7 “Usilitumie jina la Yehova Mungu wako kwa njia isiyofaa,+ kwa maana Yehova hatamwacha bila kuadhibiwa yule anayelitumia jina lake kwa njia isiyofaa.+
3 Mimi nami, nitauweka uso wangu juu ya mtu huyo, nami nitamkatilia mbali kutoka katikati ya watu wake,+ kwa sababu amempa Moleki baadhi ya uzao wake kwa kusudi la kupatia unajisi mahali pangu patakatifu+ na kulitia unajisi jina langu takatifu.+
20 Kwa hiyo wakaingia kwa mataifa ambamo waliingia, na watu wakatia unajisi jina langu takatifu+ kwa kusema hivi juu yao, ‘Hawa ndio watu wa Yehova, nao wametoka katika nchi yake.’+