Somo 13
Uganga Na Uchawi Ni Mambo Mabaya
Shetani anataka wewe ufanye mambo ya kiganga. Watu wengi hutoa dhabihu kwa babu zao wa kale waliokufa au kwa roho ili ziwalinde wasipate madhara. Wao hufanya hivyo kwa sababu wanaogopa nguvu za ulimwengu wa roho. Watu hao huvaa pete au mikufu ya mkononi ya kiganga. Wao hunywa au kusugua mwilini mwao “dawa” zinazodhaniwa kuwa zina nguvu za kiganga. Watu fulani huficha katika nyumba zao au chini ya udongo vyombo vinavyoaminiwa kuwa na nguvu za kulinda. Wengine nao hutumia “dawa” za kiganga kwa sababu wanaamini kuwa zitawaletea mafanikio katika biashara, mitihani shuleni, au uchumba.
Ukitaka ulinzi bora zaidi dhidi ya Shetani, unapaswa kuwa rafiki ya Yehova. Yehova Mungu na malaika zake wana nguvu nyingi zaidi kuliko Shetani na roho wake waovu. (Yakobo 2:19; Ufunuo 12:9) Yehova ana hamu ya kutumia nguvu zake kuwasaidia marafiki wake—wale wenye uaminifu-mshikamanifu kabisa kwake.—2 Mambo ya Nyakati 16:9.
Neno la Mungu linasema hivi: “Msifanye kuloga.” Yehova hushutumu uganga na uchawi kwa sababu mazoea hayo yanaweza kumfanya mtu atawaliwe moja kwa moja na Shetani Ibilisi.—Mambo ya Walawi 19:26.