Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb25 Mwezi wa 7 uku. 11-16
  • Tarehe 11-17/8

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tarehe 11-17/8
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2025
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2025
mwb25 Mwezi wa 7 uku. 11-16

TAREHE 11-17/8

MEZALI 26

Wimbo 88 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU

1. Ukuwe Mbali na “Mujinga”

(Dak. 10)

Mara mingi “mujinga” haheshimiwake (Mez 26:1; it-2 uku. 602 fu. 1)

Mara mingi, inaomba kumupatia ‘mujinga’ malipizi ya nguvu (Mez 26:3; w87-SW 1/10 uku. 19 fu. 12)

“Mujinga” hakuwake mutu wa kutumainia (Mez 26:6; it-1 uku. 357 fu. 3)


MAANA: Mu Biblia, neno “mujinga” inamaanisha mutu mwenye hafikiri muzuri na hatii mambo yenye Mungu anasema.

Ku masomo, ndugu moya kijana anaangalia mbele na iko napita mbali ya banafunzi benzake benye biko naangalia kitu fulani ku telefone.

2. Mali ya Kiroho

(Dak. 10)

  • Mez 26:4, 5—Mawazo yenye kuwa mu hii mistari mbili inapingana? Fasiria. (it-2 uku. 1006)

  • Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Mez 26:1-20 (th somo ya 5)

TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI

4. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Anzisha mazungumuzo kwa kutumia trakte. (lmd somo ya 1 nukta ya 5)

5. Kuendelesha Mazungumuzo

(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Endelesha mazungumuzo mu trakte yenye uliachiaka mutu wakati mulionanaka mbele ya pale. (lmd somo ya 7 nukta ya 4)

6. Kufanya Banafunzi

(Dak. 5) Saidia mwanafunzi wako ajitayarishe juu ya kuhubiria mutu wa familia yake. (lmd somo ya 11 nukta ya 5)

MAISHA YA MUKRISTO

Wimbo 94

7. Funzo ya Kipekee Itakusaidia Ukuwe “Mwenye Hekima kwa Ajili ya Wokovu”

(Dak. 15) Mazungumuzo.

Picha mbalimbali: 1. Dada moya iko najifunza kwake. Iko naangalia video moya ya luga ya ishara ku jw.org kupitia ordinatere yake. 2. Wakati ya mapumuziko, ndugu moya alishatia maekutere na iko najifunza ku telefone yake. 3. Dada moya mwenye kuzeeka iko natumikisha application “JW Library” ku tablete yake. 4. Mu mikutano, mama moya na mutoto wake mwanaume biko natumikisha application “JW Library” ku tablete.

Timoteo alijifunzaka maandiko matakatifu tangu wakati alikuwa angali mutoto. Mutume Paulo alimukumbushaka kama ile mambo yenye alijifunzaka ni ya maana sana juu ingemusaidia akuwe “mwenye hekima kwa ajili ya wokovu.” (2Ti 3:15) Juu mafundisho ya Biblia ni ya maana sana, tunapaswa kutafuta wakati ya kukuwa nasoma na kujifunza Biblia kila siku. Sasa, utafanya nini kama haufurahiake bya kujifunza?

Soma 1 Petro 2:2. Kisha uliza basikilizaji:

  • Inawezekana tujikaze kufurahia kujifunza Biblia?

  • Tunaweza kufanya nini juu tupende sana kujifunza Biblia?—w18.03 uku. 29 fu. 6

  • Namna gani byombo sawa vile JW Library® binaweza kutusaidia tujifunze mambo mingi zaidi wakati tuko nasoma na kujifunza Biblia?

Muangalie VIDEO Mambo Yenye Kutimizwa na Tengenezo—Namna ya Kutumikisha JW Library. Kisha uliza basikilizaji:

  • JW Library imekusaidia namna gani?

  • Unafurahiaka kutumikisha sehemu gani za JW Library?

  • Ni sehemu gani zenye unapenda kuanza kujifunza na kutumikisha?

8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko

(Dak. 30) lfb somo ya 8-9

Maneno ya Kumalizia (Dak. 3) | Wimbo 89 na Sala

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine