Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 14:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Na abarikiwe Mungu Aliye Juu Zaidi,+

      Ambaye amewatia wakandamizaji wako mkononi mwako!”+

      Kisha Abramu akampa sehemu ya kumi ya kila kitu.+

  • Mwanzo 28:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Na jiwe hili ambalo nimesimamisha kuwa nguzo litakuwa nyumba ya Mungu,+ na katika kila kitu utakachonipa bila shaka nitakupa wewe sehemu ya kumi.”+

  • Hesabu 18:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 “Na kwa wana wa Lawi, tazama! nimewapa kila sehemu ya kumi+ katika Israeli iwe urithi wao kwa sababu ya utumishi wao wanaofanya, utumishi wa hema la mkutano.

  • Hesabu 18:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 “Na wewe utasema na Walawi, nawe utawaambia, ‘Mtapokea kutoka kwa wana wa Israeli sehemu ya kumi ambayo nimewapa ninyi kutoka kwao kwa ajili ya urithi wenu,+ nanyi mtatoa mchango wenu kutoka katika hiyo uwe mchango kwa Yehova wa sehemu ya kumi ya hiyo sehemu ya kumi.+

  • Kumbukumbu la Torati 12:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Na hapo mtaleta matoleo yenu ya kuteketezwa na dhabihu+ zenu na sehemu zenu za kumi+ na mchango wa mkono wenu+ na matoleo yenu ya nadhiri+ na matoleo yenu ya hiari+ na wazaliwa wa kwanza wa mifugo yenu na wa kundi lenu.+

  • Kumbukumbu la Torati 14:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 “Lazima utatoa sehemu ya kumi ya mazao yako yote ya mbegu yako, yanayotoka shambani mwaka baada ya mwaka.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 31:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Na mara tu lile neno lilipoenea, wana wa Israeli+ wakazidisha mazao ya kwanza ya nafaka,+ divai mpya,+ na mafuta+ na asali+ na mazao yote ya shamba,+ nao wakaleta kwa wingi sehemu ya kumi ya kila kitu.+

  • Nehemia 13:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Na Yuda wote wakaleta ndani ya maghala+ sehemu ya kumi+ ya nafaka+ na ya divai mpya+ na ya mafuta.+

  • Malaki 3:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Leteni ghalani sehemu zote za kumi,+ ili kuwe na chakula nyumbani mwangu;+ nanyi, tafadhali, mnijaribu kwa njia hii,”+ Yehova wa majeshi amesema, “kama sitawafungulia ninyi malango ya mbinguni+ na kuwamwagia baraka hata kusiwe na uhitaji tena.”+

  • Luka 11:42
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 42 Lakini ole wenu ninyi Mafarisayo, kwa sababu ninyi hutoa sehemu ya kumi+ ya mnanaa na mchicha na ya kila mboga nyingine za majani, lakini ninyi hupuuza haki na upendo kwa Mungu! Mambo hayo mlikuwa na wajibu wa kuyafanya, na bado kutoyaacha yale mengine.+

  • Waebrania 7:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Ni kweli, watu kutoka katika wana wa Lawi+ ambao hupokea cheo chao cha ukuhani wana amri ya kukusanya sehemu za kumi+ kutoka kwa watu+ kulingana na Sheria, yaani, kutoka kwa ndugu zao, hata kama hao wametoka katika viuno vya Abrahamu;+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki