Yobu
11 Sofari+ Munaamati akajibu:
2 “Je, maneno haya yote yatakosa kujibiwa,
Ao je, kusema mingi kutafanya mutu akuwe na haki?*
3 Je, maneno yako yenye hayana maana yatanyamazisha watu?
Je, utakosa kukaripiwa na mutu kwa sababu ya maneno yako ya muzaha?+
5 Lakini ingekuwa muzuri kama Mungu angesema
Na kukufungulia midomo yake!+
6 Halafu angekufunulia siri za hekima,
Kwa maana hekima yenye kutenda inatia ndani mambo mengi.
Basi ungetambua kwamba Mungu anaruhusu sehemu fulani ya kosa lako isahauliwe.
7 Je, unaweza kuvumbua mambo mazito ya Mungu
Ao kuvumbua kila kitu juu ya* Mweza-Yote?
8 Hekima yake iko juu kuliko mbingu. Wewe unaweza kufanya nini?
Inashuka chini sana kuliko Kaburi.* Wewe unaweza kujua nini?
9 Ni ya murefu kuliko dunia
Na kubwa kuliko bahari.
10 Akipita na kumukamata mutu fulani na kuitisha tribinali,
Ni nani anaweza kumupinga?
11 Kwa maana anajua wakati watu wanatenda kwa udanganyifu.
Wakati anaona mambo maovu, je, hatayakazia uangalifu?
12 Lakini mupumbavu ataelewa
Wakati tu punda wa pori ataweza kuzaa mwanadamu.*
13 Ingekuwa muzuri kama ungetayarisha moyo wako
Na kumuinulia mikono yako.
14 Kama mukono wako unatenda mambo ya mubaya, uutupe mbali,
Na usiruhusu ukosefu wa haki ukae katika mahema yako.
15 Halafu utaweza kuinua uso wako bila kasoro;
Na utaweza kusimama imara, bila kuogopa.
16 Halafu utasahau taabu yako;
Utaikumbuka kama maji yenye yameteremuka na kukupita.
17 Maisha yako yatangaa kuliko katikati ya muchana;
Hata giza lake litakuwa kama asubui.
18 Utakuwa na uhakika kwa sababu kuko tumaini,
Na utaangalia huku na huku na kulala kwa usalama.
19 Utalala, bila mutu wa kukuogopesha,
Na watu wengi watatafuta wema wako.
20 Lakini macho ya waovu yatakuwa zaifu;
Na hawatapata mahali pa kukimbilia,
Na tumaini lao litakuwa tu kifo.”+