TAREHE 11-17/8
MEZALI 26
Wimbo 88 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)
1. Ukuwe Mbali na “Mujinga”
(Dak. 10)
Mara mingi “mujinga” haheshimiwake (Mez 26:1; it-2 uku. 602 fu. 1)
Mara mingi, inaomba kumupatia ‘mujinga’ malipizi ya nguvu (Mez 26:3; w87-SW 1/10 uku. 19 fu. 12)
“Mujinga” hakuwake mutu wa kutumainia (Mez 26:6; it-1 uku. 357 fu. 3)
MAANA: Mu Biblia, neno “mujinga” inamaanisha mutu mwenye hafikiri muzuri na hatii mambo yenye Mungu anasema.
2. Mali ya Kiroho
(Dak. 10)
Mez 26:4, 5—Mawazo yenye kuwa mu hii mistari mbili inapingana? Fasiria. (it-2 uku. 1006)
Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Mez 26:1-20 (th somo ya 5)
4. Kuanzisha Mazungumuzo
(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Anzisha mazungumuzo kwa kutumia trakte. (lmd somo ya 1 nukta ya 5)
5. Kuendelesha Mazungumuzo
(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Endelesha mazungumuzo mu trakte yenye uliachiaka mutu wakati mulionanaka mbele ya pale. (lmd somo ya 7 nukta ya 4)
6. Kufanya Banafunzi
(Dak. 5) Saidia mwanafunzi wako ajitayarishe juu ya kuhubiria mutu wa familia yake. (lmd somo ya 11 nukta ya 5)
Wimbo 94
7. Funzo ya Kipekee Itakusaidia Ukuwe “Mwenye Hekima kwa Ajili ya Wokovu”
(Dak. 15) Mazungumuzo.
Timoteo alijifunzaka maandiko matakatifu tangu wakati alikuwa angali mutoto. Mutume Paulo alimukumbushaka kama ile mambo yenye alijifunzaka ni ya maana sana juu ingemusaidia akuwe “mwenye hekima kwa ajili ya wokovu.” (2Ti 3:15) Juu mafundisho ya Biblia ni ya maana sana, tunapaswa kutafuta wakati ya kukuwa nasoma na kujifunza Biblia kila siku. Sasa, utafanya nini kama haufurahiake bya kujifunza?
Soma 1 Petro 2:2. Kisha uliza basikilizaji:
Inawezekana tujikaze kufurahia kujifunza Biblia?
Tunaweza kufanya nini juu tupende sana kujifunza Biblia?—w18.03 uku. 29 fu. 6
Namna gani byombo sawa vile JW Library® binaweza kutusaidia tujifunze mambo mingi zaidi wakati tuko nasoma na kujifunza Biblia?
Muangalie VIDEO Mambo Yenye Kutimizwa na Tengenezo—Namna ya Kutumikisha JW Library. Kisha uliza basikilizaji:
JW Library imekusaidia namna gani?
Unafurahiaka kutumikisha sehemu gani za JW Library?
Ni sehemu gani zenye unapenda kuanza kujifunza na kutumikisha?
8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo ya 8-9