Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 6/01 uku. 7
  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kazi ya Ujenzi Ambayo Inamuletea Yehova Heshima
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Hii Ndiyo Nafasi Yetu ya Kufanyia Ibada
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 6/01 uku. 7

Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Sisi ni wenye kupendelewa kama nini! Tukiwa Mashahidi wa Yehova, sisi tuna pendeleo si la kujua tu Yehova, yule Mungu pekee wa kweli na aliye hai, Muumba wa ulimwengu, lakini pia la kuchukua jina lake na kumtumikia yeye. Je, kunaweza kuwa baraka kubwa zaidi kuliko hiyo?—Isa. 43:12; Ebr. 8:11.

Tunalo tumaini la wokovu na utume wa kuhuburi habari njema ya Ufalme kusudi wengine pia waweze kumwabudu Yehova na kushiriki tumaini letu. (Mt. 24:14; Rom. 10:13, 14; 1 Thes. 5:8) Pia, tuna furaha ya kuwa undugu wa kimataifa unaofanyizwa na waabudu wanaopendana na kusaidiana kwa njia yenye kutenda. Mambo hayo yote ni yenye kuthawabisha kama nini!

Kwa njia yenye kufaa, Biblia inatualika: “Tumikieni [Yehova] kwa furaha; . . . Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru, na katika viwanja vyake kwa sifa: mumushukuru, na kubariki jina lake. Kwa kuwa [Yehova] ni mwema; rehema yake ni ya milele; na uaminifu wake vizazi na vizazi.” (Zab. 100:2-5) Kutumikia Yehova kwa furaha kunahusiana moja kwa moja na kuwa na uhusiano wa kibinafsi na wenye nguvu pamoja naye. Yeye anafanya uhusiano kama huo uwezekane, nasi tuna pendeleo la kuukomaza. Wakati tunapokuwa na aina hiyo ya uhusiano, tunajua kwamba Yehova sikuzote yuko tayari kutusaidia na kututia nguvu katika nyakati za uhitaji. Tuna hakika kwamba atatoa nguvu na mwongozo wa kiroho vinavyohitajiwa ili kupambana na matatizo ya maisha katika siku za mwisho za mfumo huu wa mambo. Ijapokuwa mikazo tunayopambana nayo, sisi ni wenye furaha katika huduma yetu, nasi tunamshukuru Yehova kila siku kwa kuwa, kama vile Neno lake linavyotukumbusha, ‘yeye anatujali sisi.’—1 Pet. 5:7.

Mnamo mwaka uliopita, Yehova kwa kweli alitubariki sana. Kwenye Mkusanyiko wa Wilaya “Watendaji wa Neno la Mungu,” tulisisimuka kuwa pamoja na maelfu ya wengine walio na imani ileile yenye thamani, tukiimba na kufurahia karamu pamoja kwenye meza ya Yehova. Kwenye Mafunzo yetu ya Kitabu, tumetia imani yetu nguvu kwa kujifunza pamoja kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! Na zaidi ya yote, lilikuwa jambo lenye kusisimua kama nini kwetu kupokea Buku I la kile kichapo kipya Unabii wa Isaya—Nuru kwa Wanadamu Wote! ‘Kikombe chetu kinafurika.’—Zab. 23:5.

Ni furaha kama nini kujua kwamba sisi, tukiwa mamilioni ya ndugu na dada wa kiroho, ni wenye umoja katika kumtumikia Yehova! Ni jambo lenye kutia moyo kama nini kusoma kuhusu vilele vipya vilivyofikiwa kuhusiana na huduma ya shambani! Tunafurahi kwa sababu ya yale mamilioni mengi yaliyohudhuria Ukumbusho wa kifo cha Bwana wetu—na walifanya hivyo ingawa hali za ulimwengu. Kadiri tunavyoona shamba la ulimwenguni pote, ni wazi kwamba “kwa kweli, mavuno ni mengi.” (Luka 10:2) Mwaka uliopita, wastani wa wanafunzi wa Biblia 5,555 kila juma walifanya maendeleo kufikia hatua ya kuonyesha wakfu wao kupitia ubatizo wa maji. Ingawa mavuno ni mengi zaidi katika sehemu fulani za dunia kuliko zingine, sisi sote tunafurahia yale anayofanya Yehova. Tunaona uhakikisho ulio wazi wa baraka yake juu ya jitihada zenye umoja za watumishi wake.

Ujenzi wa Majumba ya Ufalme mapya umekuwa sababu ya ziada ya shangilio kubwa! Tunafurahi sana kuona utegemezo wenye kutolewa kwa moyo wote kutoka kwa ndugu na dada zetu katika nchi ambazo bado zinafanya maendeleo. Mamia ya Majumba ya Ufalme yamekwisha kujengwa kwa msaada wa Vikundi kwa Ajili ya Ujenzi wa Majumba ya Ufalme, vikundi ambavyo vimepewa mazoezi yenye kuhitajiwa. Ndugu hao wanahama kutoka kutaniko moja mpaka kutaniko lingine katika nchi yao wenyewe ili kuongoza mipango ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme. Kwa kuwa maelfu ya Majumba ya Ufalme bado yanahitaji kujengwa, mwito unatolewa kwa wajitoleaji zaidi ili kusaidia katika kazi hii ya maana sana katika nchi ambazo bado zinafanya maendeleo. Ikiwa unaishi katika nchi kama hiyo, je, unaweza kujitoa? Ndugu na dada zetu wapendwa huthamini sana kama nini kuwa na Jumba la Ufalme lao wenyewe ambamo wanaweza kukutana kwa ajili ya ibada! Nao ni wenye shukrani kama nini kwa undugu wa ulimwenguni pote kwa ajili ya msaada wa kifedha wanaotoa ili kufanya jambo hilo liwezekane!

Habari kuhusu ushindi mbalimbali wa kisheria hutusisimua. Hata hivyo, mahali pengi pia kuna watu wenye uvutano ambao wangetaka kukandamiza ibada ya Yehova. Kadiri tunavyoshughulika na hali hizo, tuna hakika kwamba, kuhusiana na kusaidia, jambo la maana kwa Yehova si hesabu ya wapinzani au jinsi watumishi wake wanavyoonekana kuwa wawezao kupatwa na madhara. (2 Nyak. 14:11) Tunawapongeza kwa shauku nyinyi nyote, ndugu na dada, mnaoendelea kusimama imara kwa ajili ya ibada ya kweli.

Endeleeni kutia imani yenu nguvu na kumtegemea sana Yehova kwa ajili ya mwongozo kadiri mnavyotimiza kwa furaha madaraka yenu ya Kikristo. (Mez. 3:5, 6) Hakuna sababu yoyote ya kuvunjika moyo, hata mambo ambayo adui anaweza kuruhusiwa kufanya yawe nini. Kumbukeni kitia-moyo kilichotolewa na Elisha kwa mtumishi wake mwenye wasiwasi: “Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.” (2 Fal. 6:15-17) Leo, jeshi la kimbingu la Yehova liko tayari kulinda faida za ibada safi, kama ilivyokuwa katika siku ya Elisha. Tunatarajia wakati ujao tukiwa na tumaini. Yehova anaongoza mambo. Mataifa hayawezi kupigana naye kwa mafanikio. Ametawaza Mwana wake, akimpa mamlaka kamili ya utawala. “Heri wote wanaomkimbilia.”—Zab. 2:1-6, 12.

Tafadhali kumbukeni kwamba nyinyi nyote, ndugu na dada wapendwa, mko katika mawazo yetu yenye shauku zaidi. Sala yetu ya bidii ni kwamba kila mmoja wenu apate “kusimama [akiwa] kamili na kwa usadikisho imara katika mapenzi yote ya Mungu.”—Kol. 4:12.

Ndugu zenu,

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine