Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/00 uku. 1
  • Je, wewe ni mwenye kuvumilia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, wewe ni mwenye kuvumilia?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Muache Uvumilivu Ukamilishe Kazi Yake’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Endelea Kubakia mu Tengenezo ya Yehova
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Tuige Uvumilivu wa Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Shangwe—Sifa Yenye Tunapata Kutoka kwa Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 8/00 uku. 1

Je, wewe ni mwenye kuvumilia?

1 “Sina kisababishi cha shukrani kilicho kikubwa zaidi kuliko mambo haya, . . . kwamba watoto wangu waendelea kutembea katika kweli.” (3 Yn. 4) Uvumilivu wa watoto wa kiroho wa Yohana ulimletea furaha kubwa. Inapaswa kumfurahisha kama nini Baba yetu wa mbinguni kuona mamilioni ya wale wanaotazamiwa kuwa watoto wake ‘wakiendelea kutembea katika kweli’!—Mez. 23:15, 16; 27:11.

2 Ingawa watu wa Mungu kwa ujumla wanadumu katika utendaji wa Kikristo wenye bidii, wengine wamepunguza mwendo hatua kwa hatua. Ingawa huenda hawa walikuwa wenye nguvu wakati walipojifunza kweli kwa mara ya kwanza, kadiri miaka inavyopita, wamezama katika tabia za kuwa na ushiriki mdogo au usio wa kawaida katika kazi ya kufanya wanafunzi.

3 Kwa njia yenye kueleweka, huenda wengine wakapunguza mwendo kwa sababu ya matatizo ya kimwili na matokeo ya umri wenye kuendelea. Hata hivyo, wanapaswa kusifiwa kwa uvumilivu wao. Wanafanya yale wanayoweza. Lakini kila mmoja ambaye ameweka maisha yake wakfu kwa Mungu anapaswa kujiuliza: ‘Je, nimejiacha nikaze sana fikira juu ya ufuatiaji wa mambo ya kibinafsi hivi kwamba faida za Ufalme zinachukua tu nafasi ndogo katika maisha yangu? Je, kwa njia fulani nimekuwa “si baridi wala moto,” au je, ningali mwenye kufanya nguvu? (Ufu. 3:15, 16; Luka 13:24) Acheni sisi sote tufikiri juu ya yale tunayotenda na kufanya maendeleo ikiwa hayo yanahitajiwa, tukikumbuka kwamba Yehova anaahidi kutoa “utukufu na heshima na amani kwa kila mtu afanyaye lililo jema”—Rom. 2:10.

4 Jinsi ya kuvumilia: Ni nini kilichomsaidia Yesu avumilie? Paulo alieleza: “Kwa ajili ya shangwe iliyowekwa mbele yake alivumilia mti wa mateso, akidharau aibu, na ameketi kwenye mkono wa kuume wa kiti cha ufalme cha Mungu.” (Ebr. 12:1-3) Furaha iliyowekwa mbele ya Yesu ilipita kwa mbali majaribu ya wakati mdogo ambayo alipaswa kukabiliana nayo. Kulinda akilini furaha ambayo inawekwa mbele yetu kunaweza kutusaidia pia kuvumilia. (Ufu. 21:4, 7; 22:12) Ikiwa tunamwendea Yehova ili atupe nguvu kupitia funzo la kibinafsi, kuhudhuria kikawaida mikutano, na kudumu katika sala, tutakuwa na uwezo wa kuvumilia kwa bidii katika kazi ambayo ametutolea kufanya.

5 Yehova ni mwenye furaha wakati waaminifu wake wanapovumilia. Acheni basi tuongeze furaha yake kwa kuendelea “kutembea katika kweli.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine