Kutubu
Juu ya nini wanadamu wote wanapaswa kutubu zambi zao na kumuomba Yehova musamaha?
Ona pia Mdo 26:20
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Lu 18:9-14—Yesu anatoa mufano juu ya kukazia kama tuko na lazima ya kuungama zambi zetu na kumuomba Mungu atusaidie
Ro 7:15-25—Hata kama Paulo ni mutume na ni mwanaume mwenye imani ya nguvu, anajisikia mubaya juu inaomba apiganishe tamaa ya kufanya zambi
Biblia inasema nini kuhusu namna Yehova anajisikiaka juu ya wale wenye kutubu?
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Lu 15:1-10—Yesu anatumia mifano juu ya kuonyesha kama Yehova na malaika wanakuwaka na furaha wakati mutu anatubu
Lu 19:1-10—Zakayo, mukubwa wa wakusanya-kodi, anatubu na anabadilisha tabia yake, kisha anasamehewa na anapata wokovu
Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunatubu kikweli?
Juu ya nini zaidi ya kutubu kikweli mutu anapaswa pia kupata ujuzi wenye hauna makosa?
Ro 12:2; Kol 3:9, 10; 2Ti 2:25
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
Mdo 17:29-31—Mutume Paulo anafasiria watu wa Atene kama kukosa ujuzi njo inafanyaka watu waabudu sanamu, na anawaambia watubu
1Ti 1:12-15—Mbele ya kupata ujuzi wa kweli kuhusu Yesu, mutume Paulo alifanyaka zambi mingi juu ya kukosa kujua
Juu ya nini kutubu ni jambo ya maana sana?
Juu ya nini tunapaswa kuwa hakika kama ikiwa tunatubu Yehova atatusamehe hata kama tunafanya zambi mara mingi?
Namna gani Yehova anatendeaka wale wenye wanaungama zambi zao na kubadilika?
Ona pia “Rehema”
Tunajua namna gani kama kutubu haiko tu kusema kama tunahuzunika ao tunajisikia mubaya juu ya makosa yenye tulifanya?
2Ny 7:14; Mez 28:13; Eze 18:30, 31; 33:14-16; Mt 3:8; Mdo 3:19; 26:20
Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:
2Ny 33:1-6, 10-16—Hata kama alijiendesha mubaya kwa wakati murefu, Mufalme Manase anatubu kwa kujinyenyekeza, kuendelea kusali, na kubadilisha tabia zake
Zb 32:1-6; 51:1-4, 17—Mufalme Daudi anaonyesha kama anatubu kwa kusikitika juu ya makosa yake, kwa kuungama, na kwa kusali
Wakati watu wenye walitukosea wanatubu, juu ya nini tunapaswa kuwasamehe?
Mt 6:14, 15; 18:21, 22; Lu 17:3, 4
Ona pia “Musamaha”