KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA GĨA 19
RWĨMBO 6 Mbingu Zatangaza Utukufu wa Mungu
Igerekanie na Araĩka Barĩa Eetĩkĩkua
“Buĩ araĩka . . . kumagieni Mwathani.”—ZB. 103:20; Kimeru Bible, 2010.
JAMBO KUU
Masomo tunayoweza kujifunza kutokana na mfano wa malaika waaminifu.
1-2. (a) Nĩ na njĩra ĩrĩku tũrĩ mwanya na araĩka? (b) Nĩ na njĩra ĩrĩku tũngʼuanene na araĩka?
YEHOVA alipokuvuta kwenye kweli, alikualika ujiunge na familia yake yenye upendo ya waabudu wake wanaotoka ulimwenguni pote, inayotia ndani mamilioni ya malaika waaminifu. (Dan. 7:9, 10) Tunapofikiria kuhusu malaika, huenda tukafikiria jinsi walivyo tofauti na sisi. Kwa mfano, malaika wameishi kwa muda mrefu zaidi kuliko sisi. (Ayu. 38:4, 7) Wana nguvu nyingi kuliko sisi. Nao ni watakatifu na waadilifu kwa kiwango ambacho hatuwezi kukifikia tukiwa wanadamu wasio wakamilifu.—Luka 9:26.
2 Hata hivyo, licha ya tofauti hizo, kuna mambo mengi ambayo sisi na malaika tunafanana. Kwa mfano, tunaweza kuiga sifa nzuri za Yehova kama malaika wanavyofanya. Tuna uhuru wa kuchagua, kama malaika. Malaika wana majina ya kibinafsi, nyutu tofauti-tofauti, na majukumu mbalimbali kama sisi tu. Na tuna uhitaji wa kumwabudu Muumba wetu kama malaika wanavyofanya.—1 Pet. 1:12.
3. Nĩmbi tũũmba kwiritana kuumania na araĩka barĩa eetĩkĩkua?
3 Kwa kuwa kuna mambo mengi ambayo sisi na malaika tunafanana, mfano wao mzuri unaweza kututia moyo na kutufundisha. Kwa kweli, tunaweza kujifunza masomo mengi mazuri kutoka kwao. Katika makala hii, tutachunguza jinsi tunavyoweza kuiga unyenyekevu wa malaika hao waaminifu pamoja na upendo wao kwa watu, uvumilivu wao, na jitihada zao za kudumisha usafi wa kutaniko.
ARAĨKA NĨBETHAGĨRWA BARĨ NA NKUMA YA WINYIIA
4. (a) Nĩatĩa araĩka bonanagia nkuma ya winyiia? (b) Nĩkĩ araĩka bethagĩrwa na nkuma ya winyiia? (Zaburi 89:7)
4 Malaika waaminifu ni wanyenyekevu. Wanatii maagizo ya Yehova ingawa wana uzoefu mwingi, nguvu nyingi, na hekima. (Zab. 103:20) Wanapotimiza migawo yao, hawajivuni kamwe kuhusu mambo waliyotimiza au kujionyesha kuwa wana nguvu zinazopita za wanadamu. Wanafurahia kufanya mapenzi ya Mungu hata ikiwa wengine hawajui majina yao.a (Mwa. 32:24, 29; 2 Fal. 19:35) Wanakataa kupokea utukufu wowote ambao ni Yehova tu anastahili kupokea. Kwa nini malaika ni wanyenyekevu sana? Kwa sababu wanampenda Yehova na kumheshimu sana.—Soma Zaburi 89:7.
5. Nĩatĩa mũraĩka ũmwe oonanĩrie winyiia, rĩrĩa oonagĩĩria mũtũmwa Johana ĩatia rĩawe? (Tega kinya mbica.)
5 Fikiria simulizi moja linaloonyesha unyenyekevu wa malaika. Katika mwaka wa 96 W.K., malaika ambaye hakutajwa jina aliwasilisha maono yenye kustaajabisha kwa mtume Yohana. (Ufu. 1:1) Yohana alitendaje alipoona maono hayo? Alijaribu kumwabudu malaika huyo. Hata hivyo, kiumbe huyo wa roho mshikamanifu alimkataza mara moja, akisema: “Uwe mwangalifu! Usifanye hivyo! Mimi ni mtumwa mwenzako tu na wa ndugu zako . . . Mwabudu Mungu!” (Ufu. 19:10) Alijibu kwa unyenyekevu sana! Malaika huyo hakutaka kutukuzwa au kusifiwa. Papo hapo alimwambia Yohana amwabudu Yehova Mungu. Wakati huohuo, malaika hakumdharau Yohana. Ingawa malaika huyo alikuwa amemtumikia Yehova kwa muda mrefu sana na alikuwa na nguvu nyingi kuliko Yohana, kwa unyenyekevu alimwita Yohana mtumwa mwenzake. Na hata ingawa malaika huyo alihitaji kumrekebisha Yohana, hakumkemea au kumtendea mtume huyo aliyezeeka kwa ukali. Badala yake, malaika huyo alimtendea kwa fadhili. Huenda alitambua kwamba Yohana alifanya hivyo kwa sababu alistaajabishwa na mambo aliyoona.
Malaika alionyesha unyenyekevu alipokuwa akishughulika na Yohana (Tazama fungu la 5)
6. Nĩatĩa tũũmba kwigerekania na mũraĩka ũu wejĩrĩre mũtũmwa Johana?
6 Tunawezaje kuiga unyenyekevu wa malaika huyo? Sisi pia tunaweza kutimiza migawo yetu bila kujigamba au kutaka kutambuliwa kwa mambo tunayotimiza. (1 Kor. 4:7) Zaidi ya hilo, hatupaswi kujihisi sisi ni bora kuliko wengine ikiwa tumemtumikia Yehova kwa muda mrefu kuliko wao au ikiwa tuna mapendeleo fulani. Ukweli ni kwamba kadiri tunavyokuwa na mapendeleo mengi, ndivyo tunavyopaswa kujiona kuwa wadogo zaidi. (Luka 9:48) Kama malaika, tunataka kuwatumikia wengine. Hatutaki wengine wahisi kwamba sisi ni bora kuliko wao.
7. Nĩatĩa tũũmba kwonania winyiia, rĩrĩa tũkũbatara kwejana motaaro kana rĩrĩa tũkwoneeria muntũ ĩatia rĩawe?
7 Pia, tunaweza kuonyesha unyenyekevu ikiwa tunahitaji kumrekebisha au kumshauri mtu—iwe ni mwabudu mwenzetu au mtoto wetu. Tunapotoa shauri, huenda tukahitaji kuwa thabiti. Hata hivyo, kama malaika ambaye alimrekebisha Yohana kwa fadhili, tunaweza kuwa thabiti lakini bila kumfanya anayeshauriwa ahisi amevunjwa moyo. Ikiwa hatutajiona kuwa bora kuliko wengine, tutatoa shauri linalotegemea Biblia kwa njia ya heshima na upendo.—Kol. 4:6.
ARAĨKA NĨBENDETE ANTŨ
8. (a) Kũringana na Luka 15:10, nĩatĩa araĩka bonanagia nĩbendete antũ? (b) Nĩatĩa araĩka batũtethagia kĩrĩ ngũgĩ ya gũtũmĩria? (Tega kinya mbica karatacine ka mbere.)
8 Malaika hawajitengi na wanadamu. Wanawapenda wanadamu. Wanashangilia mtenda dhambi anapotubu, yaani, kondoo aliyepotea anapomrudia Yehova au mtu anapobadili njia zake na kuamua kumtumikia Yehova. (Soma Luka 15:10.) Pia, malaika wanatutegemeza tunapofanya kazi ya kuhubiri. (Ufu. 14:6) Ingawa hawawahubirii watu moja kwa moja, huenda wakamwongoza mhubiri kwa mtu anayetaka kujifunza kumhusu Yehova. Bila shaka, hatuwezi kusema kwa uhakika kwamba malaika wanahusika katika kisa fulani hususa. Pia, Yehova anaweza kutumia njia nyingine—kama vile roho yake takatifu—ili kuwasaidia watu au kuwaongoza watumishi wake. (Mdo. 16:6, 7) Hata hivyo, anawatumia malaika kwa njia kubwa. Basi tunapohubiri habari njema, tunaweza kuwa na uhakika kwamba malaika wako pamoja nasi ili kututegemeza.—Tazama sanduku “Sala Zao Zilijibiwa.”b
Wenzi wa ndoa wamemaliza tu mahubiri ya hadharani. Wakiwa njiani kuelekea nyumbani, dada anamwona mwanamke ambaye anaonekana ameshuka moyo. Dada huyo anatambua kwamba malaika wanaweza kutuongoza kwa watu ambao huenda wamekuwa wakitafuta msaada wa kiroho. Anachochewa kumwambia mwanamke huyo ujumbe wenye kufariji (Tazama fungu la 8)
9. Nĩatĩa tũũmba kwigerekania na wendo bwa araĩka kwerekera antũ?
9 Tunawezaje kuwaiga malaika na kuwaonyesha watu upendo? Tunaposikia tangazo kwamba mtu fulani amerudishwa kutanikoni, tunaweza kushangilia kama malaika wanavyofanya. Tunaweza kufanya yote tuwezayo ili kumkaribisha na kumhakikishia kwamba tunampenda. (Luka 15:4-7; 2 Kor. 2:6-8) Pia, tunaweza kuwaiga malaika kwa kuwa na bidii katika kazi ya kuhubiri. (Mhu. 11:6) Na kama tu ambavyo malaika wanatutegemeza tunapohubiri habari njema, sisi pia tunaweza kutafuta njia za kuwategemeza ndugu na dada katika huduma. Kwa mfano, je, tunaweza kufanya mipango ya kushiriki katika huduma na mhubiri asiye na uzoefu mwingi? Je, tunaweza kuwategemeza ndugu na dada waliozeeka au wagonjwa ili waweze kushiriki katika huduma?
10. Nĩmbi tũũmba kwiritana kuumania na ngerekano ya Sara?
10 Namna gani ikiwa hali zetu zinatuzuia kufanya yote tunayotamani kutimiza? Bado tunaweza kutafuta njia za kufanya kazi pamoja na malaika katika huduma. Fikiria mfano wa Sara,c dada aliye nchini India. Baada ya kufanya upainia kwa miaka 20, Sara alipata ugonjwa fulani na akashindwa kutoka kitandani. Inaeleweka kwamba alishuka moyo sana. Lakini kwa sababu ya kutegemezwa kwa upendo na familia yake ya kiroho na kusoma Biblia kwa ukawaida, hatua kwa hatua Sara akaanza kupata shangwe tena. Bila shaka, alihitaji kubadili njia yake ya kuhubiri ili ifaane na hali yake mpya. Kwa kuwa hakuweza hata kuketi ili aandike barua, angeweza tu kufanya mahubiri ya simu. Hivyo, aliwapigia simu watu ambao aliwahi kuwahubiria, nao walimwelekeza kwa watu ambao huenda wangependa kujifunza Biblia. Matokeo yalikuwa nini? Baada ya miezi michache, Sara alikuwa akiwafundisha Biblia watu 70—idadi ambayo hangeweza kuwafundisha peke yake! Hivyo, alikabidhi baadhi ya wanafunzi hao kwa watu wengine kutanikoni. Wengi kati ya wanafunzi hao wanahudhuria mikutano yetu. Ni lazima malaika wanafurahi sana kufanya kazi pamoja na ndugu na dada, kama vile Sara, ambao wanafanya yote wanayoweza katika kazi ya kuhubiri!
ARAĨKA NĨBONANAGIA NKUMA YA KŨŨMĨĨRIA
11. Nĩatĩa araĩka barĩa etĩkĩkua bonanĩtie nkuma ya kũũmĩĩria na njĩra ĩnene?
11 Malaika waaminifu ni mfano bora wa uvumilivu. Wamevumilia ukosefu wa haki na uovu kwa mamia ya miaka. Walimwona Shetani na viumbe wengine wa roho waliokuwa wakitumikia pamoja nao wakimwasi Yehova. (Mwa. 3:1; 6:1, 2; Yuda 6) Biblia inatuambia kuhusu malaika mwaminifu ambaye alipingwa moja kwa moja na roho mwovu mwenye nguvu. (Dan. 10:13) Zaidi ya hayo, katika historia yote ya wanadamu, malaika wamejionea watu wachache tu wakichagua kujiunga na ibada ya kweli. Licha ya mambo hayo yote, malaika hao waaminifu wanaendelea kumtumikia Yehova kwa shangwe na bidii. Wanajua kwamba kwa wakati unaofaa, Mungu ataondoa ukosefu wote wa haki.
12. Nĩmbi biũmba gũtũtethia kũũmĩĩria?
12 Tunawezaje kuiga uvumilivu wa malaika? Kama malaika, huenda tukatendewa isivyo haki au tukakabili upinzani. Lakini kama wao tunaamini kwamba Mungu ataondoa uovu wote. Hivyo, kama malaika waaminifu “[hatufi] moyo katika kufanya mema.” (Gal. 6:9) Na Mungu anaahidi kutusaidia kuvumilia. (1 Kor. 10:13) Tunaweza kumwomba Yehova roho yake takatifu, ambayo inatokeza subira na shangwe. (Gal. 5:22; Kol. 1:11) Namna gani ikiwa unakabili upinzani? Mtumaini Yehova kikamili, na usiogope. Sikuzote Yehova atakutegemeza na kukuimarisha.—Ebr. 13:6.
ARAĨKA NĨBAIRITANAGĨRIA GWĨKA KĨŨTHŨRANO KĨRĨ GĨKĨTHERU
13. Nĩ ngũgĩ ĩrĩkũ ya mwanya araĩka bathithagia ntukũne iji cia mũthia? (Mathayo 13:47-49)
13 Katika siku za mwisho, Yehova amewapatia malaika mgawo wa pekee. (Soma Mathayo 13:47-49.) Mamilioni ya watu ulimwenguni pote wanavutiwa na habari njema. Baadhi ya watu hao wanachukua hatua ya kubadili maisha yao ili wawe Wakristo wa kweli, lakini wengine hawafanyi hivyo. Malaika wamekabidhiwa mgawo wa “kuwatenganisha waovu kutoka kwa waadilifu.” Hilo linamaanisha kwamba wamepewa mgawo wa kusaidia kulinda usafi wa kutaniko. Lakini halimaanishi kwamba yeyote ambaye ameacha kushirikiana nasi kwa sababu yoyote ile hawezi kurudi kamwe; wala haimaanishi kwamba kamwe hakutakuwa na matatizo katika kutaniko. Hata hivyo, tunaweza kuwa na uhakika kwamba malaika wanafanya kazi kwa bidii ili kusaidia kudumisha usafi wa kutaniko.
14-15. Nĩatĩa tũũmba kwigerekania na araĩka, kĩrĩ kũmakĩra mantũ ja ũtheru bwa gĩkĩrundu na mĩtĩĩre ya wagĩru ndeene ya kĩũthũrano? (Tega kinya mbica.)
14 Tunawezaje kuiga jinsi malaika wanavyohangaikia usafi wa kutaniko? Kwa kufanya sehemu yetu ili kudumisha usafi wa kiadili na kiroho wa kutaniko letu. Ili kutimiza hilo, tunajitahidi kulinda moyo wetu kwa kuchagua marafiki wazuri na kukataa jambo lolote linaloweza kuharibu uhusiano wetu na Yehova. (Zab. 101:3) Pia, tunaweza kuwasaidia waabudu wenzetu waendelee kuwa waaminifu kwa Yehova. Kwa mfano, tunapaswa kufanya nini tukijua kwamba mwabudu mwenzetu ametenda dhambi nzito? Kwa sababu tunampenda mwabudu mwenzetu, tutamtia moyo azungumze na wazee. Asipofanya hivyo, tutawaeleza wazee kuhusu jambo hilo. Tungependa mwabudu mwenzetu ambaye ni dhaifu kiroho apate msaada haraka iwezekanavyo!—Yak. 5:14, 15.
15 Inasikitisha kwamba baadhi ya watu wanaofanya dhambi nzito wanahitaji kuondolewa kutanikoni. Jambo hilo linapotokea, ‘tunaacha kushirikiana’ nao.d (1 Kor. 5:9-13) Mpango huo unasaidia kudumisha usafi wa kutaniko. Zaidi ya hayo, tukiamua kutoshirikiana na watu walioondolewa kutanikoni, kwa kweli tunawaonyesha fadhili. Msimamo wetu thabiti huenda ukawachochea warudiwe na fahamu. Wakifanya hivyo, tunashangilia pamoja na Yehova na malaika wake.—Luka 15:7.
Tunapaswa kufanya nini tukijua kwamba mwabudu mwenzetu ametenda dhambi nzito? (Tazama fungu la 14)e
16. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ ũgaciũmia kwigerekania na araĩka?
16 Ni pendeleo kubwa sana kwamba Yehova ameturuhusu tujifunze kuhusu malaika na kufanya kazi pamoja nao! Acheni tuige sifa zao nzuri: unyenyekevu wao, upendo wao kwa wanadamu, uvumilivu wao, na jinsi wanavyohangaikia usafi wa kiadili na kiroho wa kutaniko. Ikiwa tutawaiga malaika hao waaminifu, sisi pia tunaweza kuwa sehemu ya familia ya waabudu wa Yehova kwa umilele wote.
RWĨMBO 123 Kutii Utaratibu wa Kitheokrasi Kwa Ushikamanifu
a Kati ya mamia ya mamilioni ya malaika, ni wawili tu wanaotajwa kwa majina katika Biblia—Mikaeli na Gabrieli.—Dan. 12:1; Luka 1:19.
b Unaweza kupata visa zaidi katika Fahirisi chini ya kichwa “Malaika” na kichwa kidogo “mwongozo wa malaika (visa mbalimbali).”
c Majina yamebadilishwa.
d Kama ilivyofafanuliwa kwenye Ripoti ya 2 ya Baraza Linaloongoza ya 2024, ikiwa mtu aliyeondolewa kutanikoni anafika kwenye mkutano, mhubiri anaweza kutumia dhamiri yake iliyozoezwa kuamua ikiwa atamsalimu kifupi na kumkaribisha.
e MAELEZO YA PICHA: Dada anamhimiza rafiki yake azungumze na wazee. Baada ya muda fulani kupita na rafiki yake anapokosa kuwaona wazee, dada huyo anawaeleza wazee kuhusu jambo hilo.