MUENDELEE KUKESHA!
Vita ya Ukraine Imefanya Chakula Ikosekane mu Dunia Yote
Tarehe 19, Mwezi wa 5, 2022, maofisa 75 wa cheo ya juu walijulisha idara ya Umoja wa Mataifa yenye kuhangaikia mambo ya usalama kama tayari chakula ilikuwa imekosekana mu dunia yote juu ya Coronavirus na mabadiliko ya hali ya hewa, na ile hali inaendelea kuwa mubaya zaidi juu ya vita mu Ukraine. Kisha pale, gazeti The Economist ilionyesha kama “tayari dunia iko na matatizo mingi, na juu ya ile vita, watu wengi sana watakosa chakula.” Biblia ilisemaka kama chakula itakosekana mu wakati yetu. Lakini, inaonyesha pia namna tunaweza kupambana na ile hali.
Biblia ilisemaka kama chakula itakosekana
Yesu alisemaka hivi: “Taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme, na kutakuwa upungufu wa chakula.”—Matayo 24:7.
Kitabu ya Ufunuo inazungumuzia wapanda-farasi ine wa mufano. Mumoja kati yao anafananisha vita. Mwingine mwenye anamufuata anafananisha njala, ni kusema, wakati yenye itakuwa nguvu kupata chakula na wakati chakula itapanda bei. “Nikaona: tazama, farasi mweusi, na yule mwenye kumupanda alikuwa na mizani mkononi mwake. Nikasikia kama sauti . . . iliyosema: ‘Kipimo cha ngano kwa denari moja, na vipimo vitatu vya shayiri kwa denari moja.’”—Ufunuo 6:5, 6, Verbum Bible.
Ile maunabii ya Biblia inazungumuzia kukosekana kwa chakula, na iko natimia leo mu hii wakati yenye Biblia inaita “siku za mwisho.” (2 Timoteo 3:1) Juu ya kujua mambo mingi zaidi kuhusu “siku za mwisho” na kuhusu wapanda-farasi ine wenye kitabu ya Ufunuo inazungumuzia, angalia video Dunia Imebadilika Tangu 1914 na usome habari “Wale Wapanda-Farasi Ine—Ni Nani?”
Namna Biblia inaweza kutusaidia
Biblia iko na mashauri yenye inaweza kutusaidia kupambana na magumu, sawa vile kukosa chakula na hata njala. Ona mashauri fulani mu habari “Jinsi ya Kuishi Ukiwa na Pesa Kidogo.”
Tena, Biblia inatupatia tumaini kama mambo itakuwa muzuri. Inaahidi kama kuko siku yenye “kutakuwa nafaka nyingi juu ya dunia” na kila mutu atakuwa na chakula mingi. (Zaburi 72:16) Juu ya kujua mambo mingi kuhusu tumaini yenye Biblia inatoa na juu ya nini tunaweza kuitumainia, soma habari “Tumaini Bora la Wakati Ujao.”