MAISHA YA MUKRISTO
Upendo wa Kweli Ni Nini?
Yehova alianzisha ndoa ili mwanaume na mwanamuke waishi pamoja maisha yao yote. (Mwa 2:22-24) Wanaweza kuachana kama tu mumoja wao anafanya uzinifu. (Mal 2:16; Mt 19:9) Kwa sababu Yehova anapenda ndoa ikuwe yenye furaha, ametolea Wakristo kanuni zenye zinaweza kuwasaidia wachague bibi ao bwana kwa hekima, na waendelee kuwa na furaha katika ndoa.—Mhu 5:4-6.
MUANGALIE KWENU VIDEO UPENDO WA KWELI NI NINI? KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:
Sababu gani mashauri yenye Frank na Bonnie walimutolea mutoto yao Mamie, ilikuwa yenye hekima na upendo?
Sababu gani kuwaza kama unaweza kubadilisha tabia za muchumba wako ni kukosa hekima?
Paul na Priscilla walimutolea Mamie shauri gani lenye hekima?
Sababu gani Patrick na Rachel walipata magumu katika ndoa yao?
Jonathan na Mamie walikuwa na mipango gani ya kiroho yenye kufanana?
Sababu gani unapaswa kufikia kujua ‘ule mutu wa siri wa moyoni’ wa mutu mbele ya kufanya naye naziri ya ndoa? (1Pet 3:4)
Upendo wa kweli ni nini? (1Kor 13:4-8)