TAREHE 29/9–5/10
MUHUBIRI 3-4
Wimbo 93 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)
Mukuwe napitisha wakati nyiye bawili, na pia pamoya na Yehova
1. Mufanye Kamba Yenu ya Nyuzi Tatu Ikuwe Nguvu
(Dak. 10)
Mukuwe na mazungumuzo yenye kujenga (Muh 3:1; ijwhf habari ya 10 fu. 2-8)
Mufanye bitu pamoya (Muh 4:9; w23.05 uku. 23 fu. 12-14)
Mujikaze kuwa na burafiki ya karibu pamoya na Yehova (Muh 4:12; w23.05 uku. 20 fu. 3)
UJIULIZE, ‘Kutakuwa matokeo gani mu ndoa yangu kama naanza kupitisha wakati ya murefu mbali na bibi ao bwana yangu, ao kama naenda mu vacance bila yeye, ao tena kama nafanya safari ya muda murefu juu ya kazi?’
2. Mali ya Kiroho
(Dak. 10)
Muh 3:8—Ni wakati gani njo haiko “wakati wa kupenda”? (it-F “Amour” fu. 39)
Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Muh 4:1-16 (th somo ya 2)
4. Kuanzisha Mazungumuzo
(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Tumia Munara wa Mulinzi Na. 1 2025 juu ya kuanzisha mazungumuzo. Ujikaze kujipatanisha na hali wakati mutu anaonyesha kama anafurahia habari ingine. (lmd somo ya 2 nukta ya 5)
5. Kuendelesha Mazungumuzo
(Dak. 4) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Anzisha funzo ya Biblia na mutu mwenye aliitika Munara wa Mulinzi Na. 1 2025. (lmd somo ya 9 nukta ya 4)
6. Hotuba
(Dak. 5) lmd nyongeza ya A nukta ya 12—Kichwa: Mungu Anatendeaka Batu Yote Sawasawa na Hakuwake na Ubaguzi. (th somo ya 19)
Wimbo 131
7. Tumainia Muongozo wa Yehova Wakati Matatizo Inatokea mu Ndoa Yako
(Dak. 15) Mazungumuzo.
Yehova alishapatia bibi na bwana Bakristo byote byenye biko nabyo lazima juu bakuwe na furaha ya kweli mu ndoa yabo. Hata vile, wakati fulani kutakuwa tu matatizo kati ya bibi na bwana. (1Ko 7:28) Kama habatatue ile matatizo, habatakuwa tena na furaha, na banaweza hata kuwaza kama maisha ya ndoa imebashinda. Unaweza kufanya nini kama uko na magumu ya hivi mu ndoa yako?
Filme Upendo wa Kweli Ni Nini? inazungumuzia bibi na bwana bijana benye biko na matatizo ya nguvu mu ndoa yabo. Unakumbuka shauri yenye baba alimupatiaka mutoto wake mwanamuke wakati alipenda kukamata uamuzi wenye ulipinga mapenzi ya Yehova?
Muangalie VIDEO Upendo wa Kweli Ni Nini?—Sehemu. Kisha uliza basikilizaji:
Juu ya nini tunapaswa kufuata muongozo wa Yehova wakati kunatokea matatizo mu ndoa?—Isa 48:17; Mt 19:6
Kama uko na matatizo mu ndoa yako, ujikaze kubakia karibu na Yehova kwa kusali, kwa kukusanyika, kwa kusoma na kujifunza Biblia, na pia kwa kuhubiri. Juu ya kutatua matatizo, tumikisha kanuni za Biblia, na utafute habari zingine mu bichapo byetu. Kufanya vile kutakusaidia kuona mambo vile Yehova anaiona, na utaonyesha kama uko na lazima ya musaada wake na baraka yake.—Mez 10:22; Isa 41:10.
Muangalie VIDEO Amani ya Uongo Isikudanganye!—Darrel na Deborah Freisinger. Kisha uliza basikilizaji:
Mufano wa ndugu Darrel na dada Deborah inakufundisha nini kuhusu namna ya kutatua matatizo ya nguvu mu ndoa?
8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo ya 22, utangulizi wa sehemu ya 5, na somo ya 23