-
Yeremia 25:17Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
17 Basi nikakamata kile kikombe katika mukono wa Yehova na kufanya mataifa yote yenye Yehova alinituma kwao yakunywe:+
-
-
Yeremia 25:22Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
22 wafalme wote wa Tiro, wafalme wote wa Sidoni,+ na wafalme wa kisiwa chenye kuwa katika bahari;
-
-
Ezekieli 26:3Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
3 kwa hiyo, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Angalia, niko juu yako, Ee Tiro, na nitainua mataifa mengi ili yakushambulie, kama vile bahari inainua mawimbi yake.
-
-
Amosi 1:9, 10Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
9 Yehova anasema hivi:
‘Kwa sababu Tiro ameasi+ mara tatu (3), na kwa sababu ameasi mara ine (4), sitabadilisha hilo,
Kwa sababu walitia kikundi chote cha watu wenye walihamishwa katika mukono wa Edomu,
Na kwa sababu hawakukumbuka agano la ndugu.+
10 Kwa hiyo nitatuma moto juu ya ukuta wa Tiro,
Na utateketeza minara yake yenye ngome.’+
-