-
Mukumbuke Bibi ya LotiMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 10
Mukumbuke Bibi ya Loti
Loti aliishi na Abrahamu, baba yake mudogo, mu inchi ya Kanaani. Kisha, Abrahamu na Loti wakakuwa na wanyama mingi. Lakini fasi ya kukulishia wanyama ikakuwa kidogo. Abrahamu aliambia Loti: ‘Hatuwezi tena kuishi pamoja hapa. Unaweza kuchagua kwenye unapenda kuenda na mimi nitaenda ngambo ingine.’ Abrahamu hakujipendelea, hauone vile?
Loti aliona fasi ya muzuri sana karibu na muji wenye kuitwa Sodoma. Kulikuwa maji mingi na majani ya mubichi. Basi akachagua ile fasi na akahamia kule na familia yake.
Watu wa Sodoma na Gomora walikuwa wabaya sana; Gomora ilikuwa pembeni ya Sodoma. Kusema kweli, walikuwa wabaya sana mupaka Yehova akaamua kuharibu ile miji. Lakini Mungu alipenda kuokoa Loti na familia yake. Alituma malaika wawili wawaambie: ‘Mufanye haraka! Mutoke katika muji huu! Yehova anataka kuuharibu!’
Loti hakutoka palepale. Aliendelea kukawia. Kwa hiyo malaika walikamata mukono wa Loti, wa bibi yake, na watoto wake wawili wanamuke na kuwapeleka inje ya muji, kisha wakawaambia: ‘Mukimbie ili musikufe! Musiangalie nyuma, mukiangalia nyuma mutakufa!’
Wakati walifika mu muji wa Soari, Yehova alifanya mvua ya moto na kiberiti inyeshe mu miji ya Sodoma na Gomora. Ile miji mbili iliharibiwa kabisa. Bibi ya Loti hakumutii Yehova, aliangalia nyuma na akakuwa nguzo ya chumvi! Lakini Loti na watoto wake wanamuke waliokoka kwa sababu walimutii Yehova. Walijisikia mubaya sana kwa sababu bibi ya Loti hakumutii Yehova. Lakini, walifurahi kwa sababu walisikiliza Yehova.
“Mukumbuke bibi ya Loti.”—Luka 17:32
-
-
Imani Yake InajaribiwaMambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
-
-
SOMO LA 11
Imani Yake Inajaribiwa
Abrahamu alifundisha mutoto wake Isaka kumupenda Yehova na kutumainia ahadi zake. Lakini, wakati Isaka alikuwa na miaka 25 hivi, Yehova aliambia Abrahamu afanye jambo fulani lenye lilikuwa nguvu sana. Alimuambia afanye nini?
Mungu aliambia Abrahamu: ‘Tafazali, ukamate mutoto wako wa pekee na umutoe zabihu kwenye mulima, katika inchi ya Moria.’ Abrahamu hakujua ni juu ya nini Yehova alimuambia afanye vile. Lakini, alimutii Yehova.
Asubui sana ya siku ya kufuata, Abrahamu, watumishi wake wawili na Isaka walianza safari ya kuenda Moria. Kisha safari ya siku tatu, waliona milima kwa mbali. Abrahamu aliwaambia watumishi wake wangojee, wakati yeye na Isaka wanaenda kutoa zabihu. Abrahamu aliambia Isaka abebe kuni, na Abrahamu akakamata kisu. Isaka aliuliza baba yake: ‘Munyama mwenye tutatoa zabihu iko wapi?’ Abrahamu akamujibu: ‘Mutoto wangu, Yehova atamuleta.’
Wakati walifika ku mulima walijenga mazabahu. Kisha, Abrahamu akafunga mikono na miguu ya Isaka na kumuweka juu ya mazabahu.
Abrahamu akakamata kisu ili amuue. Palepale, sauti ya malaika wa Yehova ikatoka mbinguni na kusema: ‘Abrahamu! Usiumize mutoto wako! Sasa ninajua kama unaamini kabisa Mungu kwa sababu ulikuwa tayari kumutoa mutoto wako kuwa zabihu.’ Kisha, Abrahamu akaona kondoo-dume mwenye pembe zake zilikuwa zimebana mu miti midogo-midogo. Palepale akamufungua Isaka na kutoa ule kondoo-dume akuwe zabihu pa nafasi ya Isaka.
Kuanzia ile siku, Yehova aliita Abrahamu kuwa rafiki yake. Unajua ni juu ya nini? Ni juu Abrahamu alifanya mambo yote yenye Yehova alimuomba afanye, hata kama wakati fulani hakuelewa juu ya nini Mungu alimuambia afanye vile.
Yehova alirudilia ile ahadi yenye alikuwa ameambia Abrahamu: ‘Nitakubariki na nitafanya uzao wako ao watoto wako wakuwe mingi.’ Ni kusema, Yehova angebariki watu wote wazuri kupitia familia ya Abrahamu.
“Mungu alipenda ulimwengu sana na hivyo akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee, ili kila mutu mwenye anamuamini asiharibiwe lakini apate uzima wa milele.”—Yohana 3:16
-