Ezekieli
15 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, muti wa muzabibu uko tofauti namna gani na muti mwingine wowote ao tawi la miti ya pori? 3 Je, kipande cha muti huo kinaweza kutumiwa kufanyia kazi? Ao je, watu wanautumia kutengeneza kipande kidogo cha muti cha kuninginizia vyombo? 4 Angalia! Unatupwa katika moto ili ukuwe kuni, na moto unateketeza miisho yote mbili na kuunguza katikati. Je, sasa unafaa kwa kazi yoyote? 5 Hata wakati ulikuwa muzima, haungetumiwa kwa chochote. Je, itakuwa na mafaa yoyote wakati moto utakuwa umeuteketeza na kuunguza?”
6 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Kama vile mbao za muzabibu kati ya miti ya pori, yenye nimetoa ili ikuwe kuni kwa ajili ya moto, ni vile nitatendea wakaaji wa Yerusalemu.+ 7 Nimekunja uso wangu juu yao. Wameponyoka kutoka katika moto, lakini moto utawateketeza. Na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova wakati nitakunja uso wangu juu yao.’”+
8 “‘Na nitafanya inchi ikuwe ukiwa+ kwa sababu wametenda kwa kukosa uaminifu,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”