Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 6/13 uku. 14-15
  • Je, Tangazo Hili Lilikubaliwa na Mungu?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Tangazo Hili Lilikubaliwa na Mungu?
  • Amuka!—2013
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wakaaji wa Inchi za Amerika Walilazimishwa Kuwa Wakatoliki
  • “Tangazo Lenye Kuleta Haya, Lenye Kukufuru, na Lisilo la Haki”
  • Sheria Zenye Ziligawanya Makontinenti
    Amuka!—2015
  • Kujulisha Neno la Mungu Katika Inchi ya Hispania ya Zamani
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Mahali Ambapo Mipaka Haina Maana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Amuka!—2013
g 6/13 uku. 14-15
[Picha katika ukurasa wa 14]

MAMBO TUNAYOJIFUNZA KUTOKANA NA HISTORIA | TANGAZO

Je, Tangazo Hili Lilikubaliwa na Mungu?

“Ikiwa hamufanye hivyo, . . . kwa musaada wa Mungu, nitakuja kwenu kwa nguvu, na nitawapiganisha kila mahali na kadiri ninavyoweza, nitawatia chini ya mamlaka ya Papa na Mufalme wa Espanye; na nitachukua bibi zenu na watoto wenu na kuwafanya kuwa watumwa, . . . na nitachukua mali zenu na kuwaumiza kadiri nitakavyoweza. . . . Vifo na mateso yote mutakayopata yatakuwa juu ya vichwa vyenu, wala si juu ya Mufalme wa Espanye ao juu yetu.”

HILO ni moja kati ya matangazo ya kipumbavu sana ambayo serikali imewahi kutoa. Maneno hayo ni sehemu ya tangazo linalojulikana kwa jina la el Requerimiento katika Kihispania, ambalo wavamizi ao washambuliaji wa Espanye walipaswa kusoma kwa sauti kubwa kati ya mwaka wa 1501 na 1600, walipofika katika Amerika wakiwa na kusudi la kushambulia.

Wakoloni hao wa Espanye walikuwa kwa kweli wakiwatangazia wakaaji wa inchi za Amerika nini, na kwa sababu gani?

Wakaaji wa Inchi za Amerika Walilazimishwa Kuwa Wakatoliki

Kisha tu Colomb kufika Amerika katika mwaka wa 1492, inchi ya Espanye na Portugal, kila moja ilidai kwamba ina haki ya kutawala maeneo hayo mapya. Kwa sababu mataifa yote hayo mawili yalimuona papa kuwa mwakilishi wa Kristo hapa duniani, yalipokuwa na ugomvi kati yao yalikuwa yakiita papa ili ayasaidie yasikilizane. Chini ya uongozi wa papa, kanisa liligawia Espanye na Portugal maeneo hayo mapya, lakini mbele ya kufanya hivyo inchi hizo mbili ziliombwa kutuma wamisionere ili waende kuwalazimisha wakaaji wa inchi za Amerika wawe wakatoliki.

Mashambulizi yalipokuwa yakiendelea, utawala wa Espanye ulitafuta njia za kutetea kisheria vitendo vya wakoloni hao. Utawala wa Espanye ulisema kama kwa kuwa papa aliongozwa na Mungu alipowapatia maeneo hayo, wakoloni walikuwa huru kuwatendea wakaaji wa inchi namna wanavyotaka, kuwanyanganya mali yao na kuzuia uhuru wao.

Utawala wa Espanye uliandika tangazo fulani ili kuwajulisha wakaaji wa inchi za Amerika uamuzi wa papa. Wakaaji wa inchi walilazimishwa kukubali Ukristo na kutawaliwa na mufalme wa Espanye. Wakuu wa Espanye walifikiri kwamba walikuwa na haki ya kupigana na wakaaji na haki ya kumutendea vibaya mukaaji yeyote wa inchi ambaye angekataa, na walifikiri pia kwamba Mungu aliwaunga mukono.

“Jeuri iliruhusiwa kwa sababu fulani, basi watu walitenda kama wenye kurukwa na akili. Kwa hiyo, wakubwa wa Espanye walitunga visababu ili kuonyesha kwamba vitendo hivyo vilikuwa vya haki.”​—Francis Sullivan, profesa wa teolojia ambaye alikuwa Muyeswiti

“Tangazo Lenye Kuleta Haya, Lenye Kukufuru, na Lisilo la Haki”

Tangazo hilo lilisomwa ili kutuliza zamiri ya watawala wa Espanye na kutetea mashambulizi hayo ya kikoloni. Mara kwa mara, wakoloni hao wa Espanye walisoma tangazo hilo wakiwa katika mashua mbele waanze mashambulizi na pia wakiwa kwenye inchi kavu, walilisomea watu ambao hawakuelewa luga za Ulaya. Wakati mwengine, walisoma tangazo hilo katika vijiji vyenye nyumba za misonge, vilivyobaki ukiwa kwa kuwa wakaaji wa inchi walikuwa wemekwisha kukimbia kwa sababu ya woga.

Damu ilimwangika sana kwa sababu ya kuwalazimisha watu wawe wakatoliki. Kwa mufano, katika mwaka wa 1550 huko Chili, Waaraukania 2 000 walichinjwa katika mapigano. Kuhusu Waaraukania ambao hawakufa, mukoloni Pedro de Valdivia alimuambia mufalme hivi: “Nilitoa ruhusa ya kukata mikono na pua za watu 200 waliokamatwa katika mapigano. Niliwatendea hivyo kwa sababu walikataa kutii amri ambazo niliwatumia mara nyingi.”a

Labda kusoma tangazo hilo kulituliza zamiri za wakoloni hao. Hata hivyo, lilishindwa kuleta maendeleo yoyote katika dini ya Espanye. Bartolomé de las Casas, misionere aliyekuwa mutawa, ambaye aliishi kati ya mwaka wa 1501 na 1600 alijionea matokeo mabaya ya Tangazo hilo, aliandika hivi: “Tangazo hilo lilikuwa lenye kuleta haya, lenye kukufuru, na lisilo la haki, la kipumbavu na la ovyo sana! Tangazo hilo lilichafua sana kanisa la Kikristo.” Muandikaji wa habari Gonzalo Fernández de Oviedo alisema kwa uchungu kwamba mauaji hayo ya wakaaji wa asili wa Amerika yaliwafanya waone Ukristo kuwa dini ya bure sana.

Je, ni Mungu ndiye anapaswa kulaumiwa kwa sababu ya mauaji hayo ambayo wakubwa wa siasa na wa dini walidai kwamba waliyafanya kwa jina la Mungu? Biblia inasema hivi: ‘Hasha, Mungu wa kweli hatende kwa uovu, na Mweza-Yote kutenda isivyo haki!’​—Ayubu 34:10.

a Kulingana na vyanzo fulani vya habari, tangazo el Requerimiento liliondolewa katika mwaka wa 1573.

NAMNA MATUKIO YALIVYOFUATANA

  • 1492 ▸ Colomb anafika katika Kontinenti Mupya (Amerika)

  • Karibu na 1493 ▸ Papa Alexandre wa 6 anamupatia mufalme wa Espanye na wa Portugal maeneo ya kutawala katika Kontinenti Mupya (Amerika)

  • 1513 ▸ Tangazo hilo linaanza kutumiwa

  • 1550 ▸ Waaraukania karibu 2 000 wanauawa katika inchi ya Chili

  • 1573 ▸ Ufalme wa Espanye unaondoa waziwazi Tangazo la el Requerimiento

MAELEZO MAFUPI

  • El Requerimiento lilikuwa tangazo lenye kuogopesha ambalo lilitolewa na wakoloni wa Espanye walipofika katika Amerika kati ya mwaka wa 1500 na 1600.

  • Wakaaji wa inchi “walilazimishwa” kukubali mamlaka ya Kanisa Katoliki.

  • Maneno ya Tangazo hilo yalisomwa kwa sauti kubwa katika Kihispania ao Kilatini kwa wakaaji wa inchi ambao hawakuelewa luga hizo zote mbili.

  • Hilo lilikuwa moja kati ya matangazo yenye kusumbua sana katika historia ya Waamerika.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine