Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/00 uku. 2
  • Programu ya mikutano ya utumishi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu ya mikutano ya utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Vichwa Vidogo
  • Juma Toka Agosti 14
  • Juma Toka Agosti 21
  • Juma Toka Agosti 28
  • Juma Toka Septemba 4
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 8/00 uku. 2

Programu ya mikutano ya utumishi

Juma Toka Agosti 14

Wimbo 114

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Toa maelezo kuhusu ripoti ya utumishi wa shambani ya Machi ya nchi na ya kutaniko lenu. Kunabaki tu miisho-juma miwili mnamo Agosti; kwa hiyo, tia kila mmoja moyo ashiriki katika huduma kabla ya mwezi kwisha. Rudilia programu kwa ajili ya utumishi wa shambani ya mwisho-juma.

Dak. 15: “Pigana Pigano Bora la Imani.” Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu. Chukua maelezo mengine ya ziada kutoka katika kitabu Huduma Yetu, kurasa 44-5, kuhusu jinsi viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko hupanga utendaji wa utumishi wa shambani kwa ajili ya vikundi vyao na jinsi wao hutoa uangalifu kwa wowote wale wanaohitaji msaada wa kibinafsi ili kushiriki na kuripoti huduma yao kwa ukawaida.

Dak. 18: Jinsi Unavyoweza Kufaidika kwa Kwenda Shuleni. Baba mmoja anazungumza na watoto wake ili kuwasaidia waone kwa nini elimu fulani ya kimwili ni yenye mafaa. (Ona kitabu Vijana Huuliza, kurasa 133-9.) Vijana wengi hufikiri kwamba kwenda shuleni ni mwito wa kushindana katika jamii ya leo isiyotawalika. Wanajisikia pia wenye kuchoshwa, wakikata maneno kwamba yale wanayojifunza hayatakuwa na thamani kubwa yenye kutumika. Baba anarudilia kanuni za Kimaandiko na sababu nzuri zinazofanya liwe jambo la hekima kupata kiasi cha kutosha cha elimu ya kimwili. Anatia watoto wake moyo wajifunze vizuri na kuwa wenye kusikiliza kwa uangalifu darasani.

Wimbo 127 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Agosti 21

Wimbo 143

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti. Fanyisha onyesho moja la kutumikisha katika utumishi wa shambani ambalo limetayarishwa vizuri, likionyesha jinsi ya kujibu ulizo: “Sababu gani Mungu wa upendo angeruhusu kuteseka kuendelee muda mrefu sana?” (Kitabu Kutoa Sababu, ukurasa 134) Tia kila mmoja moyo ashiriki katika huduma mwisho-juma huu.

Dak. 8: “Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja.” Hotuba. Tangaza tarehe ya kusanyiko la pekee lijalo, ikiwa hiyo inajulikana, na usihi wote wahudhurie siku nzima. Tia wahubiri moyo waalike watu waliopendezwa hivi karibuni na pia wanafunzi wa Biblia.

Dak. 25: “Je, Wewe Ni Mwenye Kujipatia Faida?” Maulizo na majibu.

Wimbo 152 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Agosti 28

Wimbo 165

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote watoe ripoti za utumishi wa shambani za Agosti. Viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko wanapaswa kuona kila mtu katika kikundi chao kusudi ripoti zote ziweze kukusanywa kufikia Septemba 6.

Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.

Dak. 20: “Mikutano Hufaidi Vijana.” Mazungumzo ya maulizo na majibu yakiongozwa na mzee. Wakati wa kuzungumzia fungu 8, fikirieni mambo fulani yenye kutumika ambayo huendeleza kukaza fikira na kuwa mwangalifu wakati wa mikutano. (Ona Amkeni! ya Septemba 22, 1998, kurasa 19-20.) Tia wazazi moyo wawe imara katika kuomba watoto wao wahudhurie kikawaida mikutano yote.—Ona jambo lililoonwa katika Mnara wa Mlinzi wa Septemba 1, 1997, ukurasa 25.

Wimbo 176 na sala ya kumalizia.

Juma Toka Septemba 4

Wimbo 196

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Kazia yale mambo kuhusu “Usimamizi wa Akiba ya Vichapo Katika Majumba ya Ufalme.”

Dak. 10: Wakati Wetu Ni wa Pekee. Hotuba inayotolewa na mzee, ikiwa na msingi juu ya Mnara wa Mlinzi wa Novemba 15, 1996, kurasa 22-3.

Dak. 20: “Je, Wewe Ni Mwenye Kuvumilia?” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tia wote moyo wafikiri juu ya matokeo yao binafsi katika kuonyesha uvumilivu katika huduma ya Kikristo. Ikiwa udhaifu unakuwa wazi, kuna uhitaji wa kujiimarisha kiroho. Tia ndani maelezo kutoka katika Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 1, 1999, kurasa 20-1, mafungu 17-21. Alika wahubiri wawili au watatu ambao wamevumilia kwa uaminifu kwa kipindi cha miaka mingi waeleze yale wanayofanya kibinafsi ili kuvumilia.

Wimbo 206 na sala ya kumalizia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine