Kujikumbusha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.
1. Tunaweza kujifunza nini kutokana na amri iliyo katika andiko la Kutoka 23:19? [w06 4/1 uku. 31 fu. 1-5]
2. Urimu na Thumimu zilikuwa nini, na jinsi gani zilitumiwa katika Israeli ya zamani? (Kut. 28:30) [w06 1/15 uku. 18; w01 9/1 fu. 27]
3. Namna gani Yehova alizungumza na Musa “uso kwa uso”? (Kut. 33:11, 20) [w04 3/15 uku. 27]
4. Tunaweza kujifunza nini kutoka kwa Waisraeli ambao walitoa vitu vya kimwili na kutumia ufundi wao ili kujenga maskani? (Kut. 35:5, 10) [w99 11/1 uku. 31 fu. 1-2]
5. Kisitiri (voile) kinachozungumziwa kwenye andiko la Kutoka 40:28 kinafananisha nini katika hekalu kuu la kiroho la Mungu? [w00 1/15 uku. 15 fu. 7-8]
6. Ni sehemu gani ya zabihu ya Yesu inayotukumbusha “toleo la kuteketezwa,” ambalo lilitiwa lote kwenye mazabahu? (Law. 1:13) [w04 5/15 uku. 21 fu. 3]
7. Tunajifunza nini kutokana na wazo la kwamba “mafuta yote ni ya Yehova”? (Law. 3:16, 17) [w04 5/15 uku. 22 fu. 2]
8. Kutia damu ya kondoo ndume mwenye kuwekwa rasmi kwenye sikio la kuume, mkono wa kuume, mguu wa kuume wa Haruni na wa wana wake kulimaanisha nini? (Law. 8:23, 24) [it-2-F uku. 460 fu. 3]
9. Walawi 12:8 inatutolea uelewaji gani kuhusu wazazi wa Yesu, na tunaweza kujifunza nini kutokana na hilo? [w98 12/15 uku. 6 fu. 5]
10. Zabihu mbalimbali za wanyama zilizotolewa Siku ya Upatanisho ya kila mwaka zilifananisha nini kuhusiana na zabihu ya Yesu? (Law. 16:11-16) [w98 2/15 uku. 12 fu. 2]