-
Anatoa Mifano Mbili Kuhusu Mashamba ya MizabibuYesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
-
-
SURA YA 106
Anatoa Mifano Mbili Kuhusu Mashamba Ya Mizabibu
MATAYO 21:28-46 MARKO 12:1-12 LUKA 20:9-19
MUFANO KUHUSU WATOTO WAWILI
MUFANO KUHUSU WALIMAJI WA SHAMBA LA MIZABIBU
Kwenye hekalu, Yesu anatoka tu kuwavuruga wakubwa wa makuhani na wazee wa watu, wenye walimutega kwa kumuuliza ni kwa mamlaka ya nani anafanya mambo. Jibu la Yesu linawanyamazisha. Kisha anatoa mufano wenye kuonyesha namna wako kabisa.
Yesu anaeleza: “Mutu fulani alikuwa na watoto wawili. Akamuendea wa kwanza, akamuambia, ‘Mutoto wangu, leo uende kufanya kazi katika shamba la mizabibu.’ Huyu akamujibu na kusema, ‘Sitaenda,’ lakini kisha, akasikitika na akaenda. Akamukaribia wa pili na kumuambia jambo lilelile. Huyo akajibu, ‘Nitaenda, Bwana,’ lakini hakuenda. Kati ya hao wawili, ni nani alifanya mapenzi ya baba yake?” (Matayo 21:28-31) Jibu liko wazi: ni mutoto wa kwanza mwenye mwishowe alifanya mapenzi ya baba yake.
Basi Yesu anaambia wale wenye kumupinga: “Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba wakusanya-kodi na makahaba wanawatangulia ninyi kuingia katika Ufalme wa Mungu.” Mbele, wakusanya-kodi na makahaba hawakumutumikia Mungu. Lakini, kama ule mutoto wa kwanza, walifikia kutubu na sasa wanamutumikia. Tofauti na wao, viongozi wa dini wako kama ule mutoto wa pili, wanasema kuwa wao ni watu wenye kumutumikia Mungu, lakini wanashindwa kufanya hivyo kabisa. Yesu anawaambia: “Yohana alikuja kwenu na kuwaonyesha mambo yenye kuwa sawa, lakini hamukumuamini. Hata hivyo, wakusanya-kodi na makahaba walimuamini, na hata kisha ninyi kuona jambo hilo, hamukusikitika ili mumuamini.”—Matayo 21:31, 32.
Yesu analeta mufano mwengine tena. Mara hii, Yesu anaonyesha kwamba viongozi wa dini hawashindwe tu kumutumikia Mungu, lakini wao ni waovu. Yesu anaeleza: “Mutu fulani alipanda shamba la mizabibu na kulizungushia ukuta, akachimba shimo kwa ajili ya kikamulio cha divai na akasimamisha munara; kisha akalipangisha kwa walimaji na akasafiri kuenda katika inchi ingine. Wakati kipindi chake kilifika akatuma mutumwa kwa walimaji ili akusanye kutoka kwao sehemu fulani ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wakamukamata, wakamupiga, na wakamufukuza mikono wazi. Tena akatuma mutumwa mwingine kwao, na huyo wakamupiga kwenye kichwa na kumukosea heshima. Na akatuma mwingine, na huyo wakamuua, na wengine wengi, wamoja wao wakawapiga na wengine wakawaua.”—Marko 12:1-5.
Je, watu wenye wanasikiliza Yesu wataelewa mufano huo? Pengine wanakumbuka maneno haya ya Isaya: “Shamba la mizabibu la Yehova wa majeshi ni nyumba ya Israeli; watu wa Yuda ndilo shamba lenye alikuwa anapenda sana. Aliendelea kutumaini haki, lakini angalia! kulikuwa ukosefu wa haki.” (Isaya 5:7) Ni kama tu mufano wa Yesu. Mwenye shamba ni Yehova, na shamba la mizabibu ni taifa la Israeli, lenye kukingwa na kulindwa na Sheria ya Mungu. Yehova alituma manabii ili kufundisha watu wake na kuwasaidia wazae matunda ya muzuri.
Lakini, “walimaji” walitesa na kuua “watumwa” wenye walitumwa kwao. Yesu anasema: “Mutu mumoja [mwenye shamba la mizabibu] mwenye alibakia naye alikuwa mwana wake mupendwa. Akamutuma wa mwisho, akisema: ‘Watamuheshimia mwana wangu.’ Lakini wale walimaji wakaambiana, ‘Huyu ndiye muriti. Mukuje, tumuue, na uriti utakuwa wetu. Basi wakamukamata na kumuua.”—Marko 12:6-8.
Sasa Yesu anauliza: “Mwenye shamba la mizabibu atafanya nini?” (Marko 12:9) Viongozi wa dini wanajibu: “Kwa sababu ni waovu, ataleta uharibifu mubaya juu yao na kupangisha shamba hilo la mizabibu kwa walimaji wengine, wenye watamupatia matunda kwa wakati wake.”—Matayo 21:41.
Kwa hiyo, bila kujua wanatangaza hukumu juu yao wenyewe, kwa sababu wako kati ya “walimaji” wa “shamba la mizabibu” la Yehova, ni kusema, taifa la Israeli. Matunda yenye Yehova anatazamia kwa wale walimaji inatia ndani imani katika Mwana wake, Masiya. Yesu anawaangalia viongozi hao wa dini na kuwaambia: “Je, hamujasoma hata siku moja andiko hili: ‘Jiwe lenye wajenzi walikataa ndilo limekuwa jiwe kubwa la pembe. Hili limetoka kwa Yehova, na ni la ajabu katika macho yetu’?” (Marko 12:10, 11) Kisha Yesu anawaambia waziwazi hivi: “Ndiyo sababu ninawaambia ninyi, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa taifa lenye kuzaa matunda yake.”—Matayo 21:43.
Waandishi na wakubwa wa makuhani wanatambua kama Yesu “alisema mufano huo juu yao.” (Luka 20:19) Sasa kuliko wakati mwengine wowote, wanataka kumuua mwenye kuwa na haki ya kuwa “muriti.” Lakini wanaogopa watu, wenye wanamuona Yesu kuwa nabii, kwa hiyo hawajaribu kumuua wakati huo.
-
-
Mufalme Anaita Wenye Walialikwa Kwenye Karamu ya NdoaYesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
-
-
SURA YA 107
Mufalme Anaita Wenye Walialikwa Kwenye Karamu Ya Ndoa
MUFANO WA KARAMU YA NDOA
Utumishi wa Yesu unakuwa karibu na kufika mwisho. Anaendelea kutumia mifano ili kuonyesha waziwazi tabia za waandishi na wakubwa wa makuhani. Kwa hiyo, wanataka kumuua. (Luka 20:19) Lakini Yesu anaendelea kufunua tabia zao. Anatoa mufano mwengine:
“Ufalme wa mbinguni unaweza kufananishwa na mufalme mwenye alifanyia mwana wake karamu ya ndoa. Na akatuma watumwa wake waite wale wenye walialikwa kwenye karamu ya ndoa, lakini hawakutaka kuja.” (Matayo 22:2, 3) Yesu anaanza mufano wake kwa kutaja “Ufalme wa mbinguni.” Bila shaka, “mufalme” anapaswa kuwa Yehova Mungu. Mwana wa mufalme na wale wenye kualikwa kwenye karamu ya ndoa ni nani? Hapo pia, haiko nguvu kutambua kwamba mwana wa mufalme ni Yesu, na wale wenye walialikwa ni wale wenye watakuwa pamoja na Mwana katika Ufalme wa mbinguni.
Ni nani wenye wanaalikwa wa kwanza? Yesu na mitume wamekuwa wakihubiria nani juu ya Ufalme? Wayahudi. (Matayo 10:6, 7; 15:24) Walikubali agano la Sheria katika mwaka wa 1513 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, na wakakuwa wa kwanza kupata nafasi ya kufanyiza “ufalme wa makuhani.” (Kutoka 19:5-8) Lakini, ni wakati gani wangeitwa kwenye “karamu ya ndoa”? Kwa kweli, mualiko huo ulianza katika mwaka wa 29 wakati wetu, wakati Yesu alianza kuhubiri juu ya Ufalme wa mbinguni.
Waisraeli wengi waliitikia mualiko huo namna gani? Kama vile Yesu alisema, “hawakutaka kuja.” Viongozi wengi wa dini na watu hawakukubali kama yeye ni Masiya na Mufalme mwenye aliwekwa na Mungu.
Kwa hiyo, Yesu alionyesha kwamba Wayahudi walipewa nafasi ingine: “Tena [mufalme] akatuma watumwa wengine, na kusema, ‘Muambie wale wenye walialikwa: “Muangalie! Nimetayarisha chakula changu cha muchana, ngombe-dume wangu na wanyama wenye kunona wamechinjwa, na kila kitu kiko tayari. Mukuje kwenye karamu ya ndoa.”’ Lakini kwa sababu hawakuhangaika, wakaenda, mumoja kwenye shamba lake mwenyewe, na mwingine kwenye biashara yake; lakini wengine wakakamata watumwa wake, wakawatendea kwa zarau na kuwaua.” (Matayo 22:4-6) Hilo linapatana na mambo yenye yangefanyika kisha tu kuanzishwa kwa kutaniko la Kikristo. Wakati huo, Wayahudi walikuwa wangali na nafasi ya kuwa katika Ufalme, lakini wengi walikataa mualiko huo, na hata kuwatendea mubaya ‘watumwa wa mufalme.’—Matendo 4:13-18; 7:54, 58.
Taifa hilo lilipatwa na nini? Yesu anaeleza: “Mufalme akakasirika sana, akatuma majeshi yake na kuua wale wauaji na kuchoma muji wao.” (Matayo 22:7) Wayahudi walipata matokeo hayo mabaya katika mwaka wa 70 kisha kuzaliwa kwa Yesu, wakati Waroma waliharibu “muji wao,” Yerusalemu.
Ni kusema kama hakuna mwengine mwenye angealikwa kwa sababu wao walikataa mualiko wa mufalme? Hapana, kulingana na mufano wa Yesu. Anaendelea kusema: “Kisha akaambia watumwa wake, ‘Karamu ya ndoa iko tayari, lakini wale wenye walialikwa hawakustahili. Kwa hiyo, muende kwenye barabara zenye kupeleka inje ya muji, na mualike kwenye karamu ya ndoa mutu yeyote mwenye mutapata.’ Basi watumwa hao wakaenda kwenye barabara na kukusanya wote wenye walipata, watu waovu na watu wazuri; na chumba cha karamu za ndoa kikajaa watu wenye kula chakula.”—Matayo 22:8-10.
Maneno hayo yalitimia wakati mutume Petro alisaidia watu wa mataifa, ni kusema, watu wenye hawakuwa Wayahudi kwa kuzaliwa ao kwa kugeuzwa imani, ili wakuwe Wakristo wa kweli. Katika mwaka wa 36 kisha kuzaliwa kwa Yesu, mukubwa wa jeshi Muroma Kornelio na familia yake walipokea roho ya Mungu, na kupata tumaini la kuwa sehemu ya ufalme wa mbinguni wenye Yesu alizungumuzia.—Matendo 10:1, 34-48.
Yesu anaonyesha kama haiko wote wenye kuja kwenye karamu ndio mwishowe watakubaliwa na “mufalme.” Anasema: “Wakati mufalme aliingia ili kuchunguza wageni, akaona mutu mwenye hakukuwa anavaa nguo ya ndoa. Basi akamuuliza, ‘Mwenzangu, uliingia humu namna gani bila nguo ya ndoa?’ Akakosa la kusema. Halafu mufalme akaambia watumishi wake, ‘Mumufunge mikono na miguu, kisha mumutupe inje katika giza. Ni kule atalia na kusaga meno yake.’ Kwa maana wenye walialikwa ni wengi, lakini wenye walichaguliwa ni wachache.”—Matayo 22:11-14.
Pengine viongozi wa dini hawaelewe maana ao mambo yote yenye iko anazungumuzia. Lakini, wanachukizwa na wanaazimia hata zaidi kuondolea mbali mutu mwenye kuwapatisha haya hivyo.
-
-
Wanashindwa Kumunasa Yesu Katika Mitego YaoYesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
-
-
SURA YA 108
Wanashindwa Kumunasa Yesu Katika Mitego yao
MATAYO 22:15-40 MARKO 12:13-34 LUKA 20:20-40
VITU VYA KAISARI KWA KAISARI
WENYE WATAFUFULIWA WATAFUNGA NDOA?
AMRI ZENYE KUWA KUBWA ZAIDI
Maadui wa Yesu wanakasirika. Ametoka tu kuzungumuzia mifano yenye kufunua uovu wao. Sasa Wafarisayo wanataka kumutega. Wanapenda aseme jambo fulani lenye litafanya wamutoe kwa gavana Muroma, na wanalipa wanafunzi wao fulani ili wamunase katika mitego.—Luka 6:7.
Wanamuambia hivi: “Mwalimu, tunajua wewe unasema na kufundisha bila kukosea na hauna ubaguzi, lakini unafundisha njia ya Mungu kupatana na kweli: Je, tunaruhusiwa kulipa Kaisari kodi ya kichwa ao hapana?” (Luka 20:21, 22) Yesu hadanganywe na maneno yao yenye kuonekana kuwa ya muzuri, kwa sababu yanaficha ujanja na unafiki wao. Kama anasema, ‘Hapana, hamupaswe kulipa kodi hiyo,’ atashitakiwa kuwa mutu mwenye anataka kupindua utawala wa Roma. Lakini kama anasema, ‘Ndiyo, mulipe kodi,’ watu wenye hawapendi kutawaliwa na Waroma watakasirika na kumugeukia. Basi, anajibu namna gani?
Yesu anajibu hivi: “Sababu gani munanijaribu, ninyi wanafiki? Munionyeshe feza moja ya kichele ya kodi.” Wakamuletea dinari. Akawaambia: “Sura hii na muandiko huu ni ya nani?” Wakasema: “Ni ya Kaisari.” Kisha Yesu akawatolea muongozo wa muzuri sana: “Basi, mulipe Kaisari vitu vya Kaisari, lakini Mungu vitu vya Mungu.”—Matayo 22:18-21.
Watu hao wanashangazwa na maneno ya Yesu. Kisha kunyamazishwa na jibu lake lenye hekima, wanaenda zao. Lakini siku ingali inaendelea, na mitego ya kumunasa haijamalizika. Kisha Wafarisayo kushindwa kumunasa, viongozi wa kikundi kingine cha dini wanamukaribia Yesu.
Wasadukayo, wenye wanasema kama hakuna ufufuo, wakamuuliza ulizo kuhusu ufufuo na ndoa kati ya mutu na bibi ya ndugu yake. Wanauliza: “Mwalimu, Musa alisema: ‘Kama mutu yeyote anakufa bila kupata watoto, ndugu yake anapaswa kumuoa bibi yake na kumuinulia ndugu yake uzao.’ Sasa kulikuwa ndugu saba (7) katikati yetu. Wa kwanza akaoa na akakufa, na kwa sababu hakukuwa na uzao wowote, akamuachia ndugu yake bibi yake. Ikakuwa vilevile kwa ule wa pili na wa tatu (3), mupaka wote saba (7). Mwishowe, ule mwanamuke naye akakufa. Basi, wakati wa ufufuo, ule mwanamuke atakuwa bibi ya nani kati ya hao saba (7)? Kwa maana alikuwa bibi yao wote.”—Matayo 22:24-28.
Yesu anatumia maandishi ya Musa yenye kukubaliwa na Wasadukayo, kwa kusema hivi: “Munakosea, kwa sababu hamujue Maandiko wala nguvu za Mungu. Kwa maana wakati wanafufuliwa kutoka kwa wafu, wanaume hawaoe na wanamuke hawaolewe, lakini wao ni kama malaika wa mbinguni. Hata hivyo, kuhusu kufufuliwa kwa wafu, je, hamukusoma katika kitabu cha Musa, katika habari kuhusu ule muti mudogo wa miiba, kwamba Mungu alimuambia: ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo’? Yeye haiko Mungu wa wafu, lakini ni Mungu wa wazima. Mumekosea sana.” (Marko 12:24-27; Kutoka 3:1-6) Watu wakashangazwa na jibu lake.
Yesu amewanyamazisha Wafarisayo na Wasadukayo, kwa hiyo, viongozi hawa wapinzani wanajiunga pamoja ili kuja kumujaribu tena. Mwandishi mumoja anamuuliza: “Mwalimu, ni amri gani ndiyo kubwa zaidi katika Sheria?”—Matayo 22:36.
Yesu anajibu: “Ya kwanza ni hii, ‘Sikia, Ee Israeli, Yehova Mungu wetu ni Yehova mumoja, na unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.’ Ya pili ni hii, ‘Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.’ Hakuna amri nyingine yenye kuwa kubwa zaidi kuliko hizi.”—Marko 12:29-31.
Wakati ule mwandishi alisikia jibu hilo, akajibu hivi: “Mwalimu, umesema muzuri kupatana na kweli, ‘Yeye ni Mumoja, na hakuna mwingine isipokuwa yeye’; na mutu kumupenda kwa moyo wake wote, na kwa uelewaji wake wote, na kwa nguvu zake zote, na pia kumupenda jirani yake kama yeye mwenyewe ni muzuri sana kuliko matoleo yote mazima ya kuteketezwa na zabihu.” Halafu Yesu, wakati alitambua kwamba amejibu kwa hekima, akamuambia: “Wewe hauko mbali na Ufalme wa Mungu.”—Marko 12:32-34.
Kwa muda wa siku tatu (Nisani 9, 10, na 11) Yesu amekuwa akifundisha katika hekalu. Watu fulani, kama vile ule mwandishi, wamefurahia kumusikiliza. Lakini hapana viongozi wa dini, wenye sasa ‘hawawezi tena kumuuliza ulizo.’
-
-
Anakemea Waziwazi Viongozi Wa Dini Wenye KumupingaYesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
-
-
SURA YA 109
Anakemea Waziwazi Viongozi Wa Dini Wenye Kumupinga
MATAYO 22:41–23:24 MARKO 12:35-40 LUKA 20:41-47
KRISTO NI MWANA WA NANI?
YESU ANAFUNUA UNAFIKI WA WATU WENYE KUMUPINGA
Viongozi wa dini wenye kumupinga Yesu wanashindwa kumuharibishia Yesu sifa ao kumunasa katika mutego ili wamutoe kwa Waroma. (Luka 20:20) Sasa, wakati angali kwenye hekalu tarehe 11 Mwezi wa Nisani, Yesu anawageukia na kuwaonyesha yeye ni nani. Yeye ndiye anaanzisha mazungumuzo. Anawauliza hivi: “Munawaza nini juu ya Kristo? Yeye ni mwana wa nani?” (Matayo 22:42) Inajulikana muzuri kwamba Kristo, ao Masiya, anapaswa kuwa katika kizazi cha Daudi. Na ni hivyo wanamujibu.—Matayo 9:27; 12:23; Yohana 7:42.
Yesu anauliza: “Basi, sababu gani Daudi kwa kuongozwa na roho anamuita Kristo Bwana, wakati anasema, ‘Yehova alimuambia Bwana wangu: “Kaa kwenye mukono wangu wa kuume mupaka niweke maadui wako chini ya miguu yako”’? Basi, kama Daudi anamuita Bwana, yeye ni mwana wake namna gani?”—Matayo 22:43-45.
Wafarisayo wanabakia kimya, kwa sababu wanatumainia kupata mutu wa kizazi cha Daudi ili awakomboe kutoka katika mikono ya Waroma. Lakini akitumia maneno ya Daudi yenye kupatikana katika Zaburi 110:1, 2, Yesu anaonyesha kwamba Masiya hapaswe kuwa tu mutawala mwanadamu. Yeye ni Bwana wa Daudi, na kisha kukaa kwenye mukono wa kuume wa Mungu, ataanza kutawala. Jibu la Yesu linanyamazisha waandishi na Wafarisayo.
Wanafunzi na wengine wengi wamekuwa wakisikiliza. Sasa Yesu anaanza kuzungumuza nao na kuwaambia wafanye angalisho na waandishi na Wafarisayo. Wao “wamejiikalisha katika kiti cha Musa” ili kufundisha Sheria ya Mungu. Yesu anaelezea hivi wasikilizaji wake: “Mambo yote yenye wanawaambia, muyafanye na kuyashika, lakini musitende kulingana na matendo yao, kwa maana wao wanasema lakini hawatende mambo yenye wanasema.”—Matayo 23:2, 3.
Kisha Yesu anawapatia mifano ya unafiki wao, na kusema: “Kwa maana wanapanua visanduku vyenye kuwa na maandiko ndani vyenye wanavaa kama ulinzi.” Wayahudi fulani walivaa kwenye paji la uso ao kwenye mukono visanduku vidogo kama hivyo vyenye vilikuwa na maneno ya Sheria. Wafarisayo wananenepesha visanduku vyao ili kuonyesha watu kama wako na bidii kuhusu Sheria. Tena, “wanarefusha sehemu za chini za nguo zao.” Waisraeli walipaswa kutia uzi kwenye sehemu ya chini ya nguo zao, lakini Wafarisayo walirefusha sehemu hizo za chini kwenye nguo zao. (Hesabu 15:38-40) Wanafanya yote hayo “ili waonekane na watu.”—Matayo 23:5.
Hata wanafunzi wa Yesu wangeambukizwa na tamaa hiyo ya kutaka makubwa, kwa hiyo anawashauria hivi: “Lakini ninyi, musiitwe Rabi, kwa maana Mwalimu wenu ni mumoja, na ninyi wote ni ndugu. Zaidi ya hayo, musiite mutu yeyote baba yenu duniani, kwa maana Baba yenu ni mumoja, Ule wa mbinguni. Wala musiitwe viongozi, kwa maana Kiongozi wenu ni mumoja, Kristo.” Kwa hiyo basi, wanafunzi wanapaswa kuwa na mawazo gani juu yao na wanapaswa kutenda namna gani? Yesu anawaambia: “Lakini mwenye kuwa mukubwa zaidi kati yenu anapaswa kuwa mutumishi wenu. Kila mutu mwenye kujiinua atanyenyekezwa, na kila mutu mwenye kujinyenyekeza atainuliwa.”—Matayo 23:8-12.
Tena, Yesu anatangazia waandishi na Wafarisayo wanafiki ole mbalimbali zenye kufuatana. Anasema hivi: “Ole kwenu, waandishi na Wafarisayo, wanafiki! kwa sababu munafungia watu Ufalme wa mbinguni; kwa maana ninyi wenyewe hamuingie, na wale wenye wanataka kuingia munawazuia.”—Matayo 23:13.
Yesu anakemea Wafarisayo sababu hawajue mambo ya maana kulingana na mawazo ya Yehova. Kwa mufano, wanasema: “Kama mutu yeyote anaapa kwa hekalu, hakuna ubaya; lakini kama mutu yeyote anaapa kwa zahabu ya hekalu, anapaswa kutimiza kiapo chake.” Kwa kukazia sana akili yao juu ya zahabu yenye kuwa kwenye hekalu kuliko kukazia ibada yenye inapaswa kutolewa kwenye hekalu, wanaonyesha kwamba wao ni vipofu. Na ‘wamepuuza mambo mazito zaidi ya Sheria, ni kusema, haki, rehema, na uaminifu.’—Matayo 23:16, 23; Luka 11:42.
Yesu anaita Wafarisayo hawa ‘viongozi vipofu, wenye kuchuya imbu lakini wanameza ngamia!’ (Matayo 23:24) Wanatosha imbu katika divai yao wakati wa karamu kwa sababu kidudu hicho hakiko safi. Lakini kupuuza mambo mazito ya Sheria ni kama vile kumeza ngamia mwenye pia wakati wa karamu ni munyama muchafu, tena mukubwa sana.—Mambo ya Walawi 11:4, 21-24.
-