Isaya
16 Mutume kondoo-dume kwa mutawala wa inchi,
Kutoka Sela kupitia jangwa,
Mupaka kwenye mulima wa binti ya Sayuni.
2 Kama ndege mwenye alifukuzwa katika chicha yake,*+
Ni vile mabinti wa Moabu watakuwa kwenye nafasi za kuvukia za Arnoni.+
3 “Mutoe shauri, mutimize uamuzi.
Fanya kivuli chako cha katikati ya muchana kikuwe kama usiku.
Ficha wenye walisambazwa na usitoe wale wenye kukimbia.
4 Acha watu wangu wenye walisambazwa wakae ndani yako, Ee Moabu.
Ukuwe mahali pao pa kujificha kwa sababu ya mwenye kuharibu.+
Mukandamizaji atafikia mwisho wake,
Uharibifu utafikia mwisho,
Na wale wenye kukanyanga-kanyanga wengine wataharibiwa kutoka katika dunia.
5 Kisha kiti cha ufalme kitafanywa kuwa imara kabisa katika upendo mushikamanifu.
Ule mwenye kukiikalia katika hema ya Daudi atakuwa muaminifu;+
6 Tumesikia kuhusu kiburi cha Moabu—iko* na kiburi sana+—
Majivuno yake na kiburi chake na kasirani yake kali;+
Lakini maneno yake yenye hayana maana yataisha.
Wale wenye walipigwa wataomboleza kwa sababu ya keki za zabibu za Kir-hareseti.+
8 Kwa maana matuta ya Heshboni+ yamekauka.
Muzabibu wa Sibma,+
Watawala wa mataifa wamekanyanga-kanyanga matawi yake mekundu yenye kungaa;*
Walikuwa wamefika mupaka Yazeri;+
Walikuwa wameenea mupaka katika jangwa.
Machipukizi yake yalikuwa yameenea na kufika mupaka katika bahari.
9 Ndiyo sababu nitalilia muzabibu wa Sibma kama vile ninalilia Yazeri.
Machozi yangu yatakulowanisha, Ee Heshboni na Eleale,+
Kwa kuwa kupiga vigelegele kwa sababu ya matunda yako ya kipindi cha joto na mavuno yako kumeisha.*
10 Shangwe na furaha zimeondolewa katika shamba la matunda,
Na hakuna nyimbo za furaha ao kupiga vigelegele katika mashamba ya mizabibu.+
Mwenye kukanyanga hakanyange tena divai katika chombo cha kukamulia divai.
Kwa maana nimefanya vigelegele vimalizike.+
11 Ndiyo sababu niko na musukosuko ndani yangu kuhusu Moabu,+
Kama wakati kinubi kinapigwa,
Na utu wangu wa ndani sana kuhusu Kir-hareseti.+
12 Hata kama Moabu anajichokesha kwenye mahali pa juu na kuenda kusali katika patakatifu pake, hatatimiza kitu chochote.+
13 Hili ndilo neno lenye Yehova alisema zamani kuhusu Moabu. 14 Na sasa Yehova anasema: “Katika kipindi cha miaka tatu (3), kama miaka ya mufanyakazi wa kulipwa,* utukufu wa Moabu utapatishwa haya kwa muvurugo mwingi wa kila namna, na wale wenye watabakia watakuwa kidogo sana na wa hali ya chini.”+