Isaya
“Angalia! Damasko haitakuwa muji tena,
Na itakuwa rundo la mabomoko.+
2 Miji ya Aroeri+ itaachwa;
Itakuwa mahali kwenye makundi yatakuwa yanalala,
Bila mutu wa kuyaogopesha.
3 Miji yenye ngome itakosekana katika Efraimu,+
Na ufalme katika Damasko;+
Na wale wenye kubakia wa Siria
Watakuwa kama utukufu wa Waisraeli,”* ni vile Yehova wa majeshi anasema.
5 Itakuwa kama vile wakati muvunaji anakusanya nafaka yenye kusimama
Na wakati mukono wake unavuna masuke ya nafaka,
Kama vile wakati mutu anaokota masalio ya nafaka katika Bonde* la Refaimu.+
6 Ni masalio tu ndiyo yataachwa,
Kama vile wakati muzeituni unapigwa:
Ni zeituni mbili ao tatu (3) tu zenye kukomaa ndizo zinabakia kwenye tawi la murefu zaidi,
Ni ine (4) ao tano (5) tu kwenye matawi yake yenye kuzaa matunda,”+ ni vile Yehova Mungu wa Israeli anasema.
7 Siku hiyo mwanadamu ataangalia Mutengenezaji wake, na macho yake yataangalia Mutakatifu wa Israeli. 8 Hataangalia mazabahu,+ kazi ya mikono yake;+ na hataangalia kile vidole vyake vimetengeneza, ikuwe miti mitakatifu* ao vinara vya uvumba.
9 Siku hiyo miji yake yenye ngome itakuwa kama mahali kwenye kumeachwa katika pori,+
Kama tawi lenye liliachwa mbele ya Waisraeli;
Itakuwa eneo lenye limeachwa.
11 Muchana unajengea shamba lako lupango kwa uangalifu,
Asubui unaotesha mbegu zako,
Lakini mavuno yatakosekana katika siku ya ugonjwa na maumivu yenye hayawezi kupona.+
12 Sikiliza! Kuko fujo ya vikundi vingi vya watu,
Wenye wako na muchafuko kama wa bahari nyingi!
Kuko makelele ya mataifa,
Yenye sauti yao ni kama kishindo cha maji yenye nguvu!
13 Mataifa yanatoa sauti kama kishindo cha maji mengi.
Atayakemea, na yatakimbilia mbali,
Yakifukuzwa kama maganda ya mbegu ya milima mbele ya upepo,
Kama muchongoma wenye kupeperushwa* mbele ya upepo wa zoruba.
14 Mangaribi kuko jambo lenye kuogopesha sana.
Mbele ikuwe asubui haviko tena.
Hilo ndilo fungu la wale wenye kukamata vitu vyetu kinguvu,
Na kura ya wale wenye kunyanganya vitu vyetu.