Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 103 uku. 238-uku. 239 fu. 2
  • ‘Ufalme Wako Ukuje’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Ufalme Wako Ukuje’
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kusudi la Mungu Ni Nini Kuhusu Dunia?
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Mungu Anapenda Wanadamu Wakuwe na Maisha ya Namna Gani?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Mungu Ana Kusudi Gani juu ya Dunia?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Mungu Anapenda Dunia Ikuwe Namna Gani?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 103 uku. 238-uku. 239 fu. 2
Wakubwa na watoto wanafurahia maisha mu Paradiso

SOMO LA 103

“Ufalme Wako Ukuje”

Yehova alitoa ahadi hii: ‘Hakutakuwa tena kilio, maumivu, magonjwa, wala kifo. Nitapanguza machozi yote kutoka katika macho yao. Mambo yote ya mubaya ya zamani itasahauliwa.’

Yehova alitia Adamu na Eva mu bustani ya Edeni. Alipenda waishi kwa furaha na amani. Walipaswa kumuabudu Baba yao wa mbinguni na kujaza dunia. Adamu na Eva hawamukutii Yehova, lakini kusudi la Yehova halikubadilika. katika hiki kitabu, tumeona kama mambo yote yenye Mungu anasemaka haikosake kutimia. Ufalme wake utaleta baraka za muzuri sana mu dunia, sawa vile alimuambiaka Abrahamu.

Wakubwa, watoto, na wanyama wa pori wako pamoja mu Paradiso

Karibuni, Shetani na pepo wake wachafu wataharibiwa, na watu wote wabaya hawatakuwa tena ku dunia. Kila mutu atamuabudu Yehova. Magonjwa itaisha, na kifo kitaisha. Kila siku, tutaamuka na nguvu na furaha. Dunia itakuwa paradiso. Kila mutu atakuwa na chakula kizuri na ataishi mu nyumba yake bila kuogopa. Watu watakuwa wapole. Watatendeana muzuri. Hatutaogopa wanyama wa pori, nao hawatatuogopa.

Itakuwa muzuri sana wakati Yehova ataanza kufufua watu! Tutafurahi kuonana na Abeli, Noa, Abrahamu, Sara, Musa, Rutu, Esta, Daudi na wengine wenye walimutumikiaka Mungu zamani. Tutatumika nao ili kufanya dunia ikuwe paradiso. Sikuzote tutakuwa na kazi mingi ya kufurahisha.

Yehova anapenda ukuwe katika paradiso. Katika paradiso, utafikia kumujua mu namna yenye hauwezi hata kuwazia sasa. Tuendelee basi kumukaribia Yehova zaidi na zaidi, kuanzia sasa mupaka milele!

“Unastahili, Yehova Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote.”​—Ufunuo 4:11

Maulizo: Wakati Ufalme wa Mungu utaanza kutawala ku dunia, maisha yetu itakuwa namna gani? Kati ya watu wenye tumezungumuzia katika hiki kitabu, utapenda kuonana na nani katika paradiso?

Ufunuo 21:3, 4; Ayubu 33:25; Mezali 2:21, 22; Isaya 11:2-10; 33:24; 65:21; Matayo 6:9, 10; Yohana 5:28, 29; 17:3

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine