Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • gf somo 15 uku. 24-25
  • Marafiki Wa Mungu Hufanya Mambo Mema

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Marafiki Wa Mungu Hufanya Mambo Mema
  • Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Familia Yako Inaweza Kuwa na Furaha
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Maisha ya Familia Yanayomupendeza Mungu
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Juu ya Nini Tuheshimie Mamlaka?
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Unaweza Kufanya Nini ili Ukuwe na Maisha ya Familia Yenye Furaha?
    Umusikilize Mungu ili Uishi Milele
Ona Habari Zaidi
Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
gf somo 15 uku. 24-25

Somo 15

Marafiki Wa Mungu Hufanya Mambo Mema

Ukiwa na rafiki unayempenda na kumheshimu, wewe hujaribu kuwa kama yeye. “BWANA ni mwema na mwenye haki,” Biblia yasema. (Zaburi 25:⁠8) Ili tuwe marafiki wa Mungu, ni lazima tuwe watu wema na wenye haki. Biblia inasema hivi: “Iweni waigaji wa Mungu, mkiwa watoto wapendwa, na endeleeni kutembea katika upendo.” (Waefeso 5:​1, 2) Hapa pana njia kadhaa za kufanya hivyo:

Wasaidie wengine. “Acheni sisi tufanye lililo jema kuelekea wote.”​—⁠Wagalatia 6:⁠10.

Fanya kazi kwa bidii. “Mwibaji na asiibe tena, bali acheni afanye kazi ya bidii, akifanya kwa mikono yake kazi iliyo njema.”​—⁠Waefeso 4:⁠28.

Dumu ukiwa safi kimwili na kiadili. “Acheni tujisafishe wenyewe kila unajisi wa mwili na wa roho, tukikamilisha utakatifu katika hofu ya Mungu.”​—⁠2 Wakorintho 7:⁠1.

Watendee washiriki wa familia yako kwa upendo na heshima. “Acheni kila mtu . . . kati yenu ampende hivyo mke wake kama yeye mwenyewe; kwa upande mwingine, mke apaswa kuwa na staha yenye kina kirefu kwa mume wake. Watoto, iweni watiifu kwa wazazi wenu.”​—⁠Waefeso 5:33–6:⁠1.

Wapende wengine. “Acheni tuendelee kupendana, kwa sababu upendo ni wa kutoka kwa Mungu.”​—⁠1 Yohana 4:⁠7.

Tii sheria za nchi. “Acheni kila nafsi iwe katika ujitiisho kwa [serikali] . . . Walipeni wote haki zao, kwa yeye atakaye kodi, kodi.”​—⁠Waroma 13:​1, 7.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine