Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 32:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Kwa hiyo akasema, ‘Acha niufiche uso wangu kutoka kwao,+

      Acha nione mwisho wao utakuwaje baadaye.

      Kwa maana wao ni kizazi chenye upotovu,+

      Wana ambao ndani yao hamna uaminifu.+

  • Ayubu 34:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Yeye mwenyewe anaposababisha utulivu, ni nani, basi, anayeweza kulaumu?

      Na anapoficha uso wake,+ ni nani anayeweza kumwona,

      Iwe ni kuelekea taifa+ au ni kuelekea mwanadamu, yote yakiwa ni mamoja?

  • Zaburi 27:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  9 Usinifiche uso wako.+

      Usimgeuzie mbali mtumishi wako kwa hasira.+

      Uwe msaada wangu.+

      Usinitupe wala usiniache, Ee Mungu wa wokovu wangu.+

  • Zaburi 104:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Ukiuficha uso wako, wanaingiwa na wasiwasi.+

      Ukiiondoa roho yao, wanakata pumzi,+

      Na kurudi katika mavumbi yao.+

  • Ezekieli 39:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Nayo mataifa yatalazimika kujua kwamba ilikuwa kwa sababu ya kosa lao kwamba wao, nyumba ya Israeli, walienda uhamishoni,+ kwa sababu walijiendesha kwa kukosa uaminifu kunielekea mimi, hivi kwamba nikawaficha wao uso wangu+ na kuwatia mkononi mwa wapinzani wao, nao wakawa wakianguka, wote hao, kwa upanga.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki