24 Baba, kwa habari ya kile ambacho umenipa, ninataka kwamba, mahali nilipo, wao pia wapate kuwa pamoja nami,+ ili wauone utukufu wangu ambao umenipa, kwa sababu ulinipenda kabla ya kuwekwa kwa msingi+ wa ulimwengu.+
17 Basi, ikiwa sisi ni watoto, sisi pia ni warithi: warithi wa Mungu kwelikweli, lakini warithi+ pamoja na Kristo, mradi tu tunateseka+ pamoja ili pia tutukuzwe pamoja.+
23 Niko chini ya mkazo kutokana na mambo haya mawili;+ lakini kile ninachotamani ni kule kufunguliwa na kule kuwa pamoja na Kristo,+ kwa maana hili, kwa hakika, ni bora zaidi.+
16 kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni+ akiwa na mwito wenye amri, kwa sauti ya malaika mkuu+ na kwa tarumbeta+ ya Mungu, na wale walio wafu katika muungano na Kristo watafufuliwa kwanza.+
8 Tangu wakati huu na kuendelea nimewekewa akiba ya taji la uadilifu,+ ambalo Bwana, aliye mwamuzi mwadilifu,+ atanipa kuwa thawabu+ katika siku ile,+ lakini si mimi tu, bali pia na wale wote ambao wamependa kufunuliwa kwake.