Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • gf somo 5 uku. 8-9
  • Marafiki Wa Mungu Wataishi Katika Paradiso

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Marafiki Wa Mungu Wataishi Katika Paradiso
  • Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Paradiso
    Amuka!—2013
  • “Tutaonana Katika Paradiso!”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Dunia Itakuwa Paradiso
    Roho za Wafu—Zinaweza Kukusaidia ao Kukutendea Mubaya? Zinakuwaka Kabisa?
  • Kusudi la Mungu Ni Nini Kuhusu Dunia?
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
Ona Habari Zaidi
Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
gf somo 5 uku. 8-9

Somo 5

Marafiki Wa Mungu Wataishi Katika Paradiso

Paradiso haitakuwa kama ulimwengu tunamoishi leo. Mungu hakutaka kamwe dunia ijae matatizo na huzuni, maumivu na kuteseka. Wakati ujao, Mungu ataifanya dunia iwe paradiso. Paradiso itakuwaje? Acheni tuone mambo ambayo Biblia inasema:

Watu wema. Paradiso itakuwa makao ya marafiki wa Mungu. Watatendeana mema. Wataishi kulingana na njia za Mungu za uadilifu.​—⁠Mithali 2:⁠21.

Chakula tele. Njaa haitakuwako katika Paradiso. Biblia inasema hivi: “Na uwepo wingi wa nafaka [au, chakula] katika ardhi juu ya milima.”​—⁠Zaburi 72:⁠16.

Nyumba nzuri na kazi yenye kufurahisha. Katika dunia iliyo Paradiso, kila familia itakuwa na makao yake binafsi. Kila mtu atafanya kazi inayoleta furaha ya kweli.​—⁠Isaya 65:​21-23.

Amani ulimwenguni kote. Watu hawatakuwa wakipigana wala kufa vitani. Neno la Mungu linasema hivi: “[Mungu] avikomesha vita.”​—⁠Zaburi 46:​8, 9.

Afya njema. Biblia inaahidi hivi: “Hapana mwenyeji [wa Paradiso] atakayesema, Mimi mgonjwa.” (Isaya 33:24) Pia, hakuna mtu atakayekuwa kilema wala kipofu wala kiziwi wala hakuna yeyote atakayeshindwa kuongea.​—⁠Isaya 35:​5, 6.

Mwisho wa maumivu, huzuni, na kifo. Neno la Mungu linasema hivi: “Kifo hakitakuwapo tena, wala ombolezo wala kupaaza kilio wala umivu halitakuwapo tena kamwe. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”​—⁠Ufunuo 21:⁠4.

Watu wabaya hawatakuwako. Yehova anaahidi hivi: “Waovu watatengwa na nchi, nao wafanyao hila watang’olewa.”​—⁠Mithali 2:⁠22.

Watu watapendana na kuheshimiana. Ukosefu wa haki, kuonewa, pupa, na chuki hazitakuwapo tena. Watu wataungana, nao wataishi kulingana na njia za Mungu za uadilifu.​—⁠Isaya 26:⁠9.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine