Kitulizo
Maandiko ya Biblia ya kututuliza mu hali fulani zenye kuvunja moyo
Uchungu
Ona “Mahangaiko”
Kinyongo
Watu fulani wako na uchungu juu ya magumu
Ona pia Zb 142:4; Muh 4:1; 7:7
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Maandiko yenye kutia moyo:
Habari za Biblia zenye kutia moyo:
Rut 1:6, 7, 16-18; 2:2, 19, 20; 3:1; 4:14-16—Kisha kujiunga tena na watu wa Mungu, kupata musaada wa wengine, na kusaidia wengine, Naomi anakuwa tena na furaha
Yob 42:7-16; Yak 5:11—Kwa imani, Yobu anavumilia na Yehova anamubariki sana
Watu fulani wako na uchungu juu wengine wamewatendea mubaya
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
1Sa 1:6, 7, 10, 13-16—Hana iko na uchungu sana juu Penina iko namutendea mubaya na Kuhani Mukubwa Eli anamuhukumu kwa kukosea
Yob 8:3-6; 16:1-5; 19:2, 3—Wafariji watatu wa uongo wa Yobu, wanajiona kuwa wenye haki, wanamuhukumu Yobu na ile inafanya Yobu ajisikie mubaya
Maandiko yenye kutia moyo:
Habari za Biblia zenye kutia moyo:
1Sa 1:9-11, 18—Hana anapata kitulizo kisha kumufungulia Yehova moyo wake
Yob 42:7, 8, 10, 17—Kisha Yobu kusamehe marafiki wake wa uongo, Yehova anafanya akuwe tena na afya ya muzuri na akuwe tena na furaha
Kujihukumu kupita kiasi
Ezr 9:6; Zb 38:3, 4, 8; 40:12
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
2Fa 22:8-13; 23:1-3—Mufalme Yosia na watu wake wanatambua makosa yao makubwa kisha wao kusomewa Sheria ya Musa kwa sauti kubwa
Ezr 9:10-15; 10:1-4—Ezra na Waisraeli wanajisikia mubaya sana kisha wao kujua kama wamoja kati yao wanakatala kumutii Yehova kwa kuoa wanamuke wa mataifa ingine
Lu 22:54-62—Mutume Petro anajisikia mubaya sana kisha kumukana Yesu mara tatu
Maandiko yenye kutia moyo:
Habari za Biblia zenye kutia moyo:
2Ny 33:9-13, 15, 16—Manase ni moya kati ya Wafalme wabaya sana wa Yuda, lakini, anatubu na anapata rehema
Lu 15:11-32—Yesu anazungumuzia mufano wa mwana mupotevu juu ya kuonyesha kama Yehova anakuwaka tayari kusamehe na anasameheaka kwa njia kubwa
Kuhuzunika wakati wengine wanakatala kututegemeza, wanatuumiza, ao hata kutusaliti
Ona “Huzuni”
Kuhuzunika juu ya makosa na zambi zetu
Ona “Huzuni”
Kujiona kuwa hatuko wa maana
Ona “Mashaka”
Kuwaza kama hatutamaliza tatizo fulani ao kutimiza mugao fulani
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Kut 3:11; 4:10—Musa anawaza kama hataweza kukutana na Farao na kuongoza watu wa Mungu kutoka Misri
Yer 1:4-6—Yeremia anawaza kama angali kijana sana na kama hataweza kuwa nabii wa Yehova kwa watu wenye kuwa na mioyo migumu
Maandiko yenye kutia moyo:
Habari za Biblia zenye kutia moyo:
Kut 3:12; 4:11, 12—Kwa uvumilivu, Yehova anahakikishia nabii Musa kama atamusaidia mu mugao wake
Yer 1:7-10—Yehova anahakikishia nabii Yeremia kama atamusaidia mu migao yake ya nguvu
Wivu
Ona “Wivu”
Mipaka yenye inatokana na magonjwa ao uzee
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
2Fa 20:1-3—Mufalme Hezekia anasikia mubaya sana juu anagonjwa karibu akufe
Flp 2:25-30—Epafrodito anasikia mubaya sana juu kutaniko inajua kama iko mugonjwa; ile inafanya aogope kuwa watawaza kama anashindwa kutimiza mugao wake
Maandiko yenye kutia moyo:
Habari za Biblia zenye kutia moyo:
2Sa 17:27-29; 19:31-38—Mufalme anamuheshimia sana Barzilai na kumuomba aende Yerusalemu. Lakini, kwa kiasi Barzilai anakatala ile Mwaliko juu alikuwa alishazeeka sana
Zb 41:1-3, 12—Daudi anagonjwa sana, lakini iko hakika kama Yehova atamutegemeza
Mk 12:41-44—Yesu anapongeza mujane maskini juu ya muchango yake, juu anatoa yote yenye iko nayo
Kuhuzunika kwa wakati murefu juu ya kutendewa mubaya na wengine
Ona “Kutendewa Mubaya”
Woga wa nguvu
Ona “Woga”
Mateso
Ona “Mateso”