Maelezo ya Chini
b Mahali patakatifu palikuwa ni hema kubwa ya kukutania iliyokuwa na umbo la rektangulo, ilishikwa na nguzo za mbao. Hema hiyo ilitengenezwa kwa vitu vizuri sana, kama vile, ngozi ya munyama anayeitwa foke, vitambaa vilivyopambwa vizuri, na mbao za bei kali zilizofunikwa kwa feza na zahabu. Mahali hapo patakatifu palizunguukwa na ukuta na upande wa ndani ya ukuta huo kulikuwa pia mazabahu nzuri sana kwa ajili ya zabihu. Inaonekana kwamba baadaye, vyumba vingine vilijengwa pembeni-pembeni ya hema hiyo kwa ajili ya makuhani. Labda Samweli alikuwa analala ndani ya moja ya vyumba hivyo.