-
Abrahamu na Sara Walimutii MunguMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 8
Abrahamu na Sara Walimutii Mungu
Muji wa Uru ulikuwa karibu na muji wa Babeli. Watu wa Uru waliabudu miungu mingi kuliko kumuabudu Yehova. Lakini kulikuwa mwanaume mumoja mwenye aliishi mu muji wa Uru, mwenye alimuabudu Yehova tu. Aliitwa Abrahamu.
Yehova alimuambia Abrahamu hivi: ‘Utoke mu inchi yako na uache watu wa jamaa yako, uende mu inchi yenye nitakuonyesha.’ Kisha Mungu alimupatia hii ahadi: ‘Nitakufanya ukuwe taifa kubwa, nitafanyia watu mambo ya muzuri mu dunia yote kwa sababu yako.’
Abrahamu hakujua kwenye Yehova alimuambia aende, lakini alimutumainia. Kwa hiyo Abrahamu, bibi yake Sara, baba yake Tera, na Loti, mutoto wa kaka yake, walitii, wakafunga mizigo na kuanza safari ya murefu.
Abrahamu alikuwa na miaka 75, wakati yeye na familia yake walifika mu inchi yenye Yehova alipenda kuwaonyesha. Ile inchi iliitwa Kanaani. Kule, Mungu alisema na Abrahamu na akamuambia hivi: ‘Nitapatia watoto wako hii inchi.’ Lakini Abrahamu na Sara walikuwa wazee na hawakukuwa na watoto. Basi, Yehova angetimiza ile maneno namna gani?
“Kwa imani, Abrahamu . . . alitii kwa kutoka na kuenda mahali kwenye angepokea kuwa uriti; alitoka, hata kama hakujua mahali alikuwa anaenda.”—Waebrania 11:8
-
-
Wanapata Sasa Mutoto!Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 9
Wanapata Sasa Mutoto!
Abrahamu na Sara walikuwa wamefanya miaka mingi sana tangu waoane. Waliacha nyumba yao ya muzuri kule Uru na walianza kuishi mu mahema. Lakini Sara hakukataa sababu alimutegemea Yehova.
Sara alipenda sana kupata mutoto. Aliambia Abrahamu: ‘Kama mutumishi wangu Hagari anazaa mutoto, ule mutoto atakuwa sawa mutoto wangu.’ Kisha wakati fulani, Hagari alizaa mutoto mwanaume; aliitwa Ishmaeli.
Kisha miaka mingi kupita, wakati Abrahamu alikuwa na miaka 99 na Sara miaka 89, wageni watatu waliwatembelea. Abrahamu aliwakaribisha ili wapumuzike chini ya muti na wakule chakula. Unajua wale wageni walikuwa nani? Walikuwa malaika! Waliambia Abrahamu: ‘Mwaka wenye kuja, wakati kama huu, wewe na bibi yako mutapata mutoto.’ Sara alikuwa mu hema yake na alikuwa anasikiliza. Alicheka mu moyo na kuwaza: ‘Ninaweza kweli kuzaa mutoto, hata kama niko muzee?’
Mwaka wenye ulifuata, Sara alizaa mutoto mwanaume, sawa vile malaika wa Yehova alimuambiaka. Abrahamu alipatia ule mutoto jina Isaka. Isaka maana yake “Kucheka.”
Wakati Isaka alikuwa na miaka karibu tano, Sara aliona Ishmaeli iko anamucheka Isaka. Kwa sababu alipenda kulinda mutoto wake, aliambia Abrahamu afukuze Hagari na Ishmaeli. Abrahamu alikataa kwanza. Lakini Yehova aliambia Abrahamu: ‘Usikilize Sara. Nitamulinda Ishmaeli. Lakini ni kupitia Isaka njo nitatimiza ahadi zangu.’
“Kwa imani Sara pia alipokea nguvu za kupata uzao, . . . kwa kuwa alimuona Ule mwenye alikuwa ameahidi kuwa ni muaminifu.”—Waebrania 11:11
-