-
Sisi Wote Tuko na Lazima ya KitulizoMunara wa Mulinzi (Gazeti la Watu Wote)—2016 | No. 5
-
-
HABARI KUBWA | TUNAWEZA KUPATA KITULIZO WAPI?
Sisi Wote Tuko Na Lazima Ya Kitulizo
Unakumbuka namna ulianguka wakati ulikuwa mutoto? Pengine ulijiumiza kwenye mukono ao kujikwaruza kwenye goti. Unakumbuka namna mama yako alikufariji ao kukutuliza? Pengine alisafisha kidonda chako na kukifunga kwa kitambaa. Ulilia, lakini kupitia maneno yake yenye kutuliza na namna alikukumbatia ulijisikia muzuri zaidi. Wakati huo, ulipata kitulizo kabisa.
Lakini, maisha yanakuwa nguvu zaidi wakati tunaendelea kukomaa. Magumu yanakuwa makubwa zaidi, na inakuwa nguvu zaidi kupata kitulizo. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, magumu yenye watu wakubwa wanapata, mara nyingi hayaishe kupitia kukumbatiwa ao kwa kufungwa kitambaa. Tuzungumuzie mifano fulani.
Umekwisha kupata huzuni kwa sababu ya kupoteza kazi yako? Julian anasema kwamba wakati alifukuzwa kwenye kazi, jambo hilo lilimuhangaisha sana. Alijiuliza: ‘Namna gani nitatunza familia yangu? Kisha kutumika kwa miaka mingi kwa nguvu yangu yote, sababu gani kompanyi hii inawaza kwamba sina faida?’
Pengine unahangaika sana kwa sababu ndoa yako imevunjika. Raquel anasema hivi: “Wakati bwana yangu aliniacha bila kuwazia, kumepita miezi 18, nilijisikia mubaya sana. Ilikuwa kama moyo wangu umevunjika vipande viwili. Niliumia kimwili na nilijisikia mubaya katika moyo. Jambo hilo liliniogopesha sana.”
Pengine uko na matatizo makubwa ya afya; na hauone kabisa alama yenye kuonyesha kwamba kutakuwa mabadiliko. Inawezakana wakati fulani unajisikia kama vile Ayubu. Alisema hivi kwa huzuni: “Ninachukia uzima wangu, sitaki kuishi siku zote.” (Ayubu 7:16, La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo) Pengine unajisikia kama vile Luis, mwanaume wa miaka 80 hivi. Alisema hivi: “Wakati fulani, ninajisikia tu kama ninangojea kifo.”
Ao pengine kifo cha mutu mwenye unapenda kinakufanya ukuwe na lazima ya kupata kitulizo. Robert anasema hivi: “Wakati mutoto wangu alikufa katika aksidenti ya avion, kwanza sikuamini jambo hilo. Kisha nilisikia maumivu, maumivu yenye Biblia inalinganisha na upanga murefu wenye kupita ndani ya mutu.”—Luka 2:35.
Robert, Luis, Raquel, na Julian walipata kitulizo hata kama walikuwa katika hali hizo zenye kuleta huzuni. Walipata Mutu wa kuwatolea kitulizo hicho chenye walikuwa nacho lazima. Mutu huyo ni Mungu Mweza-Yote. Namna gani Mungu anatolea watu kitulizo? Atakupatia pia kitulizo chenye uko nacho lazima?
-
-
Namna Mungu Anatolea Watu KitulizoMunara wa Mulinzi (Gazeti la Watu Wote)—2016 | No. 5
-
-
HABARI KUBWA | TUNAWEZA KUPATA KITULIZO WAPI?
Namna Mungu Anatolea Watu Kitulizo
Mutume Paulo anasema kwamba Yehovaa ni ‘Mungu wa faraja [ao, kitulizo] yote ambaye anatufariji katika ziki yetu yote.’ (2 Wakorintho 1:3, 4) Kwa hiyo, Biblia inatuhakikishia kwamba hakuna mutu mwenye Yehova anaweza kushindwa kusaidia na kwamba hakuna musiba wenye unaweza kufanya Baba yetu wa mbinguni ashindwe kutoa kitulizo.
Lakini, tunapaswa kufanya jambo fulani kama tunapenda Mungu atutolee kitulizo. Namna gani munganga anaweza kutusaidia kama hatukupatana kuonana naye? Nabii Amosi aliuliza hivi: “Je, watu wawili watatembea pamoja isipokuwa wawe wamekutana kwa mapatano?” (Amosi 3:3) Kwa hiyo, Maandiko yanatutia moyo hivi: ‘Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.’—Yakobo 4:8.
Namna gani tunaweza kuwa hakika kwamba Mungu atatukaribia? Kwanza, kwa sababu anatuambia kila mara kwamba anapenda kutusaidia. (Ona kisanduku chenye kuwa katika habari hii.) Pili, kwa sababu tuko na ushuhuda wenye kusadikisha wa watu wa kweli kabisa wenye Mungu alitolea kitulizo. Kati ya watu hao, kuna watu wa zamani na wa wakati wetu.
Mufalme Daudi alipata magumu mengi kama vile watu wengi wenye kutafuta musaada kutoka kwa Yehova leo. Wakati fulani alimuomba Yehova hivi: “Uisikie sauti ya kusihi kwangu ninapokulilia unisaidie.” Yehova alimusaidia? Ndiyo. Daudi alisema tena hivi: “Nami nimesaidiwa, hivi kwamba moyo wangu unashangilia.”—Zaburi 28:2, 7.
DARAKA LA YESU KATIKA KUTOLEA KITULIZO WATU WOTE WENYE KUOMBOLEZA
Mungu alikamata mipango ili Yesu akuwe na daraka kubwa katika kutolea watu kitulizo. Kati ya mambo yenye Mungu alimuomba afanye, Yesu alipaswa “kufunga majeraha [ao, vidonda] ya waliovunjika moyo” na “kuwafariji wote wanaoomboleza.” (Isaya 61:1, 2) Kama vile Maandiko yalionyesha zamani, Yesu alihangaikia sana watu wenye walikuwa ‘wanataabika [ao, kusumbuka] na kulemewa na mizigo.’—Mathayo 11:28-30.
Yesu alitolea watu kitulizo kwa kuwatolea mashauri yenye hekima, kwa kuwatendea kwa wema, na hata, katika hali fulani, kwa kuponyesha magonjwa yao. Siku moja mutu mwenye ukoma alimuomba Yesu hivi: “Ikiwa tu unataka, unaweza kunitakasa.” Kwa sababu ya kumusikilia huruma, Yesu alimujibu hivi: “Ninataka. Takasika.” (Marko 1:40, 41) Na mutu mwenye ukoma akapona.
Leo, Mwana wa Mungu haiko hapa duniani ili kutolea watu kitulizo moja kwa moja. Lakini Yehova, Baba yake, “Mungu wa faraja yote,” anaendelea kusaidia wote wenye kuwa na lazima ya kitulizo. (2 Wakorintho 1:3) Tuone njia ine kubwa zenye Mungu anatumia ili kutolea watu kitulizo.
Biblia. ‘Mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi, ili kupitia uvumilivu wetu na kupitia faraja kutokana na Maandiko tukuwe na tumaini.’—Waroma 15:4.
Roho Takatifu ya Mungu. Muda kidogo tu kisha Yesu kufa, kutaniko lote la Kikristo liliingia katika kipindi cha amani. Sababu gani? Kwa sababu ‘lilitembea katika kumuogopa Yehova na katika faraja ya roho takatifu.’ (Matendo 9:31) Roho takatifu, ni kusema, nguvu yenye Mungu anatumia ili kutenda, ni yenye nguvu sana. Mungu anaweza kuitumia ili kumutolea kitulizo mutu yeyote katika hali yoyote.
Sala. Biblia inatushauria hivi: ‘Musihangaike juu ya kitu chochote.’ Kuliko kuhangaika, inasema, ‘maombi yenu na yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili.’—Wafilipi 4:6, 7.
Wakristo Wenzetu wanaweza kuwa marafiki wa kweli wenye tunaweza kutegemea ili kupata kitulizo wakati wa magumu. Mutume Paulo alisema kwamba Wakristo wenzake ni ‘musaada wenye kutia nguvu’ wakati wa ‘uhitaji na ziki.’—Wakolosai 4:11; 1 Wathesalonike 3:7.
Lakini unaweza kujiuliza namna gani mambo hayo yote yanawezekana kabisa. Tuzungumuzie sasa watu wenye walikutana na mambo yenye kuwa katika habari ya kwanza. Kama watu hao, utaona kwamba Mungu anatimiza ahadi yake hii yenye kutia moyo: ‘Kama vile mutu ambaye mama yake mwenyewe anaendelea kumufariji, ndivyo mimi nitakavyoendelea kuwafariji ninyi.’—Isaya 66:13.
a Biblia inaonyesha kama jina la Mungu ni Yehova.
-
-
Kupata Kitulizo Wakati wa MagumuMunara wa Mulinzi (Gazeti la Watu Wote)—2016 | No. 5
-
-
HABARI KUBWA | TUNAWEZA KUPATA KITULIZO WAPI?
Kupata Kitulizo Wakati Wa Magumu
Magumu yanatokea katika njia nyingi. Hatuwezi kuzungumuzia kila namna ya magumu katika habari hii, lakini acha tuzungumuzie mifano ine yenye tumekwisha kutaja. Tuone namna watu wenye walipambana na magumu tofauti walipata kitulizo cha kweli kutoka kwa Mungu.
WAKATI MUTU HANA KAZI
“Nilijifunza kukubali kazi yoyote, na tuliepuka kununua vitu vyenye hatukuwa navyo lazima.”—Jonathan
Setha anakumbuka mambo yenye yalimufikia. Anasema hivi: “Mimi na bibi yangu tulipoteza kazi kwa wakati mumoja. Kwa miaka mbili tulilazimika kuishi kupitia musaada wenye familia ilitutolea na kupitia kazi ndogo za kutafutisha. Kwa hiyo, bibi yangu Priscilla, alishuka moyo, na nikajiona kuwa mutu wa bure.
“Ni nini ilitusaidia kuvumilia? Priscilla aliendelea kukumbuka maneno ya Yesu yenye kuwa katika andiko la Mathayo 6:34. Yesu alisema kwamba hatupaswe kuhangaika juu ya kesho, kwa sababu kila siku iko na mahangaiko yake. Na sala za bibi yangu zenye kutoka moyoni zilimupatia nguvu ya kuendelea kuvumilia. Kwa upande wangu, Zaburi 55:22 ilinituliza. Kama muandikaji wa zaburi hiyo, nilitupa muzigo wangu kwa Yehova, na nikajisikia kwamba amenitegemeza kabisa. Hata kama leo niko na kazi, tunaendelea kufanya maisha yetu yakuwe mepesi kulingana na shauri la Yesu lenye kuwa katika Mathayo 6:20-22. Zaidi ya yote, tumemukaribia Mungu zaidi, na mimi na bibi yangu tumekaribiana zaidi.”
Jonathan anasema hivi: “Niliogopa juu ya wakati unaokuja kwa sababu biashara yetu ndogo ya familia ilianguka. Miaka 20 ya kazi ngumu iligeuka kuwa bure kwa sababu ya matatizo ya feza (crise économique). Mimi na bibi yangu tulianza kubishana kwa sababu ya feza. Hatungeweza kununua vitu kupitia kadi yetu ya kujikopesha kwa sababu tuliogopa kwamba wataikataa.
“Lakini Neno la Mungu na roho yake takatifu vilinisaidia kukamata maamuzi ya muzuri. Nilijifunza kukubali kazi yoyote, na tuliepuka kununua vitu vyenye hatukuwa navyo lazima. Kwa sababu tuko Mashahidi wa Yehova, tulisaidiwa pia na waamini wenzetu. Walifanya tujisikie kuwa wa maana na walitusaidia wakati maisha yetu yalikuwa magumu sana.”
WAKATI NDOA INAVUNJIKA
Raquel anakumbuka mambo yenye yalimufikia. Anasema hivi: “Wakati bwana yangu aliniacha bila kutazamia, niliumia moyoni na kukasirika. Na nilijisikia mubaya sana. Lakini, nilimukaribia Mungu, na akanituliza. Amani ya Mungu ililinda moyo wangu wakati nilisali kwake kila siku. Nilijisikia kama ametengeneza moyo wangu wenye kuvunjika.
“Na kupitia Neno lake, Biblia, nilifikia kushinda hali ya kukasirika na kuweka kinyongo. Niliamini kabisa maneno ya mutume Paulo yenye kupatikana katika andiko la Waroma 12:21. Andiko hilo linasema hivi: ‘Usiache ushindwe na uovu, bali endelea kushinda uovu kwa wema.’
“Kuna wakati wenye tunapaswa ‘kuacha kutafuta kilichopotea.’ . . . Niko sasa na mipango mipya ya kutimiza katika maisha.”—Raquel
“Rafiki mumoja muzuri alinisaidia nielewe kwamba ni jambo la lazima kuendelea na maisha. Alinionyesha andiko la Mhubiri 3:6 na akaniambia kwa upole kwamba kuna wakati wenye tunapaswa ‘kuacha kutafuta kilichopotea.’ Sikufurahia shauri hilo, lakini lilikuwa shauri lenye nilikuwa nalo lazima. Niko sasa na mipango mipya ya kutimiza katika maisha.”
Elizabeth anasema hivi: “Wakati ndoa yako inavunjika, uko na lazima ya watu wa kukutegemeza. Nilipata rafiki wa sana mwenye alinitegemeza kila mara. Alilia pamoja na mimi, alinituliza, na alifanya nijisikie kuwa mwenye kupendwa kuliko kujisikia kuwa mwenye kutupiliwa. Niko hakika kwamba Yehova alitumia dada huyo ili kuponyesha vidonda vyangu vya moyo.”
WAKATI WA MAGONJWA AO UZEE
“Kisha kusali, ninasikia kwamba roho yake inanipatia nguvu.”—Luis
Luis, mwenye tulitaja katika habari ya kwanza alipata ugonjwa hatari wa moyo, na mara mbili alikaribia kufa. Kwa sasa iko na lazima ya kutumia kifaa cha kumupatia oksijeni kwa saa 16 kila siku. Anasema hivi: “Ninasali kwa Yehova kila mara. Na kisha kusali, ninasikia kwamba roho yake inanipatia nguvu. Sala inanipatia nguvu ya kusonga mbele kwa sababu niko na imani katika Mungu na kwa sababu ninajua kwamba ananihangaikia.”
Mwanamuke mumoja mwenye kuitwa Petra iko na miaka zaidi ya 80. Anasema hivi: “Ninapenda kufanya mambo mengi, lakini sina uwezo. Ninajisikia mubaya sana kuona namna nguvu zangu zinaendelea kupunguka. Ninajisikia mwenye kuchoka sana na kila siku ninapaswa kutumia dawa. Mara nyingi ninafikiria namna Yesu alimuomba Baba yake ili jambo fulani ngumu lipitilie mbali kama inawezekana. Lakini Yehova alimupatia Yesu nguvu, na ananipatia pia nguvu. Sala ni dawa yangu ya kila siku. Ninajisikia muzuri zaidi kisha kusali kwa Mungu.”—Mathayo 26:39.
Julian, mwenye amekuwa anapambana na ugonjwa wa mishipa ya ufahamu kwa miaka karibu 30, anajisikia hivyo pia. Mwanaume huyo anasema hivi: “Nimeacha kutumia kiti cha cheo katika kazi na kuanza kutumia kiti cha vilema. Lakini maisha yangu yako na maana kwa sababu nimejitolea ili kutumikia wengine. Kutoa kunaweza kupunguza mateso, na Yehova anaendelea kutimiza ahadi yake ya kutupatia nguvu wakati wa magumu. Kama vile mutume Paulo, ninaweza kusema kabisa kwamba: ‘Kwa mambo yote nina nguvu kupitia yeye anayenipatia nguvu.’”—Wafilipi 4:13.
WAKATI UNAFIWA
Antonio anakumbuka mambo yenye yalimupata. Anasema hivi: “Wakati baba yangu alikufa katika aksidenti ya barabara, sikuamini palepale. Jambo hilo lilionekana kuwa la bila haki, kwa sababu baba yangu alikuwa anajitembeza kwa miguu bila kosa lolote. Lakini sikuwa na jambo lenye ningeweza kufanya. Alipoteza ufahamu kwa siku tano mbele akufe. Nilijizuia kulia mbele ya mama yangu, lakini wakati nilikuwa peke yangu nilianza kulia sana. Niliendelea kujiuliza, ‘Sababu gani? Sababu gani jambo hilo lilitokea?’
“Katika siku hizo zenye huzuni kubwa, niliendelea kuomba Yehova anisaidie kujizuia na anipatie amani. Na hatua kwa hatua nilijisikia muzuri zaidi. Nilikumbuka kwamba Biblia inasema kuwa ‘tukio lenye halitazimiwe’ linaweza kumupata mutu yeyote. Kwa sababu Mungu hawezi kusema uongo, niko hakika kwamba nitaona tena baba yangu wakati wa ufufuo.”—Mhubiri 9:11; Yohana 11:25; Tito 1:2.
“Hata kama aksidenti ya avion iliua mutoto wetu, tunaendelea kukumbuka mambo mengi ya kufurahisha yenye tulipitisha pamoja naye.”—Robert
Robert, mwenye tulitaja katika habari ya kwanza iko na mawazo kama hayo. Anasema hivi: “Mimi pamoja na bibi yangu, tulipata amani ya akili yenye kutajwa katika andiko la Wafilipi 4:6, 7. Tulipata amani hiyo kupitia sala zetu kwa Yehova. Amani hiyo ya ndani ilitusaidia kuzungumuza na watangazaji wa habari juu ya tumaini letu la ufufuo. Hata kama aksidenti ya avion iliua mutoto wetu, tunaendelea kukumbuka mambo mengi ya kufurahisha yenye tulipitisha pamoja naye. Tunajikaza kukaza akili yetu juu ya mambo hayo.
“Wakati Mashahidi wenzetu walituambia kwamba walituona kwenye televizyo namna tulikuwa tunafasiria kwa utulivu mambo yenye tunaamini, tuliwaambia hilo liliwezekana kupitia tu sala nyingi zenye walitoa kwa ajili yetu. Ninaamini kabisa kwamba Yehova alitutegemeza kupitia ujumbe wao mbalimbali wenye kutuliza.”
Kama vile mifano yenye tunatoka kuona inaonyesha, Mungu anatolea watu kitulizo wakati wanapata magumu. Sasa wewe? Hata kama uko na magumu gani katika maisha, unaweza kupata kitulizo ili kupambana na magumu hayo.b Kwa hiyo, umutegemee Yehova ili akusaidie. Yeye ni “Mungu wa faraja yote.”—2 Wakorintho 1:3.
-