Maelezo ya Chini
a Inawezekana “sauti tulivu, ya chini” ni ya ule malaika aliyetumiwa kupeleka “neno la Yehova;” malaika anayetajwa katika andiko la 1 Wafalme 19:9. Katika mustari wa 15, malaika huyo anatajwa kuwa ni “Yehova.” Hilo linaweza kutukumbusha malaika ambaye Yehova alitumia ili kuwaongoza Waisraeli katika jangwa na ambaye Mungu alisema hivi kumuhusu: “Jina langu limo ndani yake.” (Kut. 23:21) Ni kweli kwamba hatuwezi kuwa hakika sana juu ya jambo hilo, lakini tunapaswa kukumbuka kwamba mbele ya kuja hapa duniani, Yesu alikuwa anaishi mbinguni na huko alikuwa “Neno,” ni kusema, Musemaji wa pekee wa Yehova kwa watumishi wake wengine.—Yoh. 1:1.