-
Kwa WazaziNinajifunza Biblia
-
-
Kwa Wazazi
Ni zawadi gani nzuri zaidi munayoweza kuwapatia watoto wenu? Watoto wenu wanahitaji mambo mengi katika maisha yao. Lakini musisahau kwamba wanahitaji pia upendo, muongozo na ulinzi wenu. Hata hivyo, zawadi nzuri kuliko zote ambayo munaweza kuwapatia ni hii: kuwasaidia kumujua Yehova na kujua mafundisho ya Neno lake, Biblia. (Yohana 17:3) Ujuzi huo unaweza kuwasaidia watoto wenu wamupende Yehova sana na wamutumikie kwa moyo wao wote, hata tangu utoto.—Mathayo 21:16.
Wazazi wengi wametambua kwamba kwa kawaida watoto wadogo wanafurahia mafundisho mafupi yanayotolewa kwa njia ya michezo. Kwa hiyo, tunafurahi sana kuwatolea broshua hii yenye kichwa, Ninajifunza Biblia. Kila somo limetayarishwa ili kufundisha mutoto kwa njia nyepesi. Picha na maandishi yanayofasiria picha hizo vimetayarishwa ili kufundisha zaidi sana watoto wasiozidi miaka 3. Katika kila somo muna mashauri yanayoonyesha namna ya kufanya mazoezi hayo ao michezo hiyo. Broshua hii haikutayarishwa ili kucheza tu na watoto; lakini, imekusudiwa uisome na watoto wako, na hilo linaweza kukusaidia kuzungumuza nao.
Tunatumaini kwamba broshua hii itakusaidia kufundisha watoto wako kweli ya Biblia “tangu utoto”—2 Timotheo 3:14, 15.
Ndugu zenu,
Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova
[Picha katika ukurasa wa 3]
-
-
Somo 1Ninajifunza Biblia
-
-
Somo 1
Ni nani aliyeumba dunia?
Ni nani aliyeumba bahari?
Ni nani aliyetuumba mimi na wewe?
Ni nani aliyeumba kipepeo na mabawa yake yenye rangi-rangi?
Ni Yehova Mungu ndiye aliyeumba vitu vyote.
MAZOEZI
Umusomee mutoto wako:
Umuombe aonyeshe:
Nyota Mawingu Jua
Mashua Dunia Nyumba
Bahari Kipepeo
Umuulize mutoto wako:
Jina la Mungu ni nani?
Yehova iko wapi?
Yehova aliumba nini?
[Picha katika ukurasa wa 4, 5]
-
-
Somo 2Ninajifunza Biblia
-
-
Somo 2
Angalia wanyama karibu na safina ya Noa.
Ni wanyama gani wanaolia: moo, na ni wanyama gani wanaolia: wuu?
Wanyama wa aina yote, wadogo a wakubwa, safina ya Noa iliwaokoa wote.
MAZOEZI
Umusomee mutoto wako:
Umuombe aonyeshe:
Dubu Mbwa Tembo
Twiga (Girafe) Simba Makako
Nguruwe Kondoo
Pundamilia (Zèbre) Upinde wa mvua
Umuombe mutoto wako aige mulio wa wanyama hawa:
Mbwa Simba Makako
Nguruwe Kondoo
[Picha katika ukurasa wa 6, 7]
-
-
Somo 3Ninajifunza Biblia
-
-
Somo 3
Rafiki ya Kalebu ni mugonjwa.
Basi, Kalebu anasema, nitafanya hivi:
“Nitamuandikia barua ili akuwe na furaha, kisha nitamupelekea barua hiyo!”
Kuonyesha rafiki yako wema, kutawafanya ninyi wawili mukuwe na furaha!
MAZOEZI
Umusomee mutoto wako:
Umuombe aonyeshe:
Nyumba Meza Kalebu
Jua Ndege Muti
Umuulize mutoto wako:
Unajua mutu fulani ambaye ni mugonjwa? Tunaweza kufanya nini ili akuwe na furaha?
[Picha katika ukurasa wa 8]
[Picha katika ukurasa wa 8]
[Picha katika ukurasa wa 9]
[Picha katika ukurasa wa 9]
-
-
Somo 4Ninajifunza Biblia
-
-
Somo 4
Leo mvua inanyesha.
“Siwezi kutoka inje.
Sababu gani mvua haiishe?”
Safi analia.
Kisha anashangaa!
Jua inatokea.
Mvua imekwisha.
Safi anafurahi sana!
Anakimbilia inje, anaruka-ruka. Safi anaona vitu vyenye kupendeza.
Safi anasema: “Sikujua kama mvua inayotoka kwa Mungu inakomalisha maua!”
MAZOEZI
Umusomee mutoto wako:
Umuombe aonyeshe:
Dirisha Ndege Safi
Muti Maua
Umuombe mutoto wako aonyeshe vitu visivyoonekana muzuri.
Kidudu Avion
Umuulize mutoto wako:
Sababu gani Yehova anafanya mvua inyeshe?
[Picha katika ukurasa wa 10]
[Picha katika ukurasa wa 10]
[Picha katika ukurasa wa 11]
-
-
Somo 5Ninajifunza Biblia
-
-
Somo 5
Ikiwa rafiki yako anakupatia zawadi ao anakufanyia jambo muzuri, usikose kumuambia aksanti—ao aksanti sana!
Hata ukuwe wapi na hata ukuwe unafanya nini, Kila siku usisahau kusema “Aksanti!”
MAZOEZI
Umusomee mutoto wako:
Umuombe aonyeshe:
Zawadi Mutoto mwanaume
Mulango Chakula
Umuombe mutoto wako aonyeshe vitu visivyoonekana muzuri.
Tunda Telefone
Umuulize mutoto wako:
Sababu gani ni vizuri kusema “Aksanti”?
[Picha katika ukurasa wa 12]
[Picha katika ukurasa wa 13]
[Picha katika ukurasa wa 13]
[Picha katika ukurasa wa 13]
-
-
Somo 6Ninajifunza Biblia
-
-
Somo 6
Angalia vidole vya mikono yako, na uchezeshe-chezeshe vidole vya miguu yako.
Onyesha masikio yako na kisha uonyeshe pua yako.
Angalia miguu yako inayokusaidia kukimbia, kuruka na kuzunguka, na kufurahia michezo mbalimbali!
Angalia katika kioo, unaona nini?
Yehova aliumba kila kitu kwa njia ya ajabu!
MAZOEZI
Umusomee mutoto wako:
Umuombe aonyeshe:
Vidole vya mikono yake Vidole vya miguu yake Pua yake
Masikio yake Kinywa chake
Umuombe mutoto wako aonyeshe vitu visivyoonekana muzuri.
Lipondo Paka
Umuulize mutoto wako:
Ni nani aliyetuumba mimi na wewe?
[Picha katika ukurasa wa 14]
[Picha katika ukurasa wa 15]
[Picha katika ukurasa wa 15]
[Picha katika ukurasa wa 16]
-