12 “Na sasa, Ee Israeli, Yehova Mungu wako anataka nini kutoka kwako+ ila kumwogopa+ Yehova Mungu wako, ili kutembea katika njia zake zote+ na kumpenda+ yeye na kumtumikia Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote;+
17 Jifunzeni kutenda mema;+ tafuteni haki;+ mrekebisheni mkandamizaji;+ fanyeni hukumu kwa ajili ya mvulana asiye na baba;+ teteeni masilahi ya mjane.”+
3 Yehova amesema hivi: “Toeni haki na uadilifu, nanyi mumkomboe yeye anayenyang’anywa kutoka mkononi mwa mpunjaji; wala msimtendee vibaya mkaaji mgeni yeyote, mvulana asiye na baba au mjane.+ Msiwatendee jeuri yoyote.+ Wala msimwage damu yoyote isiyo na hatia mahali hapa.+
9 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Imetosha, enyi wakuu wa Israeli!’+
“ ‘Ondoeni jeuri na uporaji,+ na mfanye haki na uadilifu.+ Acheni kutumia uwezo vibaya kuchukua vitu vya watu wangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.