UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | ZABURI 11-18
Ni Nani Anaweza Kuwa Mugeni Katika Hema la Yehova?
Kuwa mugeni katika hema la Yehova kunamaanisha kama mutu ni rafiki ya Mungu, mutu mwenye kumutumainia na kumutii. Zaburi ya 15 inaonyesha sifa zenye Yehova anapenda marafiki wake wakuwe nazo.
MUGENI WA YEHOVA ANAPASWA . . .
kuwa muaminifu
kusema kweli, hata katika moyo wake
kuheshimia watumishi wengine wa Yehova
kutii neno lake, hata kama ni vigumu
kusaidia watu wenye kuwa na lazima ya musaada bila kutumainia faida yoyote
MUGENI WA YEHOVA ANAEPUKA . . .
kupiga porojo ao kusema mambo ya uongo juu ya wengine
kutendea jirani yake mambo mabaya
kuwapunja ndugu na dada na kuwatumikisha kwa faida yake
kufanya urafiki na watu wenye hawamutumikie Yehova ao kumutii
kukubali rushwa ao kata midomo