-
2 Mambo ya Nyakati 36:15, 16Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
15 Yehova Mungu wa mababu zao akaendelea kuwaonya kupitia wajumbe wake, akiwaonya tena na tena, kwa sababu alisikilia huruma watu wake na makao yake. 16 Lakini waliendelea kuchekelea wajumbe wa Mungu wa kweli,+ na walizarau maneno yake+ na kuchekelea manabii wake,+ mupaka wakati kasirani kali ya Yehova ilikuja juu ya watu wake,+ na hivyo hawangeweza kuponyeshwa.
-
-
Ezekieli 9:9, 10Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
9 Kwa hiyo akaniambia: “Kosa la nyumba ya Israeli na Yuda ni kubwa, kubwa sana.+ Inchi imejaa umwangaji wa damu,+ na muji umejaa upotovu.+ Kwa maana wanasema, ‘Yehova ameacha inchi hii, na Yehova haone.’+ 10 Lakini mimi, jicho langu halitasikitika; wala sitakuwa na huruma.+ Nitaleta matokeo ya njia yao juu ya kichwa chao wenyewe.”
-