Watchtower ONLINE LIBRARY
Watchtower
ONLINE LIBRARY
Kĩmĩĩrũ
  • BIBLE
  • PUBLICATIONS
  • MEETINGS
  • w25 Machi tũr. 2-7
  • Menya Ũtĩĩria Kũbatithua

No video available for this selection.

Sorry, there was an error loading the video.

  • Menya Ũtĩĩria Kũbatithua
  • Mũkaria Ĩrĩa Ĩtũmagĩria Ũnene Bwa Jehova (Ngacĩti ya Kwiritana)—2025
  • Subheadings
  • Similar Material
  • ASAMARIA NĨBABATITHĨRUE
  • SAŨLŨ WA TARISO ARABATITHUA
  • KORINELIO ARABATITHUA
  • AKORINTHO BARABATITHUA
  • WĨTĨKIO BWAKU BWOMBA GWĨTAĨTITHIA IRĨMA
  • Ĩta na Mbere Kũthingata Jesũ Nyuma ya Kũbatithua
    Mũkaria Ĩrĩa Ĩtũmagĩria Ũnene Bwa Jehova (Ngacĩti ya Kwiritana)—2024
  • Rĩ, Nwithuranĩrĩte Kwirita Kĩrĩ Jehova?
    Mũkaria Ĩrĩa Ĩtũmagĩria Ũnene Bwa Jehova (Ngacĩti ya Kwiritana)—2024
  • Ĩthĩrwa na Nkuma ya Ũngʼanĩĩru Kwerekera Mantũ Jarĩa Ũtiijĩ
    Mũkaria Ĩrĩa Ĩtũmagĩria Ũnene Bwa Jehova (Ngacĩti ya Kwiritana)—2025
  • Rĩ, Nwithuranĩrĩte Nĩkenda Ũbatithua?
    Gwĩrĩrua Ũtũũro Kenya na Kenya!—Kwiritana Bibiria na Njĩra ya Kwaranĩria
See More
Mũkaria Ĩrĩa Ĩtũmagĩria Ũnene Bwa Jehova (Ngacĩti ya Kwiritana)—2025
w25 Machi tũr. 2-7

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA GĨA 9

RWĨMBO 51 Tumejiweka Wakfu kwa Mungu!

Menya Ũtĩĩria Kũbatithua

“Nandi nimbi weteerete? Ukiira ubatithue.”—MATH. 22:16.

JAMBO KUU

Pata nguvu unazohitaji ili kufikia hatua ya kubatizwa kwa kuchunguza mfano wa Wasamaria, Sauli wa Tarso, Kornelio, na Wakorintho.

1. Tũrĩna itũmi birĩkũ bibiega bia gũtũma tũbatithua?

JE, UNAMPENDA Yehova Mungu, ambaye amekupatia kila zawadi njema, kutia ndani uhai? Je, ungependa kumwonyesha upendo wako? Njia bora ya kufanya hivyo ni kujiweka wakfu kwake na kuonyesha wakfu wako kupitia ubatizo. Unapofanya hivyo, unakuwa sehemu ya familia ya Yehova. Matokeo ni kwamba Yehova, Baba na Rafiki yako, atakuongoza na kukutunza kwa sababu wewe ni mali yake. (Zab. 73:24; Isa. 43:​1, 2) Pia, kujiweka wakfu na kubatizwa kunakupatia tumaini la kufurahia uzima wa milele.—1 Pet. 3:21.

2. Nĩmbi tũkaarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ?

2 Je, kuna jambo linalokufanya usite kubatizwa? Ikiwa ndivyo, hauko peke yako. Mamilioni ya watu waliokutangulia, walihitaji kufanya mabadiliko katika mwenendo wao na njia yao ya kufikiri ili wastahili kubatizwa. Sasa wanamtumikia Yehova kwa bidii na shangwe. Unaweza kujifunza nini kutoka kwa wale waliobatizwa katika karne ya kwanza? Tutachunguza baadhi ya changamoto walizokabili na mambo tunayoweza kujifunza kutokana na mfano wao.

ASAMARIA NĨBABATITHĨRUE

3. Kwombĩka nĩ mantũ jarĩkũ jamoomũ Asamaria bamwe baakũrũkĩĩrĩre mbere ya kũbatithua?

3 Wasamaria katika siku za Yesu walikuwa washiriki wa kikundi cha kidini kilichokuwa karibu na majiji ya kale ya Shekemu na Samaria, kaskazini mwa Yudea. Kabla ya kustahili kubatizwa, Wasamaria walihitaji kujifunza kikamili zaidi kuhusu Neno la Mungu. Wasamaria walikubali kwamba vitabu vitano tu vya kwanza vya Biblia, yaani, Mwanzo hadi Kumbukumbu la Torati, viliongozwa na roho, na huenda pia kitabu cha Yoshua. Hata hivyo, Wasamaria walitarajia kwamba Masihi angekuja, kulingana na ahadi ya Mungu inayopatikana kwenye Kumbukumbu la Torati 18:​18, 19. (Yoh. 4:25) Ili wabatizwe, walihitaji kumkubali Yesu kuwa Masihi aliyeahidiwa. “Wasamaria wengi” walifanya hivyo. (Yoh. 4:39) Huenda wengine walihitaji kushinda ubaguzi uliokita mizizi kati ya Wasamaria na Wayahudi.—Luka 9:​52-54.

4. Kũringana na Mathithio 8:​5, 6, 14, nĩatĩa Asamaria bamwe bathithĩrie barĩkwigua ntũmĩĩri ya Filipo?

4 Ni nini kilichowasaidia Wasamaria kubatizwa? Filipo mweneza-injili alipohubiri “kumhusu Kristo,” baadhi ya Wasamaria ‘walikubali neno la Mungu.’ (Soma Matendo 8:​5, 6, 14.) Walikubali kumsikiliza Filipo ingawa alikuwa Myahudi. Huenda walikumbuka mistari katika Pentateuki iliyosema kwamba Mungu hana ubaguzi. (Kum. 10:​17-19) Vyovyote vile, “[walikazia] fikira mambo ambayo Filipo alikuwa akisema” kumhusu Kristo, na waliona uthibitisho ulio wazi kwamba Filipo alikuwa akitegemezwa na Mungu. Pia, alikuwa akifanya ishara nyingi, kutia ndani kuwaponya wagonjwa na kufukuza roho waovu.—Mdo. 8:7.

5. Nĩmbi ũũmba kwiritana kuumania na Asamaria?

5 Wasamaria hao wangeweza kuruhusu ubaguzi au kutokuwa na ujuzi kuwazuie kufanya maendeleo. Lakini hawakuruhusu mambo hayo yawazuie. Wasamaria hawakukawia kubatizwa baada ya kusadiki kwamba Filipo alikuwa amewafundisha kweli. Simulizi la Biblia linasema hivi: “Walipomwamini Filipo, aliyekuwa akitangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu na kuhusu jina la Yesu Kristo, wanaume na pia wanawake wakabatizwa.” (Mdo. 8:12) Je, unasadiki kwamba Neno la Mungu ni kweli na kwamba Mashahidi wa Yehova wameshinda ubaguzi na wanajitahidi kuonyesha upendo wa kweli, unaowatambulisha Wakristo wa kweli? (Yoh. 13:35) Basi, chukua hatua mara moja, ukiwa na uhakika kwamba Yehova atakubariki.

6. Nĩatĩa ũũmba kũgunĩka kuumania na ngerekano ya Ruben?

6 Ruben, kutoka Ujerumani, alilelewa katika familia ya Mashahidi. Hata hivyo, alipokuwa kijana alikuwa na shaka kuhusu kuwapo kwa Yehova. Alishindaje shaka hizo? Alipotambua kwamba hakuwa na ujuzi wa kutosha, aliamua kujifunza zaidi. Alisema hivi: “Katika funzo langu la kibinafsi, nilihitaji kujifunza habari sahihi kuhusu shaka nilizokuwa nazo. Nilihitaji kujifunza habari kuhusu mageuzi mara kadhaa.” Alisoma kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? Chapisho hilo lilimsaidia sana Ruben. Alijiambia hivi: ‘Kwa kweli! Yehova ni halisi.’ Na alipotembelea makao makuu ya ulimwenguni pote, Ruben alithamini zaidi undugu wetu wa kimataifa wenye umoja ambao ni muujiza. Aliporudi Ujerumani, Ruben alibatizwa akiwa na umri wa miaka 17. Ikiwa una shaka kuhusu mambo uliyojifunza, fanya utafiti katika machapisho yetu. Shaka zinaweza kushindwa kwa kupata “ujuzi sahihi.” (Efe. 4:​13, 14) Na kadiri unavyosikia ripoti kuhusu upendo na umoja miongoni mwa watu wa Yehova katika sehemu nyingine za ulimwengu na kujionea hilo katika kutaniko lenu, uthamini wako kuelekea undugu wa ulimwenguni pote utaongezeka.

SAŨLŨ WA TARISO ARABATITHUA

7. Nĩ mwonere jũrĩkũ Saũlũ abataraga kũgarũra?

7 Fikiria mfano wa Sauli wa Tarso. Alikuwa anafanya maendeleo mazuri katika dini ya Kiyahudi na alikuwa na ujuzi mwingi katika Sheria za Kiyahudi. (Gal. 1:​13, 14; Flp. 3:5) Wakati huo, Wayahudi wengi waliamini kwamba Wakristo walikuwa waasi-imani, hivyo Sauli aliwatesa sana. Alifikiri kimakosa kwamba alikuwa akifanya mapenzi ya Mungu. (Mdo. 8:3; 9:​1, 2; 26:​9-11) Ili kumkubali Yesu na kubatizwa, na kuwa Mkristo, Sauli mwenyewe alihitaji kuwa tayari kuteswa.

8. (a) Nĩmbi biatetherie Saũlũ nĩkenda abatithua? (b) Kũringana na Mathithio 22:​12-16, nĩatĩa Anania aatetherie Saũlũ? (Tega kinya mbica.)

8 Ni nini kilichomsaidia Sauli kubatizwa? Bwana Yesu aliyetukuzwa alipomtokea Sauli, Sauli alipofushwa. (Mdo. 9:​3-9) Kwa siku tatu, Sauli alifunga na bila shaka alitafakari kuhusu mambo hayo yaliyompata. Naam, Sauli akasadiki kwamba Yesu alikuwa Masihi na kwamba wafuasi wake walikuwa katika dini ya kweli. Ni lazima Sauli alihisi hatia sana kwa kushiriki katika kumuua Stefano! (Mdo. 22:20) Mwishoni mwa siku hizo tatu, kwa fadhili mwanafunzi aliyeitwa Anania alimfuata Sauli, akamponya upofu wake, na kumtia moyo abatizwe bila kukawia. (Soma Matendo 22:​12-16.) Kwa unyenyekevu, Sauli alikubali msaada huo na kuanza njia mpya ya maisha.—Mdo. 9:​17, 18.

Sauli akiingia ndani ya maji ili abatizwe. Watu wachache wanamtazama kwa furaha.

Je, utakubali kitia-moyo cha kubatizwa kama Sauli alivyofanya? (Tazama fungu la 8)


9. Nĩmbi ũũmba kwiritana kuumania na Saũlũ?

9 Kuna mambo ambayo tunaweza kujifunza kutoka kwa Sauli. Angeweza kuruhusu kiburi au kuwaogopa wanadamu kumzuie kubatizwa. Lakini hakuruhusu hayo yamzuie. Kwa unyenyekevu, Sauli alibadili njia yake ya maisha alipokubali kweli kumhusu Kristo. (Mdo. 26:​14, 19) Sauli alikuwa tayari kukubali kuwa Mkristo ingawa alijua kwamba angeteswa. (Mdo. 9:​15, 16; 20:​22, 23) Baada ya kubatizwa, aliendelea kumtegemea Yehova ili amsaidie kuvumilia majaribu mbalimbali. (2 Kor. 4:​7-10) Utakapobatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova, huenda ukakabili majaribu ya imani, lakini utapata msaada. Unaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu na Kristo hawatashindwa kukutegemeza.—Flp. 4:13.

10. Nĩmbi tũkwiritana kuumania na ngerekano ya Anna?

10 Anna alilelewa katika familia ya Wakurdi huko Ulaya Mashariki. Baada ya mama yake kubatizwa, Anna alianza kujifunza Biblia akiwa na umri wa miaka 9 baada ya kupata ruhusa kutoka kwa baba yake. Hata hivyo, hilo lilitokeza matatizo na watu wao wa ukoo, ambao walikuwa wakiishi pamoja na familia yao. Watu hao wa ukoo waliona kuwa ni jambo la aibu kwa mtu kubadili dini ya familia na kuwa Shahidi. Anna alipokuwa na umri wa miaka 12, alimwomba baba yake ruhusa ili abatizwe. Baba yake alitaka kujua ikiwa huo ulikuwa uamuzi wake mwenyewe au ikiwa alikuwa akishinikizwa na mtu. Anna alimjibu, “Ninampenda Yehova.” Basi baba yake akakubali abatizwe. Baadaye, watu wa ukoo wa Anna waliendelea kumdhihaki na kumtendea kwa njia isiyofaa. Mmoja wao alimwambia hivi: “Ni afadhali ungekuwa unaishi maisha mapotovu kimaadili na kuvuta sigara kuliko kuwa Shahidi wa Yehova.” Anna alikabilianaje na hali hiyo? Anasema hivi: “Yehova alinisaidia kuwa imara, na mama na baba yangu walinisaidia sana.” Anna ameandika orodha ya pindi hususa ambazo Yehova amemsaidia maishani mwake. Mara kwa mara, anaipitia ili asisahau jinsi Yehova alivyomsaidia. Ikiwa unaogopa kwamba utateswa, kumbuka kwamba Yehova atakusaidia wewe pia.—Ebr. 13:6.

KORINELIO ARABATITHUA

11. Korinelio aarĩ muntũ ũkari atĩa?

11 Biblia inataja pia mfano wa Kornelio. Alikuwa “ofisa aliyesimamia wanajeshi 100” wa jeshi la Roma. (Mdo. 10:​1, maelezo ya chini) Kwa sababu ya cheo chake, huenda aliheshimiwa sana katika jamii na jeshi. Pia, Biblia inataja kwamba “aliwapa watu zawadi nyingi za rehema.” (Mdo. 10:2) Yehova alimtuma mtume Petro aende kumtangazia habari njema. Je, Kornelio alikawia kubatizwa kwa sababu ya cheo chake?

12. Nĩmbi biatetherie Korinelio nĩkenda abatithua?

12 Ni nini kilichomsaidia Kornelio kubatizwa? Tunasoma kwamba “[alimwogopa] Mungu, yeye pamoja na watu wote wa nyumba yake.” Na Kornelio aliomba dua sikuzote kwa Mungu. (Mdo. 10:2) Petro alipomtangazia Kornelio habari njema, yeye na familia yake walimkubali Kristo, na wakabatizwa bila kukawia. (Mdo. 10:​47, 48) Bila shaka, Kornelio alikuwa tayari kufanya mabadiliko yoyote yaliyohitajika ili yeye na familia yake waweze kumwabudu Yehova.—Yos. 24:15; Mdo. 10:​24, 33.

13. Nĩmbi ũũmba kwiritana kuumania na Korinelio?

13 Kama Sauli, Kornelio angeweza kuruhusu cheo chake kimzuie kuwa Mkristo. Lakini hakuruhusu jambo hilo limzuie. Je, utahitaji kufanya mabadiliko makubwa maishani mwako ili ustahili kubatizwa? Ikiwa ndivyo, Yehova atakuwa Msaidizi wako. Atabariki azimio lako la kumtumikia kulingana na kanuni za Biblia.

14. Nĩmbi tũkwiritana kuumania na ngerekano ya Tsuyoshi?

14 Tsuyoshi, kutoka Japani, alihitaji kufanya mabadiliko katika kazi yake ili astahili kubatizwa. Alikuwa msaidizi wa mwalimu mkuu wa shule ya Ikenobo ya ufundi wa kupanga maua. Mwalimu mkuu aliposhindwa kuhudhuria mazishi fulani, mara nyingi Tsuyoshi alimwakilisha katika desturi za mazishi za Kibudha. Hata hivyo, Tsuyoshi alipojifunza ukweli kuhusu kifo, alijua kwamba hangeweza kustahili kubatizwa ikiwa angeendelea kushiriki katika desturi hizo za mazishi. Hivyo, aliamua kutoshiriki katika desturi hizo za Kibudha. (2 Kor. 6:​15, 16) Tsuyoshi alimwambia mwalimu mkuu kuhusu jambo hilo. Matokeo yalikuwaje? Tsuyoshi aliweza kuendelea na kazi yake bila kushiriki katika desturi hizo. Alibatizwa mwaka mmoja hivi baada ya kuanza kujifunza Biblia.a Ikiwa utahitaji kubadili jambo fulani katika kazi yako ili umpendeze Mungu, uwe na uhakika kwamba atakuandalia mahitaji yako na ya familia yako.—Zab. 127:2; Mt. 6:33.

AKORINTHO BARABATITHUA

15. Nĩ mantũ jarĩkũ jamoomũ Akorintho baakurukĩĩrĩre mbere ya kũbatithua?

15 Watu katika jiji la kale la Korintho walijulikana kwa kupenda mali na kuwa na maadili mapotovu. Watu wengi huko walifanya mambo ambayo hayakumpendeza Mungu. Ni wazi kwamba hali hizo zilifanya iwe vigumu kwa mtu yeyote kukubali habari njema. Hata hivyo, mtume Paulo alipofika katika jiji hilo na kuwahubiria habari njema kumhusu Kristo, “Wakorintho wengi waliosikia wakaanza kuamini na kubatizwa.” (Mdo. 18:​7-11) Kisha, Bwana Yesu Kristo akamtokea Paulo katika maono na kumwambia hivi: “Nina watu wengi katika jiji hili.” Hivyo, Paulo akaendelea kuhubiri huko kwa mwaka mmoja na nusu.

16. Nĩmbi biatetherie Akorintho bamwe gũciinda mantũ jamoomũ jarĩa baakurukagĩĩra mbere ya kũbatithua? (2 Akorintho 10:​4, 5)

16 Ni nini kilichowasaidia Wakorintho kubatizwa? (Soma 2 Wakorintho 10:​4, 5.) Neno la Mungu na roho yake takatifu yenye nguvu, iliwasaidia kufanya mabadiliko makubwa maishani mwao. (Ebr. 4:12) Watu katika jiji la Korintho waliokubali habari njema kumhusu Kristo, waliweza kuacha tabia na mazoea kama vile ulevi, wizi, na ngono kati ya watu wa jinsia moja.—1 Kor. 6:​9-11.b

17. Nĩmbi ũũmba kwiritana kuumania na antũ ba Korintho?

17 Ona kwamba ingawa baadhi ya Wakorintho walihitaji kushinda tabia zilizokita mizizi, hawakufikia mkataa kwamba ingekuwa vigumu sana kwao kuwa Wakristo. Walijitahidi sana ili kuingia katika barabara yenye nafasi ndogo inayoongoza kwenye uzima. (Mt. 7:​13, 14) Je, unapambana ili kushinda tabia au zoea lisilofaa ili ustahili kubatizwa? Kamwe usikate tamaa! Msihi Yehova akupatie roho yake takatifu ili ikusaidie kushinda tamaa mbaya.

18. Nĩmbi tũkwiritana kuumania na ngerekano ya Monika?

18 Monika, kutoka nchini Georgia, alijitahidi sana kuacha kutumia lugha chafu na burudani isiyofaa ili aweze kustahili kubatizwa. Alisema hivi: “Nilipokuwa tineja, niliimarishwa sana na sala. Yehova alijua kwamba nilitaka kufanya jambo lililo sawa na sikuzote alinisaidia na kuniongoza.” Monika alibatizwa alipokuwa na umri wa miaka 16. Je, kuna mazoea ambayo unahitaji kuacha ili umtumikie Yehova kwa njia anayoikubali? Endelea kumwomba ili akupatie nguvu za kufanya mabadiliko. Yehova anatupatia kwa ukarimu roho yake takatifu.—Yoh. 3:34.

WĨTĨKIO BWAKU BWOMBA GWĨTAĨTITHIA IRĨMA

19. Nĩmbi biũmba gũgũtethia gũciinda mantũ jamoomũ jarĩa jakari ta irĩma? (Tega kinya mbica.)

19 Uwe na uhakika kwamba Yehova anakupenda na anataka uwe sehemu ya familia yake. Hilo ni kweli, haidhuru unakabili changamoto gani unapojitahidi kustahili kubatizwa. Yesu alikiambia kikundi cha wanafunzi wake wa karne ya kwanza hivi: “Mkiwa na imani inayolingana na mbegu ya haradali, mtauambia mlima huu, ‘Ondoka hapa uende pale,’ nao utaondoka, na hakuna jambo litakalowashinda.” (Mt. 17:20) Wanafunzi waliosikia maneno hayo walikuwa pamoja na Yesu kwa miaka michache tu, hivyo imani yao ilihitaji kukua. Lakini Yesu aliwahakikishia kwamba ikiwa wangesitawisha imani ya kutosha, Yehova angewasaidia kuondoa changamoto zilizokuwa kama milima. Yehova atakusaidia wewe pia kufanya hivyo!

Kikundi cha ndugu na dada wenye furaha wakiwa kwenye kusanyiko la eneo, wanapiga makofi huku wale waliotoka kubatizwa wakipita.

Uwe na uhakika kwamba Yehova anakupenda na anataka uwe sehemu ya familia yake (Tazama fungu la 19)c


20. Nĩatĩa ngerekano cia Akristũ ba karine ya mbere na ba ntukũne cietũ irĩa irĩ kĩthoomone gĩkĩ igũgwĩkĩra inya?

20 Ikiwa umetambua changamoto fulani zinazokuzuia kubatizwa, chukua hatua mara moja ili kuzishughulikia. Pata faraja na nguvu kupitia mifano ya Wakristo wa karne ya kwanza na wa siku zetu. Na mifano yao ikutie moyo na kukuchochea kujiweka wakfu na kubatizwa. Huo ni uamuzi bora zaidi utakaowahi kufanya!

NĨMBI WAIRITANA KUUMANIA NA AKRISTŨ BABA BA KARINE YA MBERE BWEGIE GŨCIINDA MANTŨ JAMOOMŨ MBERE YA KŨBATITHUA?

  • Asamaria

  • Saũlũ wa Tariso na Korinelio
  • Akorintho

RWĨMBO 38 Atakupa Nguvu

a Simulizi la maisha la Ndugu Tsuyoshi Fujii, linapatikana katika gazeti la Amkeni! la Agosti 8, 2005, uku. 20-23.

b Tazama video yenye kichwa ‘Kwa Nini Unasita Kubatizwa?’ kwenye jw.org.

c MAELEZO YA PICHA: Kikundi cha ndugu na dada wakiwakaribisha kwa uchangamfu waliotoka kubatizwa.

    Mauku ja Kĩmĩĩrũ (2012-2025)
    Log Out
    Log In
    • Kĩmĩĩrũ
    • Share
    • Preferences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Terms of Use
    • Privacy Policy
    • Privacy Settings
    • JW.ORG
    • Log In
    Share