Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Tia Nguvu Imani Yako Katika Mambo Yenye Unatumainia
    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2016 | Mwezi wa 10
    • 2 Biblia inasema kama imani ni “tarajio lililohakikishwa” la mambo yenye tunatumainia. Hilo linamaanisha kama wale wenye kuwa na imani wako kabisa hakika kama mambo yenye Yehova ameahidi yatatimia. (Waebrania 11:1) Hata hivyo, watu wengi leo wanatumainia na kungojea kwa hamu mambo fulani, lakini hawako hakika kama mambo hayo yatatimia kabisa. Kwa mufano, mutu fulani anaweza kutumainia kama atapata ushindi katika muchezo fulani wa bahati, lakini hawezi kuwa hakika kabisa kama atapata ushindi huo. Katika habari hii, tutaona mambo yenye tunaweza kufanya ili kutia nguvu imani yetu katika ahadi za Mungu. Tutazungumuzia pia namna imani yenye nguvu inaweza kutusaidia leo.

      3. Sababu gani tuko na imani kama ahadi za Mungu zitatimia?

      3 Hakuna mutu kati yetu mwenye alizaliwa na imani. Ili tukuwe na imani, tunapaswa kuacha roho takatifu ya Mungu iongoze mioyo yetu. (Wagalatia 5:22) Roho takatifu inaweza kutusaidia tumujue Yehova. Wakati tunaelewa kama Yehova ni mweza-yote na ni mwenye hekima, tunakuwa hakika kama ana uwezo wa kutimiza mambo yote yenye ameahidi. Yehova mwenyewe anazungumuzia ahadi zake kama vile zimekwisha kutimia. Anasema hivi: “Yamekuwa!” (Soma Ufunuo 21:3-6.) Tunajua kama Yehova anatimiza sikuzote mambo yenye anaahidi. Yeye ni ‘Mungu muaminifu.’ Ndiyo sababu tunaamini mambo yote yenye anatuambia juu ya wakati unaokuja.​—Kumbukumbu la Torati 7:9.

      WATUMISHI WA MUNGU WA WAKATI WA ZAMANI WENYE WALIKUWA NA IMANI YENYE NGUVU

      4. Watumishi wa Mungu wa wakati wa zamani walikuwa na imani katika mambo gani?

      4 Sura ya 11 ya kitabu cha Waebrania inazungumuzia majina ya wanaume na wanawake 16 wenye walikuwa na imani yenye nguvu katika ahadi za Yehova. Inazungumuzia pia wengine wengi wenye walifurahisha Yehova “kupitia imani yao.” (Waebrania 11:39) Watu hao wote walikuwa wanangojea “uzao” wenye Yehova alikuwa ameahidi. Walijua kama “uzao” huo ungeharibu maadui wote wa Mungu na kufanya dunia ikuwe tena paradiso. (Mwanzo 3:15) Na watumishi hao wa Mungu walikuwa na imani yenye nguvu kuwa Yehova angewafufua. Kwa kweli, hawakungojea wafufuliwe ili kuishi mbinguni, kwa sababu Yesu hakukuwa amekwisha kufanya jambo hilo liwezekane. (Wagalatia 3:16) Lakini, walingojea kwa hamu kuishi milele katika paradiso ya muzuri sana hapa duniani.​—Zaburi 37:11; Isaya 26:19; Hosea 13:14.

  • Tia Nguvu Imani Yako Katika Mambo Yenye Unatumainia
    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo)—2016 | Mwezi wa 10
    • 7. Yehova ametupatia nini ili kutia nguvu imani yetu, na tunapaswa kufanya nini?

      7 Ni nini itatusaidia tuendelee kuwa na imani yenye nguvu? Yehova ametupatia Biblia ili kutufundisha juu ya ahadi zake za wakati unaokuja. Katika Biblia, anatuonyesha mambo yenye tunapaswa kufanya ili tukuwe na furaha. Ndiyo sababu ni muzuri tusome Biblia kila siku na kufuata muongozo wenye inatoa. (Zaburi 1:1-3; soma Matendo 17:11.) Pia, Yehova anatupatia ‘chakula kwa wakati unaofaa’ kupitia ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara.’ (Mathayo 24:45) Kama vile tu watu wa Mungu wa wakati wa zamani, tunapaswa kusoma kwa ukawaida juu ya ahadi za Mungu na kufikiri sana juu ya ahadi hizo. Kufanya hivyo kutatusaidia tuendelee kuwa washikaminifu kwa Mungu na kungojea kwa hamu wakati Ufalme wake utatawala dunia yote.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine