Siku ya Kwanza, 20 Mwezi wa 10
Kama hamunijulishe ndoto hiyo, pamoja na maana yake, mutakatwa vipande-vipande.—Da. 2:5.
Miaka mbili hivi kisha Wababiloni kuharibu Yerusalemu. Nebukadneza, Mufalme wa Babiloni alilota ndoto yenye ilimuogopesha kuhusu sanamu kubwa sana. Alisema kama ataua wanaume wote wenye hekima, kutia ndani Danieli kama wanashindwa kumuambia ndoto yake na kama wanashindwa kuifasiria. (Da. 2:3-5) Danieli alipaswa kutenda haraka, juu kama hangefanya vile, watu wengi wangekufa. Njo maana “aliingia na kumuomba mufalme amupatie wakati ili amufasirie mufalme maana yake.” (Da. 2:16) Ile ilionyesha kama Danieli alikuwa na uhodari na imani. Juu ya nini tunasema vile? Juu mu Biblia hamuna andiko yenye inaonyesha kama Danieli alikuwaka nafasiria ndoto zamani. Aliomba marafiki wake “wasali ili wapate rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni juu ya siri hiyo.” (Da. 2:18) Yehova alijibia sala zao. Kwa musaada wa Mungu, Danieli alifasiria ndoto ya Nebukadneza. Kwa kufanya vile, aliokoa uzima wake na wa marafiki wake. w23.08 3 fu. 4
Siku ya Pili, 21 Mwezi wa 10
Ule mwenye atavumilia mupaka mwisho ataokolewa.—Mt. 24:13.
Fikiria faida za kuwa na uvumilivu. Kama tuko na uvumilivu, tutakuwa na furaha zaidi na tutatulia zaidi. Kama tuko na uvumilivu, tunaweza kuwa na afya ya muzuri kimwili na kiakili. Kama tunavumilia wengine, tutakuwa na uhusiano wa muzuri zaidi pamoya nao. Kutaniko yetu itakuwa na umoja zaidi. Kama hatukasirike haraka wakati mutu fulani anatuchokoza, ile itafanya hali isiharibike zaidi. (Zb. 37:8, maelezo ya chini; Mez. 14:29) Lakini, zaidi ya yote, tutamuiga Baba yetu wa mbinguni na tutamukaribia hata zaidi. Uvumilivu ni sifa ya muzuri kabisa yenye inatuleteaka siye wote faida! Kusema kweli, haiko mwepesi kila mara kuwa na uvumilivu, lakini kwa musaada wa Yehova, tunaweza kuendelea kuonyesha ile sifa. Na vile tuko naendelea kungoya kwa uvumilivu dunia mupya, tuko hakika kama “jicho la Yehova linalinda wale wenye kumuogopa, wale wenye kungojea upendo wake mushikamanifu.” (Zb. 33:18) Tuazimie basi kuendelea kuvaa uvumilivu. w23.08 22 fu. 7; 25 fu. 16-17
Siku ya Tatu, 22 Mwezi wa 10
Imani yenyewe bila matendo imekufa.—Yak. 2:17.
Yakobo alionyesha kama mutu anaweza kusema kama iko na imani; lakini, je, matendo yake inaonyesha imani kabisa? (Yak. 2:1-5, 9) Yakobo anazungumuzia pia mutu mwenye anaona ‘ndugu ao dada anakosa nguo ao chakula’ lakini hamutolee musaada wenye iko nao lazima. Hata kama ule mutu anasema kama iko na imani, ile imani haionekane kupitia matendo; kwa hiyo, ile imani ni ya bure. (Yak. 2:14-16) Yakobo alizungumuzia Rahabu kuwa mufano muzuri wa kuonyesha imani kupitia matendo. (Yak. 2:25, 26) Rahabu alisikia habari kuhusu Yehova na akaamini kama ni Yehova njo alikuwa anategemeza Waisraeli. (Yos. 2:9-11) Alionyesha imani yake kupitia matendo. Alilinda wapelelezi wawili Waisraeli wakati uzima wao ulikuwa mu hatari. Ile ilikuwa na matokeo gani? Ule mwanamuke, mwenye hakamilike na mwenye hakukuwa Muisraeli, alionwa kuwa mwenye haki sawa vile tu Abrahamu. Mufano wake unaonyesha ulazima wa kuwa na imani yenye inaonekana kupitia matendo. w23.12 5-6 fu. 12-13