Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 2:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Na ikawa kwamba wakati wa siku hizo nyingi, mwishowe mfalme wa Misri akafa,+ lakini wana wa Israeli wakaendelea kuugua kwa sababu ya utumwa na kulia kwa kulalamika,+ nacho kilio chao cha kuomba msaada kikaendelea kupaa juu kwa Mungu wa kweli kwa sababu ya utumwa huo.+

  • 1 Samweli 9:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 “Karibu wakati kama huu kesho nitatuma mtu kwako kutoka katika nchi ya Benyamini,+ nawe umtie mafuta+ awe kiongozi juu ya watu wangu Israeli; naye atawaokoa watu wangu kutoka mkononi mwa Wafilisti,+ kwa sababu nimeona mateso ya watu wangu, kwa maana kilio chao kimenifikia.”+

  • Zaburi 18:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Katika taabu yangu niliendelea kumwita Yehova,

      Nami niliendelea kumlilia Mungu wangu kwa ajili ya msaada.+

      Kutoka katika hekalu lake aliisikia sauti yangu,+

      Nacho kilio changu cha msaada mbele zake sasa kikafika masikioni mwake.+

  • Zaburi 145:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Atawatimizia wale wanaomwogopa tamaa yao,+

      Naye atakisikia kilio chao cha kuomba msaada, naye atawaokoa.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki