Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w10 1/10
  • 6 Sala Inaweza Kutusaidia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 6 Sala Inaweza Kutusaidia?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kumukaribia Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Namna Yehova Anajibiaka Sala Zetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Utangulizi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Namna ya Kufanya Sala Zetu Zikuwe Muzuri Zaidi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
w10 1/10

6 Sala Inaweza Kutusaidia?

SALA inaweza kutusaidia? Jibu ni ndiyo, juu Biblia inaonyesha kama sala za watumishi waaminifu wa Mungu zilikuwa zinawasaidia. (Luka 22:40; Yakobo 5:13) Sala inaweza kabisa kutusaidia tukuwe na urafiki muzuri na Mungu, na tujisikie muzuri. Namna gani?

Kwa mufano, tunapendaka kusema aksanti wakati tunapokea zawadi. Juu ya nini ni muzuri kufanya vile? Juu wakati tunaonyesha shukrani yetu, tunajisikia kuwa wenye shukrani zaidi. Ni vile pia wakati tunazungumuza na Mungu. Juu ya nini tunasema vile? Tuone mifano fulani.

Sala za shukrani. Wakati tunamushukuru Baba yetu juu ya mambo ya muzuri yenye iko anatufanyia, tunaonyesha kama tuko tunaona ile mambo. Ile inafanya tukuwe wenye shukrani zaidi, wenye furaha zaidi, na tukuwe na mawazo ya muzuri zaidi.​—Wafilipi 4:6.

Kwa mufano: Yesu alimushukuru Baba yake, juu alisikiliza na kujibia sala zake.​—Yohana 11:41.

Sala za kuomba musamaha. Wakati tunamuomba Mungu musamaha, zamiri yetu inatumika muzuri zaidi, tunaonyesha kama tunahuzunika juu ya mambo yenye tulifanya, na tunatambua kama ni jambo ya maana kumutii Mungu. Pia, ile inatusaidia tusijilaumu kupita kiasi.

Kwa mufano: Daudi alisali juu ya kuonyesha kama anatubu na kama anahuzunikia mambo yenye alifanya.​—Zaburi 51.

Sala za kuomba muongozo na hekima. Kumuomba Yehova atuongoze na atupatie hekima juu tukamate maamuzi ya muzuri, kunatusaidia tukuwe wanyenyekevu kabisa. Tena, kunatusaidia tukumbuke kama kuko mambo yenye hatuna uwezo wa kufanya. Na tena, kunatusaidia tumutumainie zaidi Baba yetu wa mbinguni.​—Mezali 3:5, 6.

Kwa mufano: Sulemani alimuomba Mungu amuongoze na amupatie hekima juu aweze kuongoza muzuri Israeli.​—1 Wafalme 3:5-​12.

Sala za wakati wa magumu. Kama tunamuambia Mungu magumu yetu, tutajisikia kuwa wenye kutulia na tutamutumainia zaidi kuliko kujitumainia siye wenyewe.​—Zaburi 62:8.

Kwa mufano: Mufalme Asa alisali wakati adui mubaya alikuwa anapenda kumushambulia.​—2 Mambo ya Nyakati 14:11.

Sala kwa ajili ya watu wenye wako na lazima ya musaada. Sala za vile zinatusaidiaka tusikuwe watu wenye kujifikiria wenyewe tu, tukuwe wenye huruma zaidi, na wenye kujitia pa fasi ya wengine.

Kwa mufano: Yesu alisali kwa ajili ya wanafunzi wake.​—Yohana 17:9-​17.

Sala za kumusifu Mungu. Wakati tunamusifu Yehova juu ya mambo ya ajabu yenye amefanya na juu ya sifa zake, tunamuheshimia zaidi na tunamuona kuwa wa maana zaidi. Tena, sala za vile zinatusaidia tumukaribie zaidi Mungu wetu na Baba yetu.

Kwa mufano: Daudi alimusifu Mungu sana, juu ya vitu vyenye aliumba.​—Zaburi 8.

Faida ingine yenye tunapata wakati tunasali ni “amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote.” (Wafilipi 4:7) Haiko mwepesi kupata amani ya akili mu hii dunia yenye inayala muvurugo. Kukuwa na amani ya akili kunaweza hata kutusaidia tukuwe na afya ya muzuri. (Mezali 14:30) Lakini tunaweza kupata amani ya akili kwa nguvu yetu wenyewe? Ao kuko jambo ingine ya maana yenye tunapaswa kufanya?

Sala iko na faida mingi; inatusaidia tujisikie muzuri, na zaidi sana inatusaidia tukuwe na urafiki muzuri na Mungu

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine