Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 10/15 uku. 12-13
  • Wakati Unalazimika Kurudia Nyumbani

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wakati Unalazimika Kurudia Nyumbani
  • Amuka!—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAGUMU
  • Namna ya Kutumia Feza Vizuri
    Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha
  • Namna ya Kutumia Feza Vizuri
    Amuka!—2014
  • 2 | Ulinde Mali Yako
    Amuka!—2022
  • Kushugulikia Madeni
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2015
g 10/15 uku. 12-13
Wazazi wanafungua mulango wakati mutoto wao muzima mwanaume anarudia nyumbani

MUSAADA KWA FAMILIA | VIJANA

Wakati Unalazimika Kurudia Nyumbani

MAGUMU

Vijana fulani wazima wameondoka nyumbani, wamepima kuishi maisha yao wenyewe, lakini wamepata magumu ya feza na wamelazimika kurudia nyumbani. Jambo hilo limekwisha kukufikia?

Hata kama unapenda baba na mama yako, inaweza kuwa vigumu kurudia nyumbani. Kwa mufano, kijana mwanamuke mwenye kuitwa Saraha anasema hivi: “Kuishi mimi mwenyewe kulinisaidia kujiaminia kwa sababu sikukuwa na lazima ya kutegemea wengine. Lakini kurudia nyumbani kulinifanya nijisikie kama mutoto tena.” Kijana mwanaume mwenye kuitwa Richard alijisikia pia hivyo. Anasema hivi: “Sikupenda kurudia nyumbani lakini sikuweza tena kujitegemeza. Nilijisikia kuwa ninashindwa.”

Ikiwa uko katika hali kama hiyo, habari hii inaweza kukusaidia uanze tena kujitegemeza.

SABABU GANI JAMBO HILO LINATOKEA?

Magumu ya feza. Vijana wengi wanashangaa wakati wanaondoka nyumbani, mara moja wanaona kama inaomba feza nyingi ili kuishi maisha yao wenyewe. Richard, mwenye tumekwisha kutaja, anasema hivi: “Feza zote zenye nilikuwa ninaweka ziliisha kwa sababu ya kujitegemeza mimi mwenyewe.” Kijana mwanamuke mwenye kuitwa Shaina alipatwa pia na magumu hayo. Aliondoka nyumbani wakati alikuwa na miaka 24 na alirudia kisha mwaka moja na nusu. Anasema hivi: “Ningetumikisha feza zangu muzuri. Niliondoka nyumbani bila feza, na nilirudia na deni.”b

Magumu ya kazi. Kupoteza kazikunaweza hata kuvuruga mipango mizuri zaidi ya mutu mwenye maisha ya kujitegemea. Shaina alitambua jambo hilo. Anasema hivi: “Nilimaliza masomo ya kuwa muganga, na nilijiunga na shirika moja lenye lilinisaidia kupata kazi. Lakini wakati nilipoteza kazi, sikukuwa na la kufanya. Nilikuwa ninaishi katika kijiji (eneo la mashambani), na sikukuwa na tumaini la kupata kazi ingine katika mambo ya matunzo!”

Kutumainia mambo yenye hayawezi kutimizwa. Vijana fulani wazima wanaanza kazi bila kujitayarisha, hawajue kile kinahitajiwa ili kupata mambo ya lazima katika maisha. Mara nyingi kazi yao ni ngumu zaidi kuliko vile walitumainia. Wanashangaa kutambua kama kujitegemea hakuwavutie tena kama vile walitumainia. Hawakuwazia kabisa kama kuwa mutu muzima kungeleta magumu mengi.

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Uzungumuze na wazazi wako juu ya kurudia nyumbani. Uzungumuzie mambo kama vile: Utakuwa na lazima ya kuishi nyumbani kwa muda gani? Wakati utakuwa nyumbani, namna gani utachangia ili kulipia mambo mbalimbali ya nyumbani? Ni kazi gani za nyumbani unaweza kusaidia kufanya? Utafanya nini ili upate tena feza za kujitegemeza? Hata kama uko na miaka ngapi, kumbuka kama unarudia katika nyumba ya wazazi wako na unapaswa kutii sheria zao.—Kanuni ya Biblia: Kutoka 20:12.

Ujifunze kutumia feza zako muzuri. Kitabu kimoja (The Complete Guide to Personal Finance: For Teenagers and College Students) kinasema hivi: “Namna unatumia feza zako inachangia sana kuonyesha ikiwa unaweza kupanga namna ya kuzitumia muzuri ili kujitegemeza mwenyewe ao hapana. . . . Kuacha kutumia feza zako juu ya vitu vyenye hauna navyo lazima ni wazo la maana lenye unapaswa kuelewa.”—Kanuni ya Biblia: Luka 14:28.

Utafute mashauri ya muzuri. Wazazi ao watu wengine wazima wanaweza kukusaidia ujue kuweka feza kwenye benki, kupanga namna ya kutumia feza zako, na namna ya kulipia garama zako. Kijana mwanamuke mwenye kuitwa Marie anasema hivi: “Nilipaswa kujifunza tena mambo ya musingi. Rafiki fulani alinisaidia kufanya liste ya vitu vya lazima na vyenye haviko vya lazima. Sikuweza kuamini: vitu vingi vyenye nilikuwa ninauza havikukuwa vya lazima kabisa! Tena, nilijifunza namna ya kukomalisha sifa ya kujizuia yenye mutu mwenye maisha ya kujitegemea anapaswa kuwa nayo.”—Kanuni ya Biblia: Methali 13:10.

Jambo la lazima haiko kazi yenye unafanya lakini ni kufanya kazi yako muzuri zaidi

Ujikaze kutafuta kazi. Kwa sababu hauna kazi, utumie wakati wako ili kutafuta kazi. Angalisho: Watu fulani wanaweza kukuambia utafute tu kazi yenye ulipanga kufanya katika maisha. Lakini hilo linaweza kufanya ukuwe na uwezekano mudogo wa kupata kazi na upoteze nafasi za kupata kazi zenye zinajitokeza! Kuliko kupoteza wakati wako ili kutafuta tu kazi ya aina fulani, ukuwe tayari kufanya kazi mbalimbali. Kumbuka kama jambo la lazima haiko kazi yenye unafanya lakini ni kufanya kazi yako muzuri zaidi. Kwa kweli, imeonekana kama wakati wafanyakazi wanazoea kazi yao na kuijua muzuri zaidi, wanaifurahia zaidi. Haiko lazima ufanye kazi yenye unapenda ili ufurahie kazi hiyo!

a Majina yamebadilishwa katika habari hii.

b Katika inchi ya Amerika, mara nyingi wanafunzi wa masomo ya juu wanapatwa na magumu kama hayo. Kulingana na ripoti moja katika gazeti The Wall Street Journal, mwanafunzi mwenye kuwa na mukopo, kwa kukadiria, anamaliza masomo na deni la dola 33 000.

MAANDIKO YA MAANA

  • ‘Umuheshimu baba yako na mama yako.’—Kutoka 20:12.

  • ‘Ni nani kati yenu anayetaka kujenga munara ambaye haketi kwanza na kuhesabu garama, ili aone kama ana kiasi cha kutosha kuukamilisha [kuumaliza]?’—Luka 14:28.

  • “Wale wanaoshauriana pamoja wana hekima.”—Methali 13:10.

KWA WAZAZI

Mutumie wakati wenye watoto wangali nyumbani ili kuwafundisha ufundi mbalimbali wa lazima wenye utawasaidia kuishi maisha ya kujitegemea. Ufundi huo unaweza kuwa kupanga namna ya kutumia feza (kama vile kutumia feza muzuri na feza za mukopo), kazi za nyumbani (kupika, kufua na kupiga pasi, na namna ya kutengeneza mambo ya lazima katika motokari), uwezo wa kuishi muzuri na watu (kupatana na watu wengine).

Ili kupata habari zingine, soma kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1, ukurasa wa 305 na 306, chenye kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova. Kinapatikana kwenye adresi yetu ya Internete www.pr2711.com/sw. Fungua kichwa MACHAPISHO > VITABU NA BROSHUA.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine