Moyo
Namna gani Biblia inaonyesha kama moyo wa mufano ni mutu wa ndani, ni kusema, mawazo, nia, sifa, na hisia?
Zb 49:3; Mez 16:9; Lu 5:22; Mdo 2:26
Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:
Lu 9:46-48—Yesu anarekebisha mitume wake juu ya mawazo ya mubaya yenye anaona mu mioyo yao
Juu ya nini tunapaswa kabisa kulinda moyo wetu?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Mwa 6:5-7—Uovu mu moyo wa mwanadamu unamufanya atende kwa jeuri na ile inafanya Mungu alete Garika
1Fa 11:1-10—Mufalme Sulemani anashindwa kulinda moyo wake, anaoa bibi wageni wenye wanafanya moyo wake usimufuate tena Yehova
Mk 7:18-23—Yesu anafasiria kama mu moyo njo munatokaka mambo yote yenye inaweza kuchafua mutu mbele ya Mungu
Namna gani tunaweza kulinda moyo wetu?
Zb 19:14; Mez 3:3-6; Lu 21:34; Flp 4:8
Ona pia Ezr 7:8-10; Zb 119:11
Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:
Efe 6:14-18; 1Te 5:8—Mutume Paulo anazungumuzia silaha za kiroho na anafasiria kama haki, imani, na upendo vinaweza kulinda moyo wa mufano sawa vile tu bamba ya kifua inalindaka moyo halisi
Namna gani tunaweza kujua kama moyo wetu wa mufano uko na tatizo?
Ona pia Mez 6:12-14
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
2Ny 25:1, 2, 17-27—Kwa wakati fulani, Mufalme Amazia anafanya mambo yenye kuwa sawa mbele ya Mungu lakini hapana kwa moyo wake wote; kisha wakati fulani, anakuwa na kiburi, na haiko tena muaminifu na anateseka juu ya ile
Mt 7:17-20—Yesu anaonyesha kama vile tu muti mubaya unatoshaka matunda ya mubaya, ni vile moyo wa mubaya unafanyaka mutu atende mubaya
Juu ya nini tunapaswa kuwa na moyo muzuri, na namna gani tunaweza kufanya vile?
Ona pia Zb 119:97, 104; Ro 12:9-16; 1Ti 1:5
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
2Fa 20:1-6—Wakati anakaribia kufa, Mufalme Hezekia anamulilia Yehova amuonyeshe rehema juu alimutumikia kwa moyo wote
Mt 21:28-32—Yesu anatoa mufano juu ya kuonyesha kama mambo yenye mutu anafanya njo inaonyeshaka hali ya moyo wake kuliko mambo yenye anasema kama atafanya
Juu ya nini inatia moyo kujua kama Yehova anachunguzaka moyo?
Ona pia 1Sa 2:3
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
1Sa 16:1-13—Nabii Samweli anajifunza kama Yehova hadanganywake na namna mutu anaonekana kwa inje; lakini anaangaliaka moyo wa mutu
2Ny 6:28-31—Sala ya Mufalme Sulemani wakati wa kumutolea Yehova hekalu inaonyesha kama Mungu anajua kabisa moyo wa mwanadamu na anamutendeaka kwa rehema kulingana na vile anaona moyo wake