuwa ‘wametoka katika mataifa yote’ wala hawamhesabii Mwana-Kondoo wokovu wao; wao ni malaika. Maneno “umati mkubwa” yanatumiwa katika miktadha katika Biblia.—Marko 5:24; 6:34; 12:37.

      Wale wanaoenda mbinguni watafanya nini huko?

      Ufu. 20:6: “Watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala wakiwa wafalme pamoja naye ile miaka elfu.” (Ona pia Danieli 7:27)

      1 Kor. 6:2: “Hamjui kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu?”

      Ufu. 5:10: “Ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu, nao watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia.”

      Ni nani anayewachagua wale watakaoenda mbinguni?

      2 The. 2:13, 14: “Tuna wajibu wa kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, akina ndugu mnaopendwa na Yehova, kwa sababu Mungu aliwachagua ninyi tangu mwanzo kwa ajili ya wokovu kwa kuwatakasa ninyi kwa roho na kwa imani yenu katika kweli. Kwa lengo hili aliwaita ninyi kupitia habari njema tunayoitangaza, kwa kusudi la kujipatia utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.”

      Rom. 9:6, 16: “Si wote wanaotokana na Israeli ni ‘Israeli’ kikweli.   . . . Haitegemei yule anayetaka wala yule anayekimbia, bali hutegemea Mungu, aliye na rehema.”

  • Misa
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Misa

      Maana: Kama inavyoelezwa na Kundi Takatifu la Ibada za Kanisa Katoliki, Misa ni “—Dhabihu ambayo katika hiyo Dhabihu ya Msalaba inadumishwa;—Ukumbusho wa kifo na ufufuo wa Bwana, aliyesema ‘fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu’ (Luka 22:19);—Karamu takatifu ambapo, kupitia ushirika wa Mwili na Damu ya Bwana, Watu wa Mungu hushiriki faida za Dhabihu ya Pasaka, hufanya upya Agano Jipya ambalo Mungu amefanya pamoja na wanadamu mara moja kwa wakati wote kupitia Damu ya Kristo, na katika imani na tumaini hutangulia kuonyesha na kutarajia karamu ya mwisho katika ufalme wa Baba, wakitangaza kifo cha Bwana ‘hata ajapo.’” (Eucharisticum Mysterium, Mei 25, 1967) Hiyo ndiyo njia ya Kanisa Katoliki ya kufanya kile wanachoelewa kwamba Yesu Kristo alifanya katika Mlo wa Jioni wa Bwana.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki