Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 37:35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Nao wanawe wote na binti zake wote wakawa wakiondoka ili kumfariji,+ lakini akawa akizidi kukataa kufarijiwa na kusema:+ “Kwa maana nitashuka kuingia katika Kaburi* nikimwombolezea mwanangu!” Na baba yake akaendelea kumlilia.

  • Hesabu 16:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Lakini ikiwa ni kitu fulani kilichoumbwa ambacho Yehova ataumba,+ nayo nchi ifungue kinywa chake na kuwameza+ na kila kitu kilicho chao, nao washuke chini wakiwa hai mpaka katika Kaburi,*+ ndipo hakika mtajua kwamba watu hawa wamemtendea Yehova bila heshima.”+

  • 1 Wafalme 2:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Nawe utende kulingana na hekima yako,+ na usiache mvi zake zishuke kwa amani+ katika Kaburi.*+

  • Zaburi 49:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kama kondoo, wao wamewekewa Kaburi;*+

      Kifo chenyewe kitawachunga;+

      Nao wanyoofu watawatawala asubuhi,+

      Nayo maumbo yao hayatakosa kuchakaa;+

      Kaburi* badala ya makao yaliyo juu ni kwa ajili ya kila mmoja.+

  • Zaburi 89:48
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 48 Ni mwanamume gani aliye hai ambaye hataona kifo?+

      Je, anaweza kuiokoa nafsi yake katika mkono wa Kaburi?*+ Sela.

  • Mhubiri 9:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Yote ambayo mkono wako unapata kufanya, yafanye kwa nguvu zako zote,+ kwa maana hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi+ wala hekima+ katika Kaburi,*+ mahali unapokwenda.+

  • Hosea 13:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 “Nitawakomboa wao kutoka katika mkono wa Kaburi;*+ nitawaokoa wao+ kutoka kwenye kifo. Ee Kifo, iko wapi michomo yako?+ Ee Kaburi,* yako wapi maangamizi yako?+ Huruma itafichwa kutoka machoni pangu.+

  • Matendo 2:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 kwa sababu hutaiacha nafsi yangu katika Kaburi,* wala hutamruhusu mshikamanifu wako aone uharibifu.+

  • Ufunuo 20:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Na bahari ikawatoa wale wafu waliokuwa ndani yake, na kifo na Kaburi* vikawatoa wale wafu+ waliokuwa ndani yake, nao walihukumiwa kila mmoja kulingana na matendo yake.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki